Jenerali Ulimwengu, kumbe hata wewe ni mnafiki!

Jenerali Ulimwengu, kumbe hata wewe ni mnafiki!

dilemma

Umesema vizuri sana. Mpaka sasa mtu asiyefahamu kuwa CCM inapaswa kuondoka madarakani kwa gharama yeyote ile ni mwehu, mjinga, mwenye akili finyu na asiyejitambua. Hata kama bado analamba masufuria ya ufisadi ajue kabisa historia itamuhukumu. Hata aje Malaika hataweza kuongoza vema ndani ya mfumo ovyoo ulioota mizizi mingi na mirefu ndani ya CCM kwa zaidi ya nusu karne sasa. Atatumikia tu mfumo huu wa kishenzi na kishetani. CCM must go and gradually disappear from world's surface kama KANU. Vyama vilivyopigania Uhuru havina maana tena katika harakati za ukombozi wa kiuchumi wa nchi husika. Badala yake vimekuwa vikwazo na laana ya maendeleo. Lazima CCM ing'oke. Muda wa kung'oka ni sasa, ni Oktoba 2015.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kumsafisha Lowasa hadharani ni kazi kweli kweli hasa kwa kuwa yeye mwenyewe hataki hata kutamka neno FISADI! Nadhani timu ya kampeni ya Ukawa wako humu. Wamlazimishe lowasa kuokoka na kukemea ufisadi hadharani na atoe tamko kuwa atakuwa kama Zakayo wa biblia aliyeongoka na kurudisha Mali yote ya dhuluma. Lowasa alazimishwe kutamka mali zake zote hadharani na alivyozipata ndipo wagombea wetu wa ubunge na udiwani wataweza kuendeleza agenda ya kutokomeza ufisadi kwenye kampeni. Lowasa pia aseme wazi wazi kuwa ataitekeleza sera ya chadema ya kuwapeleka mafisadi wote mahakamani endapo atakuwa rais. Kama hana ujasiri huo Ukawa kwisha.

Unastahili like mbili.
 
Hakuna Mtanzania mwenye akili anayekubaliana na kauli eti TUIONDOE CCM KWA GHARAMA YOYOTE ILE . Huu ni ujinga mtupu. Ina maana hata kwa gharama ya kuisambaratisha nchi kama Somalia au Libya kwenu ni sawa ili mradi eti CCM imeng'olewa madarakani. Lowassa kweli ni bomu la nyuklia ila kamwe halitalipuka, labda litamlipukia mwenyewe afe yeye peke yake labda na Chadema yake kama lile bomu la kujitoa mhanga.

Hakuna haja ya kutishana na wala hakuna mwenye lengo la kuisambaratisha nchi. Lengo ni kuhakikisha CCM inaondoka madarakani na Lowassa ndio silaha sahihi kutumika kuitupia CCM virago.

CCM walijisahau sana kuwa kuna nguvu ya umma. Tusubiri October.

Tiba
 
Umeongea vyema kabisa lakini naamini kuwa hata ktk ubunge Ukawa mmepoteza sana kwani wagombea wanavyolazimika kumsafisha Lowassa ndivyo wanavyozidi kuwa associated nae.
Sasa kazi ni kubwa na wananchi watawaona wote wako sawa in fact wagombea ubunge waliokuwa wanapiga vita ufisadi wataonekana hovyo na wanafiki
Nawasikitikia sana Ukawa ..
Kuhusu Jenerali na magazeti yake wao wanaandika kipi kibaya? Raia Mwema na Raia Tanzania inaandika hali halisi na ukweli, haijakaa kishabiki.
Acheni Ukawa kulalamika .. mlichokifanya ni kufuata mkakati bomu kabisa na litawalipukia muda si mrefu. Taratibu watanzania wanazinduka na wanatambua mlichokifanya. Mnapoteza credibility!
Na mnavyoendelea na matusi na kejeli mnazidi kuzama.

