GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Wanabodi, Usichanganye kukaa Jela na kukaa Mahabusu
Mahabusu una muda hata wa kupiga stori na kuwa na Imani kuna siku mambo yatakaa sawa, Jela sio rahisi hivyo akili inakuruka ghafla na unapata ukichaa wa muda kwenye mazingira yale
Jela Unaanza maisha ukiwa ndani ya uniform za jela
Nilikaa Jela siku nne niliona kama nimekaa mwaka.Mambo ya siku nne tu si mchezo mchezo. Niliingia jela mchana wa saa saba nikapatwa na haja ghafla, Nikaletewa ndoo ya kujisaidia, Ni ndoo chafu huwezi kuangalia mara mbili hiyo ndoo ukiwa ndio siku ya kwanza huwezi kula tena
Jela hakuna huruma, Unakutana na mtu ana kusimulia habari zake za mauaji na ujambazi kama jambo la kawaida, Ukimuangalia mtu anatisha kila sehemu ya mwili amejaa vidonda na ananuka, Kumbuka huyo ndio jirani yako na mmepangiwa cello moja na utaishi nae kwa muda
Jela kuna kila aina ya magonjwa ambayo mtu asiyefika hawezi kuelewa hili ninaloongea, Hata ukifanikiwa kutoka jela unarudi uraiani ukiwa dhaifu sana na ni rahisi
kuondoka mapema kutokana na magonjwa ya kuambukiza toka jela
Tumuonee huruma Sabaya, Kuna wakati ukizuka ugonjwa wa mlipuko jela mfano kipindupindu au TB inakuwa ni vifo na kumbakumba, Jela ni hatari
Kuna Jela na Magereza, Ukisikia Jela ni jela kweli, Haya ni magereza ya Kilimo, Huko kuna Mateso magumu sana, Unalima mpaka mikono inapasuka. Ukikosea kulima kwa mistari utapigwa fimbo na Manyampala kama Mbwa koko
Huko ni kazi na Kipigo tu
Hayo ya Keko na Segere ni magereza siyo jela hizo. Jela zipo huko Njombe, Mbeya, Ruvuma kitai Mbinga. Ni balaa
Waliokaa zaidi ya mwaka huko na wakatoka watakuwa na mengi ya kusimulia
Mahabusu una muda hata wa kupiga stori na kuwa na Imani kuna siku mambo yatakaa sawa, Jela sio rahisi hivyo akili inakuruka ghafla na unapata ukichaa wa muda kwenye mazingira yale
Jela Unaanza maisha ukiwa ndani ya uniform za jela
Nilikaa Jela siku nne niliona kama nimekaa mwaka.Mambo ya siku nne tu si mchezo mchezo. Niliingia jela mchana wa saa saba nikapatwa na haja ghafla, Nikaletewa ndoo ya kujisaidia, Ni ndoo chafu huwezi kuangalia mara mbili hiyo ndoo ukiwa ndio siku ya kwanza huwezi kula tena
Jela hakuna huruma, Unakutana na mtu ana kusimulia habari zake za mauaji na ujambazi kama jambo la kawaida, Ukimuangalia mtu anatisha kila sehemu ya mwili amejaa vidonda na ananuka, Kumbuka huyo ndio jirani yako na mmepangiwa cello moja na utaishi nae kwa muda
Jela kuna kila aina ya magonjwa ambayo mtu asiyefika hawezi kuelewa hili ninaloongea, Hata ukifanikiwa kutoka jela unarudi uraiani ukiwa dhaifu sana na ni rahisi
kuondoka mapema kutokana na magonjwa ya kuambukiza toka jela
Tumuonee huruma Sabaya, Kuna wakati ukizuka ugonjwa wa mlipuko jela mfano kipindupindu au TB inakuwa ni vifo na kumbakumba, Jela ni hatari
Kuna Jela na Magereza, Ukisikia Jela ni jela kweli, Haya ni magereza ya Kilimo, Huko kuna Mateso magumu sana, Unalima mpaka mikono inapasuka. Ukikosea kulima kwa mistari utapigwa fimbo na Manyampala kama Mbwa koko
Huko ni kazi na Kipigo tu
Hayo ya Keko na Segere ni magereza siyo jela hizo. Jela zipo huko Njombe, Mbeya, Ruvuma kitai Mbinga. Ni balaa
Waliokaa zaidi ya mwaka huko na wakatoka watakuwa na mengi ya kusimulia