Jenerali Mstaafu Venance Mabeyo ateuliwa kuwa Mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro

Jenerali Mstaafu Venance Mabeyo ateuliwa kuwa Mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,770
Reaction score
1,173
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:–


(i) Bw. Omari Juma Mkangama ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Ludewa;
(ii) Bw. Juma Abdallah Njeru ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpanda;
(iii) Bi. Hellen Emmanuel Mwambeta ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha;
(iv) Bw. Francis Genes Kafuku ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu;
(v) Dkt. Adam Omar Karia ameteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Maji kwa kipindi cha pili;
(vi) Balozi Dkt. Aziz Ponary Mlima ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi (TISEZA);
(vii) Jenerali Mstaafu Venance Salvatory Mabeyo ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kwa kipindi cha pili;
(viii) Dkt. Harrison George Mwakeyembe ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kwa kipindi cha pili;

IMG-20250716-WA0103.jpg
IMG-20250716-WA0104.jpg
 
Naona,
Mabeyo kala shavu Kwa Mara ya pili,

Hii ni "Asante iliyotukuka"

Nchi hii,
Hamna mamlaka ya uhifadhi Ina pesa nyingi sn kama ngorongoro.
Ety Asante iliyotukukaa 😄😄😄😄

Wanaapa kulinda CCM na c nchi 😄😄😄 ss kwann akistahafu akae shambani wkt nafasi yake ipo alishahaidiwa akilinda chama atakula mema ya nchi 😄😄😄

Je ingekuwa n ww ungekataa alooo😄😄😄😄
 
Back
Top Bottom