Umenena vyema mkuu yaani wamekuwa kama wamerogwa hata ukiwaambia ukweli wanakupinga na kukuatack vibaya sana kwa kejeli na matusi
 
umeongea vyema kabisa lakini naamini kuwa hata ktk ubunge ukawa mmepoteza sana kwani wagombea wanavyolazimika kumsafisha lowassa ndivyo wanavyozidi kuwa associated nae.
Sasa kazi ni kubwa na wananchi watawaona wote wako sawa in fact wagombea ubunge waliokuwa wanapiga vita ufisadi wataonekana hovyo na wanafiki
nawasikitikia sana ukawa ..
Kuhusu jenerali na magazeti yake wao wanaandika kipi kibaya? Raia mwema na raia tanzania inaandika hali halisi na ukweli, haijakaa kishabiki.
Acheni ukawa kulalamika .. Mlichokifanya ni kufuata mkakati bomu kabisa na litawalipukia muda si mrefu. Taratibu watanzania wanazinduka na wanatambua mlichokifanya. Mnapoteza credibility!
Na mnavyoendelea na matusi na kejeli mnazidi kuzama.

chonde chonde chonde tukalibali kutokubalia,haiwezekazekani binadamu wakawa na mtazamo mmoja katika issues .
 
Nakubaliana na prof James Watson kuwa sisi watu weusi tuna uwezo mdogo sana wa kufikiri,ni wewe Jenerali Ulimwengu uliyewahi kutofautiana na serikali ya ccm kisa kuandika maovu yao,wakakupora uraia wako wakisema kuwa wewe si mtanzania na ukaanza kuishi ndani ya nchi yako kwa kulipia kibali,mtu uliyewahi kuwa mkuu wa wilaya unaambiwa si raia na uishi kwa kibali,sasa hivi unaipigia kampeni ccm iendelee kutawala wewe na mwenzako Mbwambo,huu ni unafiki wa hali ya juu kupindukia,leo ccm imekuwa nzuri kwako kwa lipi hasa? Hata kama padlocks ni best yako tambua kuwa ccm ni mfumo hata aje malaika awe rais kupitia ccm hakuna kitakachobadilika,tupo vitani kuhakikisha kuwa ccm inaanguka kwa gharama yoyote ile,unapokuwa vitani huwezi kuchagua silaha za kupigania,inapobidi unaweza kutumia silaha ya adui ili kushinda vita pindi ukifanikiwa kuiteka ndo maana tukamchukua Lowassa,Lowassa ni bomu la nyuklia ktk vita dhidi ya ccm na kwa hiyo lazima tushinde hii vita,wewe na wenzako mmetugeuka ktk battle field,hamfai kabisa.



Nadhani wewe ndiyo mnafiki na matakwa ya Jenerali Ulimwengu ni sahihi na mazuri kabisa na ukiona mtu anaipenda CCM ujue ana akili sana halafu anajitambua. Usipoipenda CCM huna tofauti na Jini. Mwache mzee Ulimwengu afanye kazi yake sahihi. Mbona huwaongelei wengine huko Tanzania Daima, Majira na Mtanzania?
 
Generali siyo Mtanzania....unataka CCM wamrudishe kwao?....Achana naye wewe endelea kupiga kampeni CCM inangóka
 
Dilemma upo sawa sana hii ni tabia ya unafiki wa kupitiliza huyu watanzania walimuamini na kumuunga mono wakati wa shida akumbuka hâta gazeti lake la Raïa Mwema. ilikua silikosi kila wiki.taratibu Alianza kujiondoa ktk siasa za upinzani na kushabikia utawala. bila shaka atakua kishaahidiwa tonge serekali ijayo hawa watu wapo wengi ndani ya nchi tanzania ina viongozi wa ajabu sana.
 
Mandela alishirikiana na makaburu na wapinzani wake baada ya kuingia ikulu na siyo kabla. Kwa hiyo Mbowe amekosea kumkaribisha Lowasa na kumfanya mgombea wa chadema. Watu wenye akili za kutosha hawawezi kumpa Lowasa kura. Huyu mtu hana maadili na anatumia fedha kutafuta urais na hii ni Hatari. Nina hakika baada ya kampeni wengi wanaonfuata watabadilika na hawatampa kura. Ukawa turidhike na wabunge zaidi ya nusu ili kuithibiti serikali na Sera zetu na ilani yetu zitekelezwe na serikali itakayoundwa hata kama Tingatinga akiwa rais.

