ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,261
- 4,443
Kwanza kabisa niweke maslahi wazi kwamba mimi nina Asili ya Uchagani hata hivyo andiko hili sio msimamo wala mtazamo rasmi wa Wachaga.
Kwa muda mrefu Chama cha Chadema kimekuwa na ushirika na Jamii za kaskazini hasa Wachaga kiasi kwamba baadhi ya watu wamekuwa wakikihusisha chama hicho na Uchaga au wachaga. Hata hivyo wako wachaga kadhaa maarufu walioko ndani ya vyama vingine vya siasa ingawa vyama vyao havikutanabaishwa na wachaga au uchaga wao.
Harakati za wachaga na siasa za nchi hii ni za muda mrefu na wachaga ni moja katia ya jamii ambazo zina mafanikio makubwa ndani na nje ya siasa za Upinzani nchini Tanzania,
Katika siku za karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la uhamaji wa wanachama wa Chadema huku wengin wakichelea kusema wanakoelekea, Hii inaonesha kwamba Wanasiasa hawa ambao ni mchanganyiko wa wachaga na wasio wachaga huku wengi wakiwa wachaga wameshindwa kuendelea kuwepo ndani ya CHADEMA.
Swali ninalojiuliza ni JE wachaga Wamepokonywa Chadema?Kama Jibu ni Ndio Je wachaga wataunda Ngome nyingine? Je waliobaki ndani ya Chadema wataweza kujipambanua kama chama kisichokuwa na Mrengo wa UCHAGA au CHAMA ambacho kinawakataa/kuwabagua wachaga na badala yake kuwa chama kinachowaunganisha watazania wote?
Karibuni tujadili kuhusu mUstakabali wa siasa za CHADEMA bila Chaga Identity ambayo imekuwa kwenye chama hicho kwa muda mrefu pamoja na kwamba kimeibua vinara wa siasa katika Makabila na kanda nyingine wakiwemo Wanasiasa kama Zitto Kabwe, Kitila Mkumbo na wengine wengi.
Tupeane maoni hapa tukielekea kwenye Uchaguzi mkuu
Kwa muda mrefu Chama cha Chadema kimekuwa na ushirika na Jamii za kaskazini hasa Wachaga kiasi kwamba baadhi ya watu wamekuwa wakikihusisha chama hicho na Uchaga au wachaga. Hata hivyo wako wachaga kadhaa maarufu walioko ndani ya vyama vingine vya siasa ingawa vyama vyao havikutanabaishwa na wachaga au uchaga wao.
Harakati za wachaga na siasa za nchi hii ni za muda mrefu na wachaga ni moja katia ya jamii ambazo zina mafanikio makubwa ndani na nje ya siasa za Upinzani nchini Tanzania,
Katika siku za karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la uhamaji wa wanachama wa Chadema huku wengin wakichelea kusema wanakoelekea, Hii inaonesha kwamba Wanasiasa hawa ambao ni mchanganyiko wa wachaga na wasio wachaga huku wengi wakiwa wachaga wameshindwa kuendelea kuwepo ndani ya CHADEMA.
Swali ninalojiuliza ni JE wachaga Wamepokonywa Chadema?Kama Jibu ni Ndio Je wachaga wataunda Ngome nyingine? Je waliobaki ndani ya Chadema wataweza kujipambanua kama chama kisichokuwa na Mrengo wa UCHAGA au CHAMA ambacho kinawakataa/kuwabagua wachaga na badala yake kuwa chama kinachowaunganisha watazania wote?
Karibuni tujadili kuhusu mUstakabali wa siasa za CHADEMA bila Chaga Identity ambayo imekuwa kwenye chama hicho kwa muda mrefu pamoja na kwamba kimeibua vinara wa siasa katika Makabila na kanda nyingine wakiwemo Wanasiasa kama Zitto Kabwe, Kitila Mkumbo na wengine wengi.
Tupeane maoni hapa tukielekea kwenye Uchaguzi mkuu