Jen.Ulimwengu na Prof.Shivji

lishughulikiwe haraka kama wote tnakubaliana
na katiba mpya iwe vipi....

sasa tatizo ni kuwa wengi hawajui na wengi zaidi wanahitai kuelimishwa
 
labda tuanze humu kueleza ni nini unataka kwenye katiba mpya na nini hutaki...

mimi nataka 1,uteuzi wowote wa rais uthibitishwe na bunge...
2.wabunge wa viti maalumu wafutwe...
3.posho za wabunge zisizidi mara tano ya kima cha chini...
4.wakuu wa mikoa na wilaya afutwe...
5.mikoa iwe na mamlaka yake,kama majimbo hivi...
6,idadi ya mawaziri na wizara iwe fixed.,
7.elimu iwe bure mpaka chuo kikukuu,kama nchi za scandinavia..
8.ardhi iwe kwa watanzania tu...
na mengineyo..........
 

Nakubaliana na wewe mkuu, hata ndani ya mwaka mmoja tunaweza kuwa na katiba mpya inayokubalika na wengi. Ili tuweze kuwa na katiba mpya haraka na inayokidhi matakwa ya wengi, ni muhimu tutekeleze mawazo ya JU kama kigezo cha msingi kabisa.

Kwamba chama tawala kisipewe jukumu la kutupatia katiba mpya. Kwani wananufaika na hii ya sasa. Wanaweza kutuchelewesha hadi baada ya 2015, au wakatupatia katiba mpya lakini mbovu kuliko hii iliyopo.

Kwa kawaida, katiba mpya itapatikana haraka tu iwapo chama tawala kitakubali maoni magumu kwacho. Wasipokubaliana na jambo fulani ama watahujumu mchakato mzima au watatumia mabavu kuiandika wanavotaka
 
katiba mpya sio kitu fixed...

katiba ya tanzania sio lazima ifanane na ya kenya au nchi yoyote.....

swali ni kwa nyinyi mnaodai katiba mpya.mnataka nini ndani ya katiba?????????
 

Mindi nimekusoma nikakuelewa. Nakubaliana na wewe kabisa. Hata hivyo nakubaliana pia na wasiwasi wa kuuachia mchakato kwa uhuru hivyo hata ufikie miaka 15. Nadhani hoja kubwa ni kuwa mchakato uanze hii ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii, kuunda chombo huru na mengineyo. CDM walisema wakichukua madaraka ndani ya siku 100 wanaanzisha mchakato. Huyu bw JK hajatoa muda wowote hata pale aliposema ataunda tume. Nasisitiza Mchakato uanze na hilo ni vema wanaJF na wengine waipendao nchi yao tunapaswa kulishikia bango.
 
Binafsi nina vitu vingi sana ninavyopendelea viwepo kwenye katiba mpya.
Ila hapa nitataja vichache tu
1. Tume ya uchaguzi isiteuliwe na Rais
2.Mawaziri wapatikane kupitia bunge na si kuteuliwa na Rais
3.Mda wa Rais kukaa madarakani iwe ni miaka 4 tu,atakaa miaka 8 iwapo atashinda
uchaguzi unaofuatia.
4.Kiongozi yeyote wa juu serikalini akikutwa na utajiri alioupata kwa kuliibia Taifa
anyongwe hadi kufa au afungwe jela miaka 100 au zaidi.