Mkuu..sio lazima kutumia njia aliyoitumia MANDELA cha muhimu kufikia Lengo.....Inavyoonekana kuna watu wanatamani tuwe na Vyma vya kudumu vya upinzani hii haiwezekani kila chama kinachojitambua kina malengo yakuongoza Serikali
 
Umenena vyema mkuu yaani wamekuwa kama wamerogwa hata ukiwaambia ukweli wanakupinga na kukuatack vibaya sana kwa kejeli na matusi

Ukweli upi unaosoma huu wakuendelea kudanganya watu kwamba CCM ya Jenga NCHI hatuhitaji kwa sasa
 
yani team lowasa tatizo lao mtu akitofautiana nao kimawazo ni msaliti,katumwa, ana upeo mdogo kwenye kufikiri.. unafikiri wenye akili na ufahamu walifurahi na kupendezwa pale mlipomtukana full bright politician profesa lipumba, mkaendeleaa kwa zitto, mkaenda mbali zaidi hata mkamtukana slaa, juzi mkaanzisha matusi kwa POLEPOLE,. PROF KITILA na leo hapa unamtukana jeneral ulimwengu huyu ambaye thamani yake ktk uandishi ni hali ya juu... unachotakiwa kujuliuliza ni kwanini wasomi maprofesa na watu wenye uelewa mkubwa ktk mambo ya siasa na jamii wanampinga lowasa??? mwaka huu mtawatukana na kuwakashifu wengi wanaopingana na lowasa



Sasa nafurahi Watanzania mnaanza kuchambua kati ya Mchele na Pumba. Hakuna Msomi na Mtu anayejitambua akaisapoti CHADEMA / UKAWA na ndiyo maana kila kukicha huwa nawaambieni kuwa angalieni wale wote wanaompenda na kumuunga mkono " Kubwa la Makapi na Fisadi " a.k.a Lowassa mtagundua ya kuwa Uwezo wao wa kufikiri ni mdogo kama siyo finyu na asilimia kubwa ni Watu wahuni wahuni hivi na wana tuvituvitu fulani hivi.
 
Mandela alishirikiana na makaburu na wapinzani wake baada ya kuingia ikulu na siyo kabla. Kwa hiyo Mbowe amekosea kumkaribisha Lowasa na kumfanya mgombea wa chadema. Watu wenye akili za kutosha hawawezi kumpa Lowasa kura. Huyu mtu hana maadili na anatumia fedha kutafuta urais na hii ni Hatari. Nina hakika baada ya kampeni wengi wanaonfuata watabadilika na hawatampa kura. Ukawa turidhike na wabunge zaidi ya nusu ili kuithibiti serikali na Sera zetu na ilani yetu zitekelezwe na serikali itakayoundwa hata kama Tingatinga akiwa rais.

Wakati mwingine uwe mnafikiri kabla hujaandika matusi yako hapa!unajuaje au umetumia kipimo gani kuwa wewe una akili za kutosha? mbona huleti ushahidi wa kukosa maadili kwa Lowasa?
 
Umeongea vyema kabisa lakini naamini kuwa hata ktk ubunge Ukawa mmepoteza sana kwani wagombea wanavyolazimika kumsafisha Lowassa ndivyo wanavyozidi kuwa associated nae.
Sasa kazi ni kubwa na wananchi watawaona wote wako sawa in fact wagombea ubunge waliokuwa wanapiga vita ufisadi wataonekana hovyo na wanafiki
Nawasikitikia sana Ukawa ..
Kuhusu Jenerali na magazeti yake wao wanaandika kipi kibaya? Raia Mwema na Raia Tanzania inaandika hali halisi na ukweli, haijakaa kishabiki.
Acheni Ukawa kulalamika .. mlichokifanya ni kufuata mkakati bomu kabisa na litawalipukia muda si mrefu. Taratibu watanzania wanazinduka na wanatambua mlichokifanya. Mnapoteza credibility!
Na mnavyoendelea na matusi na kejeli mnazidi kuzama.
Naona unaongozwa na hisia badala ya uhalisia! kwani umeshapita kwenye majimbo yote ukaongea na wapiga kura?
 
