JE UNAJUA?

The Iron

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2017
Posts
1,397
Reaction score
1,470
Habari za muda huu ndugu wanaJF,ninatumaini wote ni wazima afya

Ningependa kuwapa takwimu muhimu sana siku ya leo inayohusu members wa JF

Tanzania ina jumla ya watu wazima wasiopungua mil27 na JF ina members 472,580....Hii inamaanisha JF kwa makadirio inawakilisha 0.5% ya watu wazima nchini Tanzania

Hivyo ni vigumu sana kuamini kwamba JF inafaa kuwa chombo cha kutumia katika kuakisi uhalisia uliopo katika jamii yetu ya Tanzania...comments unazoziona hapa hazina nguvu yoyote katika kupindua uhalisia wowote ule katika Tanzania

Hitimisho:Tuache kujifariji kwa michango ya 0.5%(ambayo kwenye hiyo 0.5% yenyewe kuna mgawanyiko),kama tunahitaji mabadiliko ya kweli tuingie mtaani tushawishi jamii yetu kwanza
 
Kwaiyo unataka kusema?
 
Ila kuna mapendekezo na maamuzi ya nchi yamewahi kufanywa kwa influence ya nyuzi na au komenti za JF.

Hii tusemeje?
 
Ukifika wakati wa kuingia mabarabarani ndiyo utajua JFinawakilisha mawazo ya watanzania
 
Ila kuna mapendekezo na maamuzi ya nchi yamewahi kufanywa kwa influence ya nyuzi na au komenti za JF.

Hii tusemeje?
Hebu mkuu ungetusaidia kuyaweka(japo kwa ufupi) na sisi tuyafahamu
 
Ukifika wakati wa kuingia mabarabarani ndiyo utajua JFinawakilisha mawazo ya watanzania
Duh umenikumbusha zile kelele za UKUTA na Mange Kimambi...mimi nikajua tutafanya kweli kumbe hamna kitu kabisa
Mimi nadhani wengi tuna-comment kwa hasira kutokana na ugumu wa maisha yetu au ushabiki wa kisiasa ila katika uhalisia hatuwezi fanya chochote kile
 
WanaJF huwa wanapenda kujiaminisha mambo makubwa ya kitaifa kwa comments za watu wachache humu
Mtukane jiwe basi uweke na kapicha kako mkuu, 0.5% ndogo sana watu wengi hawatakuona
 
Mtukane jiwe basi uweke na kapicha kako mkuu, 0.5% ndogo sana watu wengi hawatakuona
Mkuu hayo ni mambo ya TCRA...mimi nazungumzia jamii yote kwa ujumla
 
MAJORITY RULE(95.5%), MINORITY RIGHTS(0.5%)
 
aah mbona sasa tulikua tunahangaika tuifunge ....

Ooh sory wakuu nimeropoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…