Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 4,449
- 10,761
Nawasalimu kwa salaam yetu pendwa toka kwa mama yetu. Kwa wenzangu na mimi ambao tumewahi kupita chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa kusoma ama kutembea tu kuna maajabu yapo katika jengo la Utawala.
Ukiingia kwenye jengo hilo ndio utaweza kumuelewa yule member wa humu ambaye mara nyingi utumia kauli ya SHULENI UWA MNAAENDA KUJIFUNZA UJINGA!
Hauwezi kuamini hili jengo lina ofisi za wasomi wabobezi na waandamizi na wakiwa wanaaminiwa na nchi hii. Chakuchekesha ukipanda kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka ya tatu ni hovyo sana, hazipo katika umaridadi.
Ukianza kupanda ghorofa ya Nne unapigwa na butwaa, chini imewekwa malumalu na milango ya vioo ukweli inapendeza hapo ndio zipo ofisi za wazito wa UDSM.
Cha kujiuliza hawa wasomi wetu wapo tayari kupita sehemu chafu kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka ya tatu ila ya nne ni safi.
Na muda wa kushuka atashuka kuanzia ghorofa safi akizipita ghorofa chafu. Ndio hapo unajiuliza hawa wasomi wetu walienda shule kujifunza ujinga ama. Rekebisheni jengo lote hilo.
Ukiingia kwenye jengo hilo ndio utaweza kumuelewa yule member wa humu ambaye mara nyingi utumia kauli ya SHULENI UWA MNAAENDA KUJIFUNZA UJINGA!
Hauwezi kuamini hili jengo lina ofisi za wasomi wabobezi na waandamizi na wakiwa wanaaminiwa na nchi hii. Chakuchekesha ukipanda kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka ya tatu ni hovyo sana, hazipo katika umaridadi.
Ukianza kupanda ghorofa ya Nne unapigwa na butwaa, chini imewekwa malumalu na milango ya vioo ukweli inapendeza hapo ndio zipo ofisi za wazito wa UDSM.
Cha kujiuliza hawa wasomi wetu wapo tayari kupita sehemu chafu kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka ya tatu ila ya nne ni safi.
Na muda wa kushuka atashuka kuanzia ghorofa safi akizipita ghorofa chafu. Ndio hapo unajiuliza hawa wasomi wetu walienda shule kujifunza ujinga ama. Rekebisheni jengo lote hilo.