Ni hayo kwa sasa, nawaachia wengine kuongezea hiyo list
 
binafsi nakubaliana na maoni ya Generali Ulimwengu, ni bahati mbaya mleta mada hukumwelewa. Alichosema ni kwamba katiba si ya vyama vya siasa au kwa ajiri ya kukitoa chama fulani madarakani kwani hata katiba iliyopo inaweza kukitoa chama tawala madarakani kama tulivoona ktk uchaguzi uliopita. Kuhusu ushiriki wa wananchi, Prof. Shivji alisema ni muhimu kushirikisha watu wote na si kundi la watu wachache na hapo ndo alipogusia issue ya kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa katiba bora. Sasa hapo hawa maguru wamepotoka wapi? Tatizo kuna baadhi ya watu hapa JF wanafikiri tunataka katiba mpya kwa ajiri ya chama fulani kuingia madarakani! Tuache ushabiki jamani...hautotusaidia katika mambo ya msingi kama haya!
 
lishughulikiwe haraka kama wote tnakubaliana
na katiba mpya iwe vipi....

sasa tatizo ni kuwa wengi hawajui na wengi zaidi wanahitai kuelimishwa

Mkuu swala kwamba jambo hili halitaki haraka ni sahihi kabisa, lakini lipangiwe kukamilika kwa wakati unaokubalika siyo miaka 10 hadi 15. Kipindi cha miaka mitatu hadi mitano mtu husomea fani akapata degree, kwanini hii katiba inakuwa kama kutunga Msahafu au Biblia? Ni lazima washinikizwe watupatie Katiba mpya katika muda mwafaka siyo haraka. Muda mwafaka ni kati ya miaka mitatu na minne wa tano inaanza kutekelezwa. Ni lazima tuwe na malengo maalum katika kuipata hii Katiba. Wengine hatutaki na tunaomba Mungu tusife kabla hatujachangia maana tulivurugwa sana na hii CCM. Hatutaki kuwaacha watoto wetu kuja kutawaliwa na chama chenye mfumo wa Kifalme uliofumbwa ndani ya lugha tamu ya Jamhuri ya muungano, ambapo upande mmoja wa hiyo jamhuri umeshajitoa kisiasa siasa.
 

Mkuu Brooklyn, hilo tuko pamoja kuwa swala la Katiba siyo liwe na nia ya kupendelea chama kimoja. Lakini muda muafaka wa kuiandaa ni lazima. Usisahau kuwa CCM ndiyo ma-champion wa ku-capitalize on ujinga wa wananchi wa Tanzania na wangependa iendelee hivyo forever. Hawa ndiyo waliounda Katiba mbili zilizopita na hawakuona umuhimu wowote wa kuhakikisha inapelekewa wananchi ili waielewe. Wanazo janja nyingi za kuhakikisha ni nakala chache tu ziko mikononi mwa watu tena I wll dare say, prefarably wale wanaowaunga mkono ndiyo wangependa wawe na nakala tu! Miaka miwili ni muda tosha kuelimisha wananchi na huku maoni yakikusanywa na uandikaji wake ukakamilika mwaka wa tatu na wanne ikarudishwa kwa wananchi kujadiliwa na watano ikaanza kutekelezwa. Ni lazima upangwe muda maalum wa kumaliza hii kazi. La sivyo CCM wao watataka sana iendelee kujadiliwa miaka mia. Kama alivyokumbusha mchangiaji mmoja hapo juu hili swala lilianza kujadiliwa mwanzo wa miaka ya 90. Tume iliyoteuliwa na serikali yenyewe pia ikashauri kuundwa Katiba hakuna hatua zozote zilichukuliwa zaidi ya kulizima jambo hilo. na leo tukubali kuendelea kudai endlessly?? NO! NO! NO!
 

sikubaliani na mawazo hayo.miaka hiyo ni mingi mno kwa ccm kuendelea kuwapo hapo.kenya walichukua miaka 20?waache kutuzuga na kadi zao za ccm.ulimwengu aliyarudisha kadi ya ccm?au shivji?wameshitwa na kjazwa mapesa.mkitaka hadi walioko vijijini basi mtasubiri sana.huko vijini nani kasema kuwa hawataki katiba mpya?mmefika kijijini kwangu mkajua hawana habari na katiba mpya?wanajua.hayo ni maoni yao lakin sote tunahitaji mabadiliko.wasisingizie kuwa ni wanasiasa tu wanataka kwenda ikulu hilo si kweli.
 
