Je ungekuwa wewe hii isingekuuma?

Je ungekuwa wewe hii isingekuuma?

Ndege Tausi

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
992
Reaction score
476
Tangu jana amenuna kisa...

Muda sasa umepita tangu awe na mawasiliano na wanawake wawili, mmoja ni binti wa miaka 24 ambaye alinitambulisha kuwa ni mtumishi mwenzake anayefanya kazi kwa kujitolea, na mwingine mama wa makamo ambaye ni kiongozi mwenzake katika michezo.

Wanawake hawa wamekuwa wakimpigia simu kila mmoja kwa wakati wake. Kinachonitia shaka na kunipa hisia kuwa labda ni wapenzi wake ni mawasiliano ya mara kwa mara na namna anavyoongea nao.

Mara zote wanapompigia simu hutaka kufahamu mahali alipo na wakati mwingine kumlaumu wanapompigia na kukuta simu yake ipo bize. Huwa nayajua haya kutokana na anavyokuwa anajitetea.

Huwa anapokea simu na kuongea na mimi nikiwepo bila hofu kwani nikimuuliza huyo ni nani hujibu kuwa ni yule binti au wakati mwingine yule mama.

Sasa jana binti kapiga na kumuuliza maswali hayohayo, nikaona bora nimuulize ili aniondoe shaka. Kilichofuata hapo ni kununiwa hadi sasa asubuhi kaondoka bila kuniaga.

Naombeni mnisaidie mawazo. Je ungekuwa wewe isingekuuma ?
 
To treat a lady you have to be a gentleman.vumilia atajirekebisha.
 
Anakupenda ila atakuwa ameanza kujisahau. Kama ni kwenye kuota moto basi hachochei kuni tena.

Sasa cha kufanya nipe namba yako niwe nakupigia hadi saa tano za usiku akikuuliza ni nani unamjibu ni baba mmoja hivi wa JamiiForums. Lazima ataomba poo.
 
nipe namba yako mi mwenyewe demu wangu ananifanyia issue kama hizo afu maumivu yake si mchezo!!
 
Huyo keshakata kamba yuko mtaani mtafute umrudishe bandani,labda kuna sehemu umeanza kujisahau na wenzio wanajazilishia,be careful
 
Ahhha lazima iume rafiki yangu, ila cha kujiuliza je nimeolewa?? au bado ni urafiki tu?? kama hujaolewa sio mbaya sana bado unayo fursa ....! kwasasa kaa nae na umuulize kwa kina kulikoni?? hao ndio wanaume bana wanakwambia michepuko kwao dili, njia kuu kuna foleni. Kama bado hujaolewa kuwa makini, kumbuka kumshirikisha na Mungu pia yupo na anajibu.
 
MTU kama hakupend c lazima akwambie ishara tu utaziona anza kujitoa mapema huku ukimchunguza
 
Anakupenda ila atakuwa ameanza kujisahau. Kama ni kwenye kuota moto basi hachochei kuni tena.

Sasa cha kufanya nipe namba yako niwe nakupigia hadi saa tano za usiku akikuuliza ni nani unamjibu ni baba mmoja hivi wa JamiiForums. Lazima ataomba poo.

Nimeipenda hii, dawa ya moto ni moto.
 
Hana adabu kabisa, anawezaje kupokea simu za wanawake hata kama ni wakazini kama maongezi sio yakikazi lazima nipachimbe bila jembe, Hawa watu wanaonaga sisi tuna mioyo ya chuma, huyo wewe mtafutie advertise moja hadi aombe pooo, Amua kujifanya upo bize na simu kuliko kawaida yaani akiita huitiki hadi aite mara tatu ndio unajifanya umeshtuka " abee unaniita?????? " ikibidi kama unarafiki yako wa kike ambae anakupigia sana simu, jaribu uwe unaongea nae as if unaongea na mwanaume, yaani mpenzi, sweet, honey nyingiiiiiii akikuuliza ni nani, unamjibu ini shorti "ni rafiki yangu" alafu unanuna. ila kama anamaguvu hakikisha uwe na helment maana wanaume wengine ni weka mbali na watoto hawataniwi.
 
na wew anza kupigia watu usiku wa saa sita usiku akikuliza unasema ni yule mbaba wa bandalini
 
Hana adabu kabisa, anawezaje kupokea simu za wanawake hata kama ni wakazini kama maongezi sio yakikazi lazima nipachimbe bila jembe, Hawa watu wanaonaga sisi tuna mioyo ya chuma, huyo wewe mtafutie advertise moja hadi aombe pooo, Amua kujifanya upo bize na simu kuliko kawaida yaani akiita huitiki hadi aite mara tatu ndio unajifanya umeshtuka " abee unaniita?????? " ikibidi kama unarafiki yako wa kike ambae anakupigia sana simu, jaribu uwe unaongea nae as if unaongea na mwanaume, yaani mpenzi, sweet, honey nyingiiiiiii akikuuliza ni nani, unamjibu ini shorti "ni rafiki yangu" alafu unanuna. ila kama anamaguvu hakikisha uwe na helment maana wanaume wengine ni weka mbali na watoto hawataniwi.

We mtie ujinga mwenzio haache.
 
Anakupenda ila atakuwa ameanza kujisahau. Kama ni kwenye kuota moto basi hachochei kuni tena.

Sasa cha kufanya nipe namba yako niwe nakupigia hadi saa tano za usiku akikuuliza ni nani unamjibu ni baba mmoja hivi wa JamiiForums. Lazima ataomba poo.

Badala uongeze kigingi kwenye tairi unazidi kutoa kigingi ili gari liporomoke Co.. Ww unayako bhana
 
Ujinga gani unazungumzia??????
Kwani yeye anamoyo wa chuma, afanye hivo ili na yeye roho imuume.

Mwanaume ni mwanaume, kuna njia nyingine ya kumueleza sio hiyo maana hapo utaonekana kama unataka kushindana naye.
Kwani ameshamueleza hiyo tabia kwamba haipendi....au ndio mpaka kwa hishani ya watu wa marekani ndio muongee.
 
Mwanaume ni mwanaume, kuna njia nyingine ya kumueleza sio hiyo maana hapo utaonekana kama unataka kushindana naye.
Kwani ameshamueleza hiyo tabia kwamba haipendi....au ndio mpaka kwa hishani ya watu wa marekani ndio muongee.


Mnapenda kubembelezwa hata mkikosea eee!!!!!!! hiyo dhana ya mwanaume ni mwanaume futa kabisa hapa, mwanaume anayejielewa lazima amuheshimu mkewe, unachepuka alafu unajifanya nunda weweeeeee!!!!!!!!! haipo hio. labda kama bidada huyo ni mungu wake ila kama ni binadamu mfyuuuuuuu, Asipo mrusha roho nitamuona mjinga sana, heshima za uoga mwisho mwaka 1990 wakati mandela anatoka jela.
 
Back
Top Bottom