Jela miaka 30 kwa kumpa ujauzito mwanafunzi

Jela miaka 30 kwa kumpa ujauzito mwanafunzi

Sasa hiyo mimba wataitoa ama maana baba kijacho ndo huyo mmempelka gerezani
Hii inanifikirisha sana mimi,ndo maana kesi za namna hii haziishi sababu sheria hii hailengi kutatua kero za wanafunzi au watoto wadogo chini ya miaka 18 kuhusu kujihusisha na mapenzi ,sheria omekaa katika kumkomoa mtia mimba (mbakaji) mtiliwa mimba (baba/mama)na mtiwa mimba(binti) hapo hakuna namna mzazi wa binti lazima abebe jukumu la kulea mimba na mjukuu na atakayezaliwa

Binafsi kama serikali itadhamiria kulimaliza hili tatizo haina budi kutoa pesa kwa familia za waathirika ili kumuhudumia mwathirika na mtoto atakayezaliwa,hii ni kwa sababu kwa mtu kama mimi siwezi mfunga mtu kisa kapiga mimba binti yangu harafu baadae nijitwike mzigo wa kulea na kuhudumia mjukuu asiye na baba,ni kheri kumwajibisha mkosaji wangu kwa faini au awajibike katika malezi,lakini kama government itawajibika kutoa japo pesa kidogo ili kumhudumia mwathirika watu wengi watajitokeza kuripoti wabakaji wote.Mwisho wa siku kesi kama hizi zitakuwa historia

Mimi hapa mwaka huu nilikuwa mwalimu wa darasa kidato cha pili,wanafunzi waliopigwa mimba kwa darasa langu ni zaidi ya watoto watano ajabu ni kuwa hakuna mtia mimba hata mmoja aliyepelekwa gerezani,hii ni kutokana na utaratibu wa wazazi kuyamaliza wao kwa wao ili angalau mtoto atakayezaliwa asikose baba.
 
Hapo kosa ni kumpa mimba mwanafunzi, haijalishi ana umri gani. Kisheria tafsiri ya mwanafunzi, ni yule ambae yuko primary school au secondary school. Ingekuwa kosa ni kubaka tuu, sasa hapo ndo tungeangalia umri, aliyebakwa ana umri gani, kama binti ana umri chini ya miaka 18 hapo kosa la kubaka lipo.

Lakini kama yuko miaka 18 nakuendelea na huyo binti ameridhia kufanya mapenzi na huyo mwanaume basi kosa la kubaka halipo. Lakini kama ana miaka 18 na kuendelea halafu hajaridhia kufanya mapenzi na huyo mwanaume kosa la kubaka lipo.
Yaani unasema kumpa mwanafunzi mimba ni kosa?Vipi kama mwanafunzi huyo ana miaka 20?Nadhani kama tafsiri ndiyo hiyo basi kuna shida mahali!Suala hapa ni ubakaji na si kusema mwanafunzi!Kama binti hajafikia umri wa mtu mzima ndio inakuwa ubakaji wenyewe!
 
Hapo kosa ni kumpa mimba mwanafunzi, haijalishi ana umri gani. Kisheria tafsiri ya mwanafunzi, ni yule ambae yuko primary school au secondary school. Ingekuwa kosa ni kubaka tuu, sasa hapo ndo tungeangalia umri, aliyebakwa ana umri gani, kama binti ana umri chini ya miaka 18 hapo kosa la kubaka lipo.

Lakini kama yuko miaka 18 nakuendelea na huyo binti ameridhia kufanya mapenzi na huyo mwanaume basi kosa la kubaka halipo. Lakini kama ana miaka 18 na kuendelea halafu hajaridhia kufanya mapenzi na huyo mwanaume kosa la kubaka lipo.
Sioni mantiki ya kosa la kumpa mimba mtu mzima kisa tu ni mwanafunzi!Yaani ukimpa mimba binti wa miaka 20 ambaye hayuko shuleni ni sawa ila ukimpa mimba binti wa miaka 20 aliyeko shuleni si sawa na unakula mvua!Hapana aisee!
 
Sasa hiyo mimba wataitoa ama maana baba kijacho ndo huyo mmempelka gerezani
Nani atawatunza?? Binti na mtoto??
Mzigo unawaangukia wazazi wa binti!
Hivi vitu vinafikirisha sana, yaani!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Mambo mazito haya tukisema baba wa mtoto asifungwe abaki alee mtoto je apewe adhabu gani badala ya kifungo..?

Mana sasa watu kila kukicha wapigwa miaka 30 na ujinga hauishi wakitoa kifungo si shule nzima watapewa mimba
 
Back
Top Bottom