Jembe Lowasa na safari ya Ikulu

Jembe Lowasa na safari ya Ikulu

Jambo Tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
670
Reaction score
203
Nimefarijika sana leo kuwaona hapa
marafiki zangu wengi. Ninapowatazama
hadi machozi yananitoka na kwa uwezo
wa Mungu tutashinda kwani nyote
mnajua nia na ndoto yangu…WanaCCM
msiwe na shaka, tutavuka kwa nguvu
zetu... Wingi wenu huu unanipa faraja
katika safari yetu na kwa kumtegemea
Mungu tutashinda.” ni kauli ya aliyewahi
kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.
Lowassa alitangaza hivi karibuni kuanza
rasmi kwa safari hiyo aliyoiita ya
matumaini ya ndoto zake, ambayo
anasema itatimiza ndoto za Watanzania
za kupata elimu bure, majisafi na
maendeleo ya uhakika.
Alitoa kauli hiyo katika ibada ya shukrani
na kuupokea mwaka mpya, katika Kanisa
la Kiinjili la Kilutheri Tanzania
(KKKT),Usharika ya Monduli Mjini mkoani
Arusha.
Bila ya kutaja safari hiyo ni ipi, Lowassa
anawataka waliohudhuria ibada hiyo
waungane na kaulimbiu yake, ‘Tulifurahi
pamoja, tulihuzunika pamoja na
tutashinda pamoja’.
Hafla hiyo ya kimkakati, ilihudhuriwa na
baadhi ya wabunge, wengi wakiwa wa
CCM, wenyeviti wa mikoa kadhaa wa
chama hicho, wakiongozwa na
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM,
viongozi wa jumuiya za chama na
wengineo.
Licha ya kutoweka bayana aina ya safari
anayoanza, Lowassa ni miongoni mwa
wanaCCM wanaotajwa kuwa wanaowania
urais, kumrithi Rais Jakaya Kikwete.
Dalili hizi za Lowassa kuutaka urais na
kutafuta kabla ya kipenga kupulizwa,
zimeishtua CCM na kumtahadharisha
kuwa atapoteza sifa ya kupitishwa ifikapo
2015.
Safari tangu 1995
Tamaa ya Lowassa kuutaka urais
haikuanza leo wala jana, ni ya tangu 1995
alipojitokeza kwa mara ya kwanza.
Mwaka huo alikuwa miongoni mwa
wagombea 17 wa CCM walioomba
kuteuliwa kuipeperusha bendera ya
chama hicho.
Majina hayo yalipaswa kujadiliwa na
vikao vitatu vya CCM –Kamati Kuu,
Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu.
Kikao cha kwanza kilikua ni Kamati Kuu
ambacho Mwenyekiti wake alikuwa
Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Ali
Hassan Mwinyi lakini Baba wa Taifa,
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa bado na
ushawishi na nguvu kubwa ndani ya
chama hicho.
Nyerere bila kumung’unya maneno,
alisema wazi akiwataja wazi Lowassa na
Waziri Mkuu mstaafu, John Malecela
kuwa hawakuwa wanafaa kugombea.
Nyerere alisema Malecela alikuwa na
madhambi mengi na kwamba alikuwa
ameyabainisha katika kitabu chake cha
‘Uongozi na hatima ya Tanzania’ ambacho
pia alielezea udhaifu wa Horace Kolimba,
aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM.
 
Mbona unatoa habari maktaba !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hivi nyie mnaoshabikia hawa watu wsnaotaka kwenda ikulu kwa gharama yoyote mmedhajiuliza akiupata uraisi hela zake na wanaompa zitarudishwa vipi???? Acheni ushabiki fikirieni kwa makini kesho itakuwaje
 
Kaza buti tunakutarajia kuongoza inchi tutafarijika ukikalia kiti MH.Lowasa
 
Njaa ni kitu kibaya sana! Huyo Lowassa anawapa kiasi gani ili mmfagilie kwenye mitandao?
 
Si bure mmelogwa, na aliyewaloga kafa!
 
ni haki ya kila binadamu kutimiza ndoto zake, achene uzandiki na nyie timizeni zenu
 
this is macheavelism indeed..yaan umeiba mapesa, unawalaghai watu kupitia hyo mifweza kuutafuta urais,mazuzu yanashabkia
 
this is macheavelism indeed..yaan umeiba mapesa, unawalaghai watu kupitia hyo mifweza kuutafuta urais,mazuzu yanashabkia
 
Weziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii wanataka kutuiba na sisi EE MUNGU tuponye na hili dude na wezi wenzie!!!!!
 
Tumefurahi pamoja tumehuzunika pamoja, tutashinda pamoja..
 
Tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja' - Kaulimbiu hii inaleta matumaini sana!
 
Dah! Kwakweli kwa ushabiki huu hatutafika kokote, hivi kweli tuongozwe na wala rushwa?
 
Hakuna cha jembe wala mpini wooote maccm wezi tu hafagiliwi mtu hapa ndugu zetu wanakufa mahospitalini kwa kukosa vifaa na dawa, watoto wanakosa elimu bora kwa ajili ya hawahawa mnaowafagilia sifa za kijinga humu na njaa zenu mnaacha kuongea vitu vinavyotugusa makabwela hata ashuke malaika ndani ya ccm kwa mfumo wao wa kulindana hakuna jipya litakalokuwepo tanzania zaidi yakutufanya manamba hata sisi wenyewe manake kila kitu wameshauza kuna mikataba ya miaka 100 jiulize wewe na mimi bado tutakuwepo? Tuweke chama kingine hawa wanaojiona miungu watu wajifunze na waweze kutambua hakuna ufalme usiokuwa na mwisho .
 
this is macheavelism indeed..yaan umeiba mapesa, unawalaghai watu kupitia hyo mifweza kuutafuta urais,mazuzu yanashabkia

ulipigwa kabari ukachukuliwa hayo mafweza?kamata fursa twende zetu,
 
Back
Top Bottom