Mbona chadema ni chama cha wakristo

Naomba ktk hao Wakristo ututoe sisi wa dhehebu la Roman Catholic kwani tunajua fika kuwa Rais wetu sasa ni Mkatoliki mwenzetu Dr. John Pombe Magufuli. Nani kakuambia ipo siku Rais wa Tanzania atatoka katika madhehebu mengine? Akiwa ni Muislamu basi lazima atokee BAKWATA na akiwa ni Mkristo lazima atokee ROMAN CATHOLIC na hili halina ubishi na hata kama hayo madhehebu mengine yatagoma kumpigia kura Magufuli siyo tatizo kwa CCM kutokana na kwamba hata Sensa yao tu nchi nzima haizidi Milioni 2 ila Wakatoliki hapa nchini tunafikia Milioni 18 na nina uhakika kuwa hata wale Ndugu zetu Waislamu wa kutoka BAKWATA na wao pia ambao ni wengi halafu wanajitambua na wao pia watampigia kura Magufuli na CCM yetu.
 
ukawa vp,yan nyie mtu akiwa against nyie kwenye media kanunuliwa,hii nchi ya kidemokrasia kila m2 ana uhuru wa kusema anachotaka na kua upande anaoutaka...na kwenye demokrasia yyte lazma kuwe na kukinzana haiwezekan wote mkawa upande mkasema ni demokrasia never...nyie wnywe mlisema hakuna adui wa kudumu kwenye siasa iweje leo muanze kumponda dkt ulimwengu wakt nyie adui wenu alikua lowassa sasa hv mnambeba kwa mbeleko...achen siasa za kitoto yan inaonyesha hatuja mature kwenye siasa hata kdg
 
Ulimwengu anaandika makala zake kwa nadharia na falsasa sana. Makala zake ni abstract sana, kiasi kwamba kama ni msomaji mgeni hutazipenda. Hii haijalishi ameandika kwa Kiswahili au Kiingereza. I can vouch for this guy-I have known him for a long time to know he is a true activist/reformist. Ni mmoja ya waandishi wachache wasiopelekeshwa na dini, ukada wala ukanda.

Yeye kama mmoja wa wamiliki wa Raiamwema ni mwandishi mkongwe wa habari na anajua sio busara na ni kinyume cha maadili ya uandishi kuwapangia wenzake cha kuandika. Na inafahamika toka enzi za Rai kuwa kuna baadhi ya waandishi wao 'akili zinahama' wakati wa uchaguzi na wamewahi kuliweka bayana. Mfano Maggid wa nyakati za uchaguzi ni tofauti na wa nyakati zingine zote. Wakati wa uchaguzi, yeye ni pro CCM.

Kwa upande wa Mbwambo, huyu nae ni mwanamageuzi asiyetetereka. Amekuwa na msimamo usioyumba kwenye kutetea mageuzi. 'Tatizo' lake, uanamageuzi wake umejikita kwenye misingi-sio pragmatist. Kiukweli, kwa wafia mageuzi na washabiki wa siasa za chadema, kumpokea Lowassa ilikuwa ngumu sana kwasababu anaenda kinyume na wengi wanachokiamini. Baada ya kuandika makala zaidi ya 20 za kuponda ufisadi na Lowassa, naweza kumuelewa akikataa kumeza matapishi yake.

Namuunga mkono Lowassa kwa sababu he is a real threat to CCM.Japo naunga mkono ukawa, nina wasiwasi (kama Mbwambo) na mstakabali wa baadae wa chadema. Rejea historia ya NCCR mageuzi. Baada ya NCCR kuzimia kisiasa, upinzani wa kweli na mhemuko wa siasa za upinzani ulipoa sana-hiki ndo wanamageuzi waliojikita kwenye misingi wanakihofia. Ukiondoa ajenda ya ufisadi, chadema itazimia kisiasa. Hata hivyo tumaini lipo kwenye idadi ya wabunge wengi wanaoweza kupata. Sina tatizo na Mbowe, ni mwanasiasa makini na mahiri, amefanya kile Mandela na ANC walikifanya-kuungana na adui (National party) kuunda serikali ili kujenga nchi na kusonga mbele. Historia itamhukumu Mbowe, kama ambavyo baadhi ya weusi wanamlaumu Mandela.

Ulimwengu ahishimiwe, ni mwanamageuzi na mwanaharakati nguli. Ni kama Dr. Slaa. Hatuwezi kuthubutu kuusahau mchango wake (kama tunajiheshimu) ktk mageuzi eti kwasababu tu haungi mkono kuja kwa Lowassa, hata kama tunampenda sana Lowassa.


Akili kama hii inataka mtu ambaye anafikiria kuliko ushabiki. Washabiki hawafikirii.Sio kuwa hawana akili ya kufikiri bali wameamua kutofikiri kwa kuwa hawataki kusikia kitu tofauti na mawazo yao.
 
Back
Top Bottom