Je, wewe ni mlaji kupindukia na unashindwa kuacha tabia hiyo? Soma hapa uwaidhike

safuher

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
11,164
15,848
Suala la kula kupindukia hata kama mtu hakipendi chakula hiko kivile ni suala limezoeleka hapa duniani pengine wewe msomaji ni katika wao.

Kula chakula kingi sana ni ulafi na kushindwa kujizuia na kuidhibiti nafsi yako ipasavyo.

Kwa kawaida mwili wa binadamu tumbo lake ili ajihisi ameshiba basi akae kama dakika 5 mpaka kumi baada ya kula chakula,

hii maana yake ukijihisi umeshiba huku unaendelea kula basi jua kilichokushibisha ni chakula ulichokula dakika tano nyuma,hiki unachokula sasa hivi kinaenda kukuongezea mauzito na manyama zembe tu.

SIO SALAMA KABISA KUJIHISI UMESHIBA WAKATI UNAENDELEA KULA, NI HATARI KWA AFYA.

Wakati unatia chakula nafsi ya ulafi hujisemea "hapa nakula sana mchana jioni sili ama nakula kidogo tu"

Sio kweli hii ni shetani wa ulafi mkimbie,tia chakula kidogo tu utakachohisi umeshiba bbaada ya kula na sio wakati wa kula.

Unapokula sana ukashiba haswa hii hutanua misuli ya tumbo na kufanya tumbo liwe linatanuka jambo ambalo litafanya uwe na tumbo kubwa ambalo halitopungua kiurahisi kwa sababu kilichotanuka ni misuli.

Salama kwa tumbo lako ni ule chakula alafu usihisi umeshiba kwa kiasi cha tumbo kutanuka.

Ukila ukashibaaa sana kwanza haufeel comfortabble hata kidogo, unahemea juu juu tu.

Ukila ukashiba ndindindi unajinyima fursa ya kununua japo njugu ama tikiti ukitembea kwa sababu hakuna pa kuweka.

Tumbo ni kama kapu safarini, usitie ukalijaza na safari hujaanza, tia machungwa kidogo, then acha nafasi ya vitu vingine kukaa, unaweza kuona vitu vizuri hina pa kuweka, na tumbo hivyo hivyo.

Usione kama tumbo lako ni kwa ajili ya ugali tu, basi ukala mpaka ukinywa maji yanarudi juu. Ugali kidogo acha, tunda kidogo, karanga kidogo maji kidogo n.k

Anza leo kutia chakula ambacho ukimaliza unatamani kula tena, usitie tena hiyo ni nafsi tu pambana nayo, tia chakula cha wastani ukimaliza utajihisi uko comfortable zaidi.

Kula kawaida kuhifadhi mwili wako.

Unafahamu kuwa tumbo linafanyia kazi chakula chako, je uko tayari kutia chakula kingi zaidi ya uwezo wa tumbo kufanya kazi?

Je, unafahamu kuwa unapokula chakula cha wastani kidogo unarahisisha mfumo wako wa mmeng'enyo wa chakula na kupata choo kwa umaridadi kabisa?

Kuna watu hula mpaka ahujitapisha kwa sababu mwanzo alijihisi furaha na utamu wakati anakula lakini alipomaliza kula akakaa dakika tano kumi akajihisi kushiba zaidi na kujiona hayupo sawa, solution anajitapisha.

Kuepuka haya yote unaweza kujipangilia kula matonge kumi tu ya chakula chako yale ya wastani.ndio matonge kumi tu jitahidi kama WEWE SIO MTU WA KAZI NGUMU NA ZA NGUVU.
 
mim huwa najifunza sanankwa watoto.mtoto anakulaaa akishibaa tu anaacha hapo hapo.
sasa unakuta mtu umepakua kias mtu anashngaa mbona kidgo.nashngaa naga sana na utu uzima huu ila nina mwil wastan na kilo 60
 
mim huwa najifunza sanankwa watoto.mtoto anakulaaa akishibaa tu anaacha hapo hapo.
sasa unakuta mtu umepakua kias mtu anashngaa mbona kidgo.nashngaa naga sana na utu uzima huu ila nina mwil wastan na kilo 60
Na watoto wadogo hula taratibu ili kile wanachokula kisiishe,si unajua ile hulka ya kitoto,biscut ataidekeza wee atakula taratibu ili isiishe,unde ndo uhalisia wa maisha yetu tunatakiwa kuishi.

