mnyikungu
JF-Expert Member
- Jul 26, 2009
- 1,960
- 2,464
Nilipokuwa shule ya msingi darasa la tano mwalimu wetu alikuja na kutuuliza utamaduni ni nini? kwa kweli hakuna aliyejibu jibu lililomlizisha mwalimu mbaka mwenyewe alipotuambia kuwa utamadumi ni uhai na kielