Je, UHURU uko wapi?

Je, UHURU uko wapi?

Trust None

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2018
Posts
1,260
Reaction score
4,421
Ikiwa leo Disemba 09, 2018 ni kumbukizi ya uhuru wa Tanganyika miaka 57 iliyopita, nimeshangaa kuona wananchi hawaipi kipaumbele siku hii. Wapo kimya kama vile ni siku za kawaida. Sitaki kuamini kama tulipata uhuru kwa SILVER PLATE ndiyo maana hatuithamini siku hii.

Nimewaza sana, kwa mfano ikatokea WAKRISTO wakafuta sherehe za KRISMASI ama WAISLAM wakafuta sherehe za IDD EL FITRY, sielewi itakuwaje. Kwa maoni yangu, UHURU ni zaidi ya SHILINGI BILIONI MOJA.

Najiuliza, hivi watoto wadogo wanaochipukia wataelewa UHURU wao ni upi na watakuwaje WAZALENDO kama hawaoni harakati na shamrashamra za uhuru?

Hata yale MAGAZETI pendwa ya leo ya THE TANZANITE na JAMVI LA HABARI hayajaipa kipaumbele siku kuu ya leo.

Tusubiri tuone UHURU wetu wakati WAPINZANI wakisherekea hivi leo.
 
Ikiwa leo Disemba 09, 2018 ni kumbukizi ya uhuru wa Tanganyika miaka 57 iliyopita, nimeshangaa kuona wananchi hawaipi kipaumbele siku hii. Wapo kimya kama vile ni siku za kawaida. Sitaki kuamini kama tulipata uhuru kwa SILVER PLATE ndiyo maana hatuithamini siku hii.

Nimewaza sana, kwa mfano ikatokea WAKRISTO wakafuta sherehe za KRISMASI ama WAISLAM wakafuta sherehe za IDD EL FITRY, sielewi itakuwaje. Kwa maoni yangu, UHURU ni zaidi ya SHILINGI BILIONI MOJA.

Najiuliza, hivi watoto wadogo wanaochipukia wataelewa UHURU wao ni upi na watakuwaje WAZALENDO kama hawaoni harakati na shamrashamra za uhuru?

Hata yale MAGAZETI pendwa ya leo ya THE TANZANITE na JAMVI LA HABARI hayajaipa kipaumbele siku kuu ya leo.

Tusubiri tuone UHURU wetu wakati WAPINZANI wakisherekea hivi leo.
Chagua lipi linakufaa, kwenda kanisani ukayajenge na MUNGU wako au ufuate program ambazo mkuu wa mkoa wako alivyoitoa namna ya kusherekea uhuru au ubaki nyumbani na familia yako.
 
Kama raia namba moja ameipuuza; na siyo mara ya kwanza kuipuuza unategemea nini kwa raia wengine. Natamani wangeupuuza mwenge unaokula pesa nyingi zaidi lakini si maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika. Anyway, huo ndo mwendo wa awamu hii. Tuvumilie tu mpaka tutakapochoka!
 
Kupata uhuru ni jambo lililokuwa mchakato tu, ndio maana hakuna nchi isiyohuru leo!

Wanachoduwaa wengi wengi ni kujiuliza matokeo ya huo uhuru, manufaa ya huo uhuru.

Leo watu wamekuwa wakiahidiwa kula matunda ya uhuru kila miaka 5 inapoisha.
Wanasubiri wee mwisho hawaoni.

Structure ya siasa zetu imelemaza watu kujua watafanyiwa, wataletewa, wataajiriwa nk. Hilo ndio tatizo!
 
Labda wa kushusha bendera, in 15% ndio wanaonufaika na matunda ya uhuru
 
Back
Top Bottom