Hata mie najiuliza Kenya walichukua mika 10 au 20? walitembelea vijiji vyote?
Jamani wananchi tunahitaji katiba mpya before next election 2015.
 

My Take, Ulimwengu na Shivji ni wananchi na raia kama mimi na wewe na kuzungumza kwao na mawaiza yao sio yana represent nchi nzima na kwenda mbele kwenye swala la Katiba wanajitoa wao wenyewe. Nashukuru tunawafahamu Nani yupo upande wa wananchi na nani anaweza kutumiwa na CCM wakati huu. This is generational thing...old generation hawajui kabisa nini vijana/new generation want and they are not listerning...it's coming realy soon.
 
Pamoja na tofauti zetu katika kuchangia maada hii, inaelekea sote tunakubaliana kimsingi, ulazima wa kutungwa kwa Katiba mpya. Hata hivyo, tatizo linaloweza kutukabili baadaye; kama hatukutahadhari; ni namna ya kuwalazimisha watawala wetu kuiheshimu Katiba hiyo. Mathlani, pale inapothibitika kwamba uongozi wetu wa ksiasa hauipi katiba hiyo nguvu za kisheria kama inavyostahili, Raia atafanyaje kurekebisha hali hiyo?
 

1. Mawaziri wasiwe wabunge bali wathibitishwe na bunge

2. Wabunge wawe ni wakazi halisi wa majimbo wanayowakilisha

3. Tume ya Uchaguzi iteuliwe na bunge
 
Hata mie najiuliza Kenya walichukua mika 10 au 20? walitembelea vijiji vyote?
Jamani wananchi tunahitaji katiba mpya before next election 2015.

Ndugu yangu Kenya walianza siku nyingi sana, nadhani tokea mara baada tu ya uhuru wao. Chama cha KANU kiliweka misingi ya mapambano ya kudai haki kutokana na maamuzi yake ya kimsingi toka zamani kabisa, mfano kuhusu umiliki wa ardhi. siasa za KANU za kupendelea ustawi wa wachache walio nacho na masikini awe masikini kwelikweli, ziliwaandaa wakenya kwa mapambano. hapa kwetu misimamo kama Azimio la Arusha, ambalo liliweka misingi ya wananchi kumiliki uchumi wa taifa, msukumo kwa vijiji na kuwekeza katika kilimo ambacho ndio kinachotoa ajira kubwa kabisa nchini, ilihakikisha kwamba maslahi ya wengi yanazingatiwa. Ni kweli kulikuwa na makosa makubwa tu lakini ya aina ambayo inaweza kurekebishwa na serikali makini. ni baada ya azimio la Zanzibar ndio misingi ya wachache kumiliki uchumi na utajiri wa nchi na walio wengi kuzama katika umaskini, na hapo maandalizi ya hali itakayosababisha mapambano yalianza. Ndio maana hata uchaguzi wa 1995, pale ambapo ilionekana uwezekano wa NCCR chini ya Mrema kuiondoa CCM madarakani, uliona wananchi wakihamasika sana na uchaguzi ule. wananchi walikuwa tayari wameona hali mbaya iliyopo na walikuwa wanatafuta mabadiliko, kama vile maji yanavyotafuta njia ya kupita.

mimi sisemi tuchukue miaka 3, au 5 au 10. mimi ninachosema tu ni kwamba tufanye maandalizi vizuri. good planning is 50% success. tukifanya kosa sasa hivi, CCM wanaweza kutumia nafasi hii kushinda kirahisi na kupitisha katiba isiyotufaa. kumbuka unahitaji ushiriki wa watanzania wengi zaidi katika mchakato huu. na watanzania hao wawe wanaelewa tunachozungumza. je, watanzania walio wengi wanaelewa kinachozungumzwa sasa hivi? wako tayari kwa mapambano ya kudai katiba mpya, hata kwa kutoa gharama kubwa binafsi? my take ni kwamba kama watu wakielewa hasa tunachozungumza, watakuwa tayari kwa mapambano.
 

