Marlex Jr
JF-Expert Member
- Nov 6, 2015
- 1,823
- 2,425
Tunahitaji kubadili mfumo wetu wa kujiendesha...tuwe na Sheria nzuri na Bora kuanzia hapo mwelekeo wetu kama taifa utakuwa ktk njia sahihi.Mimi naogopa sana na mtu yeyote mwenye akili aje hapa anisaidie kutafakari. Sisi sote tunaongozwa kwa misingi ya katiba na sheria na hakuna kiumbe yupo juu ya sheria.
************
Ni hivi Mkuu yapo machache yakufikiria, kuwaza na kuwazua kujua kinachoendelea
Labda tujiulize machache dhidi ya katiba ile ambayo wengi mmelua mkishadadia kwamba tulikua tunaendeshwa kwa misingi ya SHERIA na katiba;
1. Sheria ilikua wapi mkuu tulipokua tunatoa magogo Tanga kuyapeleka Mombasa kisha kuyarudisha tena Tanzania ili yaonekane ni imported?
2. Sheria ilikua wapi wale Twiga walipokua wanapanda ndege kwenda ughaibuni?
3. Katiba ilikua wapi bandari ilipogeuka chumo la wezi na walarushwa?
4. Sheria ilikua wapi Mafuta yalipokua yanatolewa Bandarini kwa kibali cha transit yakapelekwa hadi Mbeya kisha yakarudishwa Chalinze kumwagwa kwenye petrol station?
5. Katiba ilikua wapi kuwamulika waliozifanya ofisi za Serikali kama vibanda vyao binafsi vya kujitajirisha?
ANGALIZO
Naomba usiniletee stori za Serikali ilikua ni ya CCM.
Sasa basi kinachofanyika ni kile wazungu wanachosema THE END JUSTFIES THE MEANS kwa ukiritimba na umangimeza wa Sheria tulizonazo Rais Magufuli asingeweza kufanya hata 1/10 ya alichokifanya Kama angehitaji kufuata mlolongo wa sheria.
Mfano mdogo tu PPRA Act inasema hakuna manunuzi yoyote kufanyika bila kupitishwa na Bunge moja lakini mbili lazima kuwe na Proforma invoice tatu za kuonyesha ushindani na the lowest bider ndiye atakayepewa tenda.
Unadhani ingeichukua Serikali muda gani kupitisha?
1. Ununuaji wa Ndege
2. Ujenzi wa SGR
3. Ujenzi wa Bwawa la Umeme mto Rufiji
4. Ujenzi wa vituo vya afra na hospitali za Wilaya na mikoa pamoja na ujenzi wa nyumba za watumishi?
5. Unadhani ingehitaji malumbano kiasi gani kupitisha ujenzi wa Daraja la mfugale, Ubungo, salenda, kivuko cha Mwanza, ujenzi wa meli nk?
Kama sheria ilikuwepo na haikusaidia kupambana na uhalifu vipi Kama Sheria haitatumika kuzuia maendeleo ya nchi hiyo hiyo?
Tatizo ninaloliona Mimi ni kwamba uwepo wa Sheria nzuri si kinacholeta maendeleo bali uwepo wa kiongozi imara ndio kunakoleta maendeleo.
NADONDOSHA MIC
Hizi Sheria za kujiwekea makongwa si nzuri kwa ustawi wa taifa letu maana unatoa upenyo kwa kiongozi kufanya jambo lolote.
Kiongozi mzuri na imara ni yule anaye tokea ktk mfumo sahihi.