Jerry Muro na Zitto Kabwe, Something familiar

Jerry Muro na Zitto Kabwe, Something familiar

Anajiona kuwa yeye ndiye mwenye akili kuzidi watu wote.
 
Kama alifanya yeye kweli ulitaka aseme alifanya na nani? Acha wivu husio na mashiko. Hoja yako ingekuwa na mshiko kama ungeonesha wapi alisema nilifanya wakati walifanya wengi, otherwise ni majungu na siasa za maji taka!

mkuu acha kupanic,inamaana hmskii majukwaani akisema kauli kama hizo, "mimi nimeamua kukikuza chama mikoan pote" "mimi niliiangusha serikali ya awamu ya nne mara nne" "mimi natetea masilahi ya taifa" "mimi ni mzarendo" "mimi niliibua kashifa ya escrow,EPA,RICHMOND"
 
Siku akiiba yeye na akisema sisi tuliiba utakubali??????? kama amefanya yeye ni haki yake kusema mimi. Hawezi kusema sisi wakati ni yeye kwakuwa hata siku atakapoiba atakuwa ni mimi na sio sisi.
 
Siku akiiba yeye na akisema sisi tuliiba utakubali??????? kama amefanya yeye ni haki yake kusema mimi. Hawezi kusema sisi wakati ni yeye kwakuwa hata siku atakapoiba atakuwa ni mimi na sio sisi.

Uwe muelewa basi mambo mengine huwezi kufanya peke yako huo si uungwana
 
Ubinafsi huwa hauthamini watu wengine
 
Mimi ninafikiri deep down ni mdhaifu sana ndio maana anatumia nguvu nyingi kujishawishi kuwa he is good. Angalia watu anaozunguka nao, karibu wote ni wale waliochini yake iwe kielimu au kimaisha, hii inamuassure yeye binafsi kuwa yuko juu.
Anasikitisha
 
siku nyingine utakuja na "kwa nini zito anaenda chooni?", au "kwa nini zito amenilia vyangu?".
hata usemeje, umimi ni udhaifu mkubwa sana. A Y A T O L L A H Zitto ana ubinafsi, majivuno, na kiburi. Ndio maana anaona kila kitu ni yeye tu!!!

Huo ndio ukweli.
 
A selfish person acts superior to
others, putting his personal desires
above the needs of others. The
selfish person demonstrates no
consideration for other people's
feelings, nor does he care about
other people's thoughts or opinions.
Domineering and controlling
behaviors are prevalent with a selfish
person. He is typically self-serving
and self-involved.
 
Mimi ndio Mbunge pekee kijani niliyeiangusha Serikali mara 4, mimi ndiye Mbunge pekee niliyeweza kuwasilisha hoja binafsi zikaitikisa Serikali, mimi ndio mbunge pekee niliyefukuzwa na kupora chama cha watu, nikabadili katiba, nikajipa Cheo ninachotaka ndani ya siku 7.
 
Mimi ndio Mbunge pekee kijani niliyeiangusha Serikali mara 4, mimi ndiye Mbunge pekee niliyeweza kuwasilisha hoja binafsi zikaitikisa Serikali, mimi ndio mbunge pekee niliyefukuzwa na kupora chama cha watu, nikabadili katiba, nikajipa Cheo ninachotaka ndani ya siku 7.

hahaahahha kumbe aliiangusha serikali mara4 aliingia msituni nin labda serikali ya congo anasmea
mkuu umenuchekesha huo mstari wa pili hahahahha
 
Habari wanaUkumbi!
Nataka kuuliza kitu kimoja ambacho kimekua kikiendekezwa na wanasiasa wengi kama kete ya kutafuta huruma ya wanancni;
Ninamaanisha kua hizi sifa anapojisifia mtu kua ooh mimi ndiye niliyepipeleka hoja ya kuundwa tume ya uchunguzi bungeni, mimi ndiye niliyeandaa saini za kumng'oa waziri mkuu bungeni!Sijui mimi ndiye niliyesababisha baraza la mawairi kuvunjwa, mara Mimi ndiye niliyeibua ufisadi wa ESCROW!

SWALI; Sasa kama mtu alikua na nia ya kulisaidia taifa ni kwanini ajisifie muda wote mbele ya uma?Kwani wananchi hawalijui hilo? Kumbe inawezekana kila kitu anachokifinya bungeni hua anakiweka kibindoni kama mtaji wake wa baadaye na sio kulisaidia taifa, Kumbe wema wote wanaoufanya ni kwa ajili ya kuwauzia wananchi kwa kwa bie ya kupewa kura! Kumbe siku moja wananchi wakimuudhi atasusia kufanya hayo yote maana nis yake ilikua sio kwa ajili ya taifa!
Kwenu wanajamii tusaidiane juu ya hili kama lina maslahi na tija kwa taifa.
 
Thibitisha mkuu!!

Zitto ni mbinafsi sana.Wakati wenzake wanahangaika kwenye majimbo ya uchaguzi kupigia kampeni wagombea wa Chadema yeye haakuonaekana kabisa mfano jimbo la mbunge Nasari na kule Shinyanga.Je alikuwa wapi ? akumbuke Chadema imejengwa na wanachadema wote sio yeye tu na alijaribu kutaka kuibomoa akashindwa !