Tunayo mengi ya kujifunza kwa watoto wadogo
 
Inategemeana na kazi unayofanya, kwa wale masela wa machimboni migodini (kimeruka) nadhani angle hii wamenielewa namaanisha nini

Kule hakuna neno kushiba bali kinachoangalia pale kila mtu amenyanyuka baada kuhakikisha sufuria iko tupu.

Watu kama hao ukiwaambia mara yao ya mwisho kushiba ni lini utawaumiza tu kichwa kuvuta kumbukumbu za utotoni.

Kuna daktari alituambia tule chakula chenye ukubwa kulingana na ngumi yako, yani kiufupi doctor alishauri watu wale tonge moja kisha wanawe maji
 
Watu wanatamani uwape mbinu ya kuongeza hamu ya kula wewe unaleta mauzauza? 😆😆
Siku hizi kula imekuwa kama adhabu,,,, hebu nifundishe namna ya kuongeza hamu ya kula
Mkuu sijagusia kuhusu hamu ya kula.

Sidhani kama watatarajia jambo ambalo sijaligusia.
 
Inategemeana na kazi unayofanya, kwa wale masela wa machimboni migodini (kimeruka) nadhani angle hii wamenielewa namaanisha nini

Kule hakuna neno kushiba bali kinachoangalia pale kila mtu amenyanyuka baada kuhakikisha sufuria iko tupu.

Watu kama hao ukiwaambia mara yao ya mwisho kushiba ni lini utawaumiza tu kichwa kuvuta kumbukumbu za utotoni.

Kuna daktari alituambia tule chakula chenye ukubwa kulingana na ngumi yako, yani kiufupi doctor alishauri watu wale tonge moja kisha wanawe maji
Hukumuelewa dokta.

Ukubwa wa ngumi haupimwi na kile kinachotengenezwa ndani ya ngumi.

Ukubwa wa ngumi hupimwa mkono mzima kwa umbo lake nje.
 
Inategemeana na kazi unayofanya, kwa wale masela wa machimboni migodini (kimeruka) nadhani angle hii wamenielewa namaanisha nini
Nshapiga mfano wa hizo kazi aisee sio mchezo.

Mfanya kazi ngumu uzi haumuhusu,japokuwa nayeye sio salama sana kula akajaza tumbo ndindindi,naye pia anatakiwa ale kwa wastani ili kuupa nafasi tumbo kuchakata vizuri chakula chake
 
Hukumuelewa dokta.

Ukubwa wa ngumi haupimwi na kile kinachotengenezwa ndani ya ngumi.

Ukubwa wa ngumi hupimwa mkono mzima kwa umbo lake nje.
ngumi ni ngumi tu kwa ukubwa wowote ule wa ngumi ukiu convert kwenye ugali bado ni tonge tu, labda iwe ngumi ya unju
 
ngumi ni ngumi tu kwa ukubwa wowote ule wa ngumi ukiu convert kwenye ugali bado ni tonge tu, labda iwe ngumi ya unju
Kama msimamo wako ni huo sawa..

Lakini kuanza kujadili ukubwa wa tonge linalotengenezwa na ngumi ati ni sawa na ngumi iliyotengezatongi hilo huo itakuwa ni upotezaji wa muda.😁😁😁
 
Serious huwa nachoka
Naweza kuwekewa chakula hapo nikala robo ama nusu ya sahani...nikishahisi njaa imeisha nachoka kuendelea na mood ya kula inakata🤣🤣
Una mwili mzuri sana,kula ni jambo la dharura tuu kama kukabwa na mkojo...
 
Back
Top Bottom