Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,073
Hilo ndilo swali la msingi ambalo sisi watanzania tunapaswa kujiuliza, kwa kuwa kumeanza kujitokeza wanaccm ambao wameanza kuukosoa waziwazi utawala huu wa serikali ya awamu ya 5 ambapo hapo kabla ilikuwa haiwezekani kufanyika kitu kama hicho na badala yake tuliwazoea wapinzani pekee wakipambana na hali hii ya kupigwa risasi mchana kweupe na watu "wasiojulikana" kutekwa kwa raia mbalimbli na baadaye kupatikana, matukio ya kuuawa wananchi wasio na hatia na matukio mengi ya aina hiyo yamekuwa ya kawaida sana kwenye utawala huu wa serikali ya awamu ya 5
Wapinzani wamelalamika wee, wanaharakati wa haki za binadamu wamepigia kelele wee na baadhi ya viongozi wa dini nao wamelalamika weeee........ Lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kukomesha hali hiyo.
Tukaamza kuona mabandiko ya wanaccm kwenye mitandao ya kijamii, lakini Mara tu inapobainika na kuwekwa wazi kwenye jamii kuwa waliobandika mabandiko hayo ni wanaccm, watumiaji hao Mara moja wamekuwa wakikanusha kuwa siyo wao waliopost hizo taarifa na badala yake account zao zimekuwa hacked!
Refer taarifa za kukanusha za akina Ole Sendeka, Ridhiwan Kikwete na Shyrose Bhanji
Lakini hivi sasa wamejitokeza wanaccm "majasiri" na kueleza waziwazi msimamo wao kuwa hawakubaliani na mfumo wa kisiasa unaoendeshwa na utawala wa awamu ya 5
Wanaccm ambao wameonyesha kuupinga waziwazi mfumo huu serikali ya awamu ya 5 kwa kuwataja wachache tu ni Hussein Bashe na Nape Nnauye
Nimeanza kuyakumbuka maneno ya Mheshimiwa Tundu Lissu kuwa mtu huyu akishaumaliza upinzani atakuja kwenu CCM, kwa kuwa historia duniani kote ya "madikteta" ndiyo "formula" yao ya kuanza na upinzani na hatimaye kumalizana na wale "wanaowashwawashwa" ndani ya chama chake!
Hatimaye watanzania wote bila kujali itikadi zetu za kisiasa tumeamua kuupinga utawala huu kwa nguvu zote.
Kwa kuwa tumeona ndiyo njia pekee iliyobaki kabla Taifa letu halijasambaratika na kuelekea shimoni.
Mungu ibariki Tanzania
Wapinzani wamelalamika wee, wanaharakati wa haki za binadamu wamepigia kelele wee na baadhi ya viongozi wa dini nao wamelalamika weeee........ Lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kukomesha hali hiyo.
Tukaamza kuona mabandiko ya wanaccm kwenye mitandao ya kijamii, lakini Mara tu inapobainika na kuwekwa wazi kwenye jamii kuwa waliobandika mabandiko hayo ni wanaccm, watumiaji hao Mara moja wamekuwa wakikanusha kuwa siyo wao waliopost hizo taarifa na badala yake account zao zimekuwa hacked!
Refer taarifa za kukanusha za akina Ole Sendeka, Ridhiwan Kikwete na Shyrose Bhanji
Lakini hivi sasa wamejitokeza wanaccm "majasiri" na kueleza waziwazi msimamo wao kuwa hawakubaliani na mfumo wa kisiasa unaoendeshwa na utawala wa awamu ya 5
Wanaccm ambao wameonyesha kuupinga waziwazi mfumo huu serikali ya awamu ya 5 kwa kuwataja wachache tu ni Hussein Bashe na Nape Nnauye
Nimeanza kuyakumbuka maneno ya Mheshimiwa Tundu Lissu kuwa mtu huyu akishaumaliza upinzani atakuja kwenu CCM, kwa kuwa historia duniani kote ya "madikteta" ndiyo "formula" yao ya kuanza na upinzani na hatimaye kumalizana na wale "wanaowashwawashwa" ndani ya chama chake!
Hatimaye watanzania wote bila kujali itikadi zetu za kisiasa tumeamua kuupinga utawala huu kwa nguvu zote.
Kwa kuwa tumeona ndiyo njia pekee iliyobaki kabla Taifa letu halijasambaratika na kuelekea shimoni.
Mungu ibariki Tanzania
