Wenzetu wakenya wako mbioni kukamilisha Reli yao hivi karibuni nawapongeza sana kwa mambo mawili makubwa.
1. wameshirikiana na vijana wengi sana wa kitanzania kufanya kazi hii kama maopareta wa mitambo mbalimbali, madreva na kazi nyingine nyingi zilizohitaji ujuzi maalumu
2. katika hili hawakutubagua majirani zao, tofauti na nilivyokuwa naamini.
SABABU
Watanzania kwa miaka mingi sasa tulikuwa tukishiriki kujenga miundombinu hivyo kuzalisha watu wenye ujuzi mbalimbali katika shughuri za ujenzi wa miundo mbinu kuliko majirani zetu wote na kampuni ya CRBC, CCCC. Zimefanya kazi hapa nchini hivyo walichukua wafanyakazi wengi toka katika miradi waliyofanya hapa nchini
SWALI
Je mtawavumilia wakenya pia watakapokuja kutusaidia kujenga ya kwetu hivi karibuni kwani tayari wana ujuzi katika ujenzi wa reli.