Me juzi juzi tu hapa nilikua nasafiri,tumbo la kuhara likanishika ghafla..nikapaki ka mkweche kangu pembeni,nikachukua maji niliyokua nimeyanunua kwa ajili ya kunywa nikaingia kichakani nikaendesha wee mpaka nikamaliza,ila muda wote niliokua nimechuchumaa nilikua na mawazo ya itakuaje niking'atwa na nyoka?
Vipi na wewe mdau,ushawahi kukutana na hali kama hii?
Ulikuwa ukijitia uoga bila sababu mkuu, nyoka anayereact ni yule unayemkanyaga ama mnayekutana naye ghafla zero distance.
Kuchuchumaa kisha nyoka akufuate, jambo hilo haliwezekani, nyoka hukimbia watu.
Mi' ilinitokea tumeenda msibani bush huko, choo ni kimoja kikawa kinatumiwa na kina mama, sisi wanaume tujijue!
Maji ama chakula cha msibani kikaniletea mushkeli tumboni, nikaenda kujiachia vichakani huko, ndipo nilipoenda kujigundua kwamba mi ni mlemavu kabisa kama walivyo walemavu wengine!
Shazoea choo cha kukaa kwa miaka mingi natumia, kumbe kilishanilemaza, kuchuchumaa siwezi!
Nikasukumwa kwa lazima kuchuchumaa kutokana na muwasho wa kuhara, miguu ilishindwa kukunjika ili kunibeba sawa sawa, nikajilazimisha tu kwenda chini mzima mzima kama ng'ombe anayezaa, nikawa nimepiga magoti sasa huku nimeishika ardhi kwa mikono miwili nimeshindwa kujibeba na kuanza kujisaidia bila utaratibu, almanusura nijinyee!
Nilipomaliza kujisaidia nijitawadheje sasa ni vituko, iyeeh!
Nikatambaa kama mnyama toka kwenye kinyesi nikichukua tahadhari nisijichafue, nikafosi kuchuchumaa kwa nguvu magoti yakawa yananiuma sana.
Nikausogelea mti nikafosi kuukumbatia kwa kuudabua, dumu la maji poa mkononi ndiyo nikapata balonce ya kuchuchumaa kutawadha.
Nikalifanya zoezi hilo kipumbaf pumbaf ili nimalize chap kwa haraka ninusuru magoti yangu kwa maumivu.
Kwenye kunyanyuka ndo kasheshe nyingine hapo tena!
Mti nilioukumbatia kuchuchumaa ndiyo nikautumia kama mkongojo kusimamia nd'onikaanza kufunga funga suruali, kwa mkono mmoja, mkono mwingine nimeushikilia mti nikawa nimelegea kabisa.
Nikashindwa hata kuchomekea nikavaa tu nyoro nyoro kunusuru miguu yangu na kupoza maumivu!
Baada ya hapo nikawa nawaza, kungelikuwa na 'onlooker' angeliinjoi sana 'seen' hiyo na kubakia na simulizi la maisha!
Baada ya kuugundua ulemavu huo, nikaanza zoezi la chumbani la kuchuchumaa na kunyenyuka mara 15-30 kila siku na kwa sasa nipo naendelea vizuri, improvement inaonekana.