Yeye anasema mimi nilivunja Baraza la mawaziri.Je hizo taarifa mpaka akavunja alizitoa wapi ? mi nadahani yeye alikuwa msomaji tu wa taarifa aliefanya kazi kubwa na anas tahili sifa yule alietafuta taarifa hizo na kumpa huyo msemaji.

Zitto ni mbinafsi sana !
 
Sifa mojawapo ya kiongozi mbinafsi ni hiyo, matokeo chanya ya team hupenda kuona ni yeye ndio aliyasababisha; angalia kwa mfano Jerry Muro tokea ameondoka ITV bado kile kipindi cha report maalumu kinaendelea ingawa ndicho kilicho mpa umaarufu! Sina hakika kama Jerry Muro ameisha wahi kua kiongozi sehemu but with his age, siku 1 atakua so hili na liwe darasa kwake!
 
Ego is a b.i.t.c.h.Ogopa sana mtu yoyote anayependa kuweka "mimi" kwenye kila sentensi.ni ishara ya kujikweza, majivuno,ubinafsi,ubabe,ubaguzi na dharau.Ni dhambi kubwa sana mbele za Mungu.kwamba Zzk kuweza kufanya chochote ambacho anadai amewahi kukifanya kwa watanzania pasingekuwa na viongozi/watu wengine aingefanikiwa.kwamba hakuna chochote ambacho amekifanya pasipo ushirikiano na watu wengine mfano,viongozi wenzake wa chadema,wanakamati wengine kwenye poac na pac,baadhi ya members wa ccm,nk.hivyo anavyoleta umimi ni wazi kabisa amewadharau wale wote waliochangia kwa njia moja au nyingine mafanikio yake.na hii dharau ni mpaka kwa wale wananchi wote tuliompa support na kumuunga mkono kipindi hicho.Akumbuke tu kwamba "mpanda ngazi hushuka" na " tutavuna tulichokipanda"...
 
Sifa mojawapo ya kiongozi mbinafsi ni hiyo, matokeo chanya ya team hupenda kuona ni yeye ndio aliyasababisha; angalia kwa mfano Jerry Muro tokea ameondoka ITV bado kile kipindi cha report maalumu kinaendelea ingawa ndicho kilicho mpa umaarufu! Sina hakika kama Jerry Muro ameisha wahi kua kiongozi sehemu but with his age, siku 1 atakua so hili na liwe darasa kwake!

Kwani kile cheo alichonacho pale Yanga cha mdomo mali yake sio sehemu ya uongozi Mkuu..? :A S-coffee:
 
Jerry amesema anataka ubunge na alikuwa anasema sifa zake ambazo
hakuna anaeweza kuzi verify
mfano ni lini alitangazwa kuwa ni 'mwanahabari wa mfano'?
alitangazwa na nani?

ni kweli ni mwanahabari mchapakazi ..lakini titles na masifa angeacha wengine waseme

na wala hizo title na masifa hazim halalishi kuwa mbunge

Zitto the same..ni kweli alisababisha baraza la mawaziri livunjwe but hakusaidiwa?
hizo sign 70 zote hazina maana kwake?
angepungua nini kama angesema 'tulisababisha baraza la mawaziri kuvunjwa'?

Malkia Elizabeth anaposema 'we' unafikiri kuna malkia wangapi UK?
lugha ya uongozi ni sisi na we

Kaka kwa vile kuna watu bado wameonyesha kutokuelewa mukhtadha wa hoja yako, basi tambua kuwa yule adui ujinga kina Nyerere walimsema dawa yake haijapatikana...

Mtu hawezi kuwa kiongozi [namaanisha anayeongoza wengine sio msaka fursa] kama umejaa Umimi.
 
Jana niliona mahojiano kidogo ya Jerry Muro kwenye kipindi cha MKASI EATV ambacho kikubwa nilichokiona kwa Jerry Muro ni 'entitlement feelings' alizo nazo

Ingawa kiukweli anaonekana ni mzalendo na anaipenda nchi yake na pengine anastahili
kupewa nafasi zaidi lakini kila anapofungua mdomo utamsikia akisema 'mimi nilifanya hivi' 'mimi nilifanya vile'.

Kuna kipindi alisema 'mimi nilikuwa mwanahabari wa mfano Tanzania' nikabaki najiuliza hiyo status alipewa na nani? ni lini alitangazwa wa mfano?

Nafikiri tatizo la Jerry Muro ni hilo....'kutwa anasema 'mimi' 'mimi'

Siku ile Zitto anatangaza kujiunga na ACT-Wazalendo kutwa alikuwa anasema 'mimi nilisababisha baraza la mawaziri livunjwe' 'mimi nilisababisha hiki na kile.

Ingawa yote aliyoyasema naamini yana kitu chenye ukweli but kumsikia kiongozi kutwa akisema 'mimi lilifanya hivi' 'mimi nilifanya vile' it is so irritating...

Lugha ya uongozi ni 'we' ....'sisi'

Naamini humu kuna washauri wengi wa Zitto na Jerry Muro. Waambieni tu kama wanataka kufanikiwa waache sasa hiyo lugha ya 'mimi nilifanya hivi' na waanze leo kusema 'sisi' na kutumia 'we' badala ya 'i' kwenye matamshi yao.

Ni kitu kidogo sana lakini kikuubwa sana.

agustino lytonga mrema mpaka Leo sera yake ni mm nilikuwa mm nilikuwa
 
Back
Top Bottom