Tuanze kwanza na katiba hiyo mpya - je itakuwa ni ile tunayoihitaji? kumbuka katiba hii inakipa neema chama tawala, ndio maana kinajitahidi sana kuwakumbusha watanzania uzuri wa katiba hii ya sasa. Aisifuye mvua...tunajua kwamba CCM watapigana wee, na mwisho wakikubali, watateka nyara process ili kitakachoandikwa kiwapendelee. na hata hivyo wanazo njia nyingi tu za kuchelewesha mambo. na mbinu kubwa kabisa ni kwamba wanajua watanzania wengi wakipewa pesa kidogo tu wanalainika. mfano mwanasheria mkuu wa sasa. yupo pale kimaslahi zaidi, ndio maana yupo tayari kutetea misimamo ile mibovu kabisa mradi tu inakubalika na walio madarakani. sasa je, kama CCM watavuruga process, watanzania tumejiandaa kupambana na ccm na serikali yake? njia ya kushinda ni pale unapokuwa na jamii inayoelewa inachotaka. na hata ile hali unayoizungumzia, kwamba je baada ya katiba mpya kupitishwa na CCM na serikali yake wasiiheshimu, tutafanya nini? kuna mifano mingi ya serikali kuvunja katiba na kuvunja sheria za nchi. hapo kitakachoishikisha adabu serikali ni watanzania kutamka kwa kauli moja kwamba wamechoka. ni wajibu wetu kutafakari tutawafikiaje watanzania walio wengi? na tutafikiaje hali hiyo ya kuongea kwa sauti moja, angalau tukiwa na uhakika kwamba tukianzisha sekeseke, watanzania bila kujali umri, dini, dhehebu, jinsia, hali ya uchumi, elimu ya mtu, wote tutanungana na kusema HAPANA!!!
 

Ni kweli kabisa. lakini watanzania wanahitaji nini? kumbuka 1995, watanzania walijumuika na kuiunga mkono NCCR. na climax ilikuwa uchaguzi wa ubunge Temeke, ambapo serikali iliweka nguvu kubwa sana pale lakini Mrema akashinda. watanzania wengi wakawa wanaiangalia NCCR kwa leadership, iongoze mapambano. lakini kilichofuatia ni historia. NCCR ikasambaratika, na mwaka 2000 CCM ikajiimarisha na kushinda zaidi, baada ya watanzania kukata tamaa kwamba inawezekana kuwa na mapambano, wakasema bora zimwi likujualo! 2005 ndio kabisaaa!!!

Sasa ndugu yangu old generation inao wajibu wa kutoa mafundisho ya historia kwa young generation, ambao wanabeba banner ya mapambano hivi sasa. akina Shivji wamepambana tokea enzi za chama kimoja, mpaka leo. wamefundisha wengi tu, akina Jenerali Ulimwengu, na hata akina Tundu Lissu. tuwashukuru sana kwa huduma yao kwa taifa. hakuna kitu kibaya kama kuanza kwa jazba na kushindwa, au kuanza bila plan, tunahitaji plan A, plan B, na hata plan C. na watanzania wajue hilo. unapowasikiliza watu kama Jenerali Ulimwengu, Prof. Issa Shivji, inakubidi utafakari sana wanachosema. hawahitaji kusema kila kitu, lakini wanayosema yanabeba mengi.

Nadhani huduma nzuri kabisa ya JF kwa watanzania, ni kutoa uchambuzi wa plan mbalimbali za kwenda mbele. haitoshi tu kusema HAYA NA TUANZE MARA MOJA! tuanze kwa kufanya nini? Shivji anazungumzia hatua ya kwanza ya kujenga misingi ya kisiasa, ambayo ni kujadili katiba mpya katika maeneo mbalimbali. sawa, tusema tunayotaka yawepo, lakini pia tuseme misingi ya hiyo katiba mpya. na hili la misingi ndio la muhimu zaidi katika hatua hii.
 
sina uhakika kama Kenya walichukua muda mrefu kiasi hicho.

Kwani tunashindwa kufuata walivyofanya wenzetu wa Kenya?? Maana naona kama wao walitumia kama miezi kadhaa tu shughuli ikawa imeisha.

Hawa CCM hawaitaki so kinachofanyika ni kuwanunua woote ambao wanaonekana wanaushawishi mkubwa.
 
NAWAUNGA MKONO JENERALI na SHIVJI kwa maoni na mitazamo yao, maana ni mitazamo yao na hatushinikizwi kuikubali au kuikataa. Walichoeleza ni ushauri wao na maoni yao kuhusiana na katiba Mpya na kwa upande wao wanaona Watanzania wakifuata ushauri wao ndipo tutakapokuwa na katiba bora na madhubuti NARUDIA TENA HUO NI MTAZAMO WAO.

Nami napenda kusema sijawai ona wala kusikia Duniani kote kuwa KATIBA ya nchi fulani imejadiliwa na kuandikwa na wananchi wote wa nchi hiyo. Ukweli ni kwamba hata tukiamua kwenda sasa vijijini kutoa elimu ya katiba ni mategemeo yangu kuwa hatuto ambulia kitu maana Fedha itakayotengwa kwa zoezi hilo itakuwa ni mradi wa wajanja wachache kama ilivyo kawaida yetu Watanzania, pili tukumbuke kunawanao kubaliana na wazo la katiba mpya ambao ni wengi lakini wasio na madaraka ya kiuongozi serikalini hivyo si wasimamizi wa vyombo vya dola na mfumo wa utawala wa nchi yetu, lakini wasio kubaliana na katiba mpya ndio wasimamizi wa mfumo wa siasa na utawala wa nchi na pia vyombo vya dola vi chini yao hivyo hawa jamaa wana nafasi kuwa ya kuharibu mchakato mzima wa utoaji elimu kwa wananchi. Ndio maan DEMOKRASIA ndio mfumo uliokubalika na wengi kufikia maamuzi makubwa ya nchi yetu.

Hapa napenda nieleweke kuwa kusubiri watanzania waelimike kuhusiana na katiba mpya ndipo tuanze kazi ya kuitunga/kuiandaa dhana hiyo kwangu si sahihi, mfano mwaka 1992 tulipoingia ktk mfumo wa vyama vingi ndipo madai ya katiba mpya yalipoanza hadi leo ni kama miaka 19 lakini watanzania bado hawaja elimika kuhusu katiba( namaanisha si watanzania wote walioelimika kuusu katiba) sasa tujiulize ili wote waelimike itahitaji miaka mingapi? Pili wote tumesoma shule, shule ndio mfumo maalum wa kuelimisha lakini si kweli kuwa wote walioingia shule wameelimika hivyo hata tukisema tuelimishane kwanza ndio tuandike katiba mpya si wote watakao elimika pengine ni wengi ambao hawata elimika je ikiwa hivyo itatupasa tuhairishe kuadika katiba mpya na kuanza zoezi la kuelimishaji upya?

Kwa uelewa wangu mfumo wa maamuzi DUNIANI unaendeshwa kwa kufuata dhana ya SIMPLE MAJORITY. Kwa urahisi ni kuwa kundi la watu linaweza kuwaamulia wenzao ikiwa tu litawashinda MFANO litawashinda kwa njia ya kura (chaguzi), au kwa njia ya mabavu(mapinduzi ya kijeshi au ya kiraia(ivory coast) au kwa njia ya kuwazidi uelevu(nchi maskini (watawaliwa) na tajiri (watawala yaani wakoloni)) Kwa maana nyepesi sikuzote watawala uwaamulia watawaliwa au waelevu(wasomi) uwaamulia maamuma(wasio wasomi) yaani wasielimika.NDIO maana UCHAGUZI wa mwaka 0ct 2010 ni asilimia 48% ya watanzania waliojiandikisha ambao ni kama 9.8 milioni ndio walio waamulia watanzania zaidi ya 45milion (waliojiandikisha na wasio jiandikisha) nani awe RAIS wao na wabunge wao (bila kujali kulikuwa na uchakachuaji(uchakachuaji unaangukia ktk kundi la uamuzi wa kiutawala)

HIVYO hata siku moja tusitegemee watanzania tulio na tuliozidi miaka 18 tunaweza kwa pamoja kuamua kuandika katiba mpya kwa pamoja wote tukiwa na uelewa wa katiba HAITAPATA KUTOKEA KAMWE. Hivyo waliopo wenye uelewa na wawajuze wenzao wakati wa mchakato wa uandishi wa katiba ukiendelea namaanisha mfumo wa uelimishaji unaotakiwa ni ule usio rasmi yaani anayetaku kuelimika kuhusu katiba mpa na aelimishwe na asiyetaka tumuache aendelee kujenga nchi maana kaamua kuamuliwa kuhusu katiba. NDIO maana wenzetu KENYA Wamepitisha katiba yao kwa mbinde na kutokukubaliana lakini kimsingi wamekubaliana kuwa katiba si msahafu kama kuna mapungufu watayafanyia kazi mbele ya safari maana katiba ni ni nyaraka HAI yaani inazaliwa inakuwa na inazeeka ikibidi kufa na kuzaliwa nyingine ( ila uhai wake unawezakuwa mrefu sana kuliko wa binadamu) Tukumbuke wakenya hawakuanza kupeana elimu ya katiba ndio waanze kuiandika mfumo uliotumika niuleule utumikao duniani kama nilivyoeleza hapo juu.

CHA MSINGI aliyetaka kujua KATIBA nini na manufaa yake kwa wananchi na TAIFA kwa ujumla, alipaswa kujielimisha toka mwaka 1992 hadi sasa na ambaye umri ulikuwa haumruhusu yaani alikuwa mdogo na sasa amekuwa hadi sasa anamuda wa kuelimika kuhusu katiba. Cha msingi ni kuwa hatuitaji kujua kila kifungu cha katiba kwa kukiweka kichwani au kujua mbinu au ustadi wa kuiandika ( watu wenye ustadi huo wapo) CHA muhimu mwananchi ajue kiba ni nini, inamchango gani kwa ustawi wake binafsi na wa taifa lake, inafanya kazi gani, kwanini ni sheria mama, je yeye anahusika vipi ktk kuiandaa katiba, mawazo yake na maoni yake yanamanufaa gani nk. NI VYEMA TUKAELEWA SI KILA WAZO AU MCHANGO WA MWANACHI UTAINGIZWA KTK KATIBA, NDIO MAANA MWISHO WA SIKU TUNAPIGA KURA KUIPITISHA AU KUIPINGA. cha muhumu ni dhana ya WIN WIN SITUATION i apply ktk maamuzi, yaani uwezi kila ukitakacho kiwemo ktk KATIBA cha muhimu kunautakavyopoteza na kupata hivyo uwiano wa unachopoteza na kupata ndio utakaokusukuma ktk kulidhia katiba mpya au kuikataa wakati wa upigaji kura

MUDA WA KATIBA MPYA NI SASA NA HATUNA MUDA WA KUSUBIRI KATIBA NI DOCUMENT HAI INAZALIWA, KUKUA NA KUFA NA KUZALIWA .................. Hivyo tuiandike, tukibaini makosa tutairekebisha, na vizazi vijavyo vikibaini kuwa imepitwa na wakati kama hii ya sasa ya mwaka1977 wataandika nyingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…