voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,553
- 11,885
View: https://youtu.be/45tUyT29Xx8?si=FiDJLgdgOnGlidgn
Nimewaona hawa wataalamu wa "TMA" kupitia Luninga ya "ITV"habari saa mbili jioni hii. wametoa tahadhali ya mvua kubwa za majanga almaarufu kama El-nino!
Ambazo wanasema zitanyesha kwa wingi sana mwezi huu,na huenda zikavunja madaraja ya reli na miundombinu mingi ya Barabarani na mafuriko nchi nzima.
Ni vema na shukrani ziwaendee.kama itakuwa kweli. Na hii ni mara ya kwanza kwa kitengo hiki kujitokeza na kutoa tahadhali ya janga kubwa kama hili nchini.
Shaka yangu kuu:
Ni kwamba haya masuala ya utabiri wa hali ya hewa, hayatolewi kwa kipande kipande cha ardhi au mipaka ya nchi fulani pekee.
Bali tunaona likiwa ni suala ambalo ni "Global" nikimaanisha ni la kidunia kama "Planet World"
Na tunashuhudia kupitia luninga mbalimbali Duniani zikiwemo maarufu kama CNN, Aljazeera, BBC, France international nk.
Hawa wanaripoti hali ya hewa kwa Dunia nzima na hata tunaona ikionyesha ziwa victoria bahari ya Hindi Dar es Salaam kwa kina kabisa.
Na mara zote imekuwa inatokea kuwa kweli na ninadhani hata hivi vyombo vyetu hapa nchini huwa vina Paste saa ingine kutoka huko.
Sasa basi, hoja yangu na Mashaka yangu ni kwamba haiwezekani vifaa vya Tanzania ambavyo kiuhalisia haviwezi kuzidi vile vya mataifa ya magharibi ambao wanaviona vimbunga na kuwaondoa raia wao maeneo hatarishi.
Kwamba vya kwetu vimeiona El- Nino ya mwezi wa tisa leo?
Ila vile vya nje wanako kopi havijaiona hiyo?
Hii mimi nasema ulu msemo maarufu wa watani zangu wa kichaga.
"NGASHTUKA"
Kuna wahuni wanajaribu kwa kila namna kututoa kwenye mjadala wa DP-WORLD kwa kutaka kututia hofu jamii ili tujisahau kwao wapitishe mambo yao chap, kupitia bunge lijalo kwa kubadili vile vifungu viwili vya dheria ya uwekezaji.
Kwa kuondoa kinga ya "TUNU" za Taifa.
Je, majirani zetu Kenya wao hii haiwahusu?
Au hawana utaalamu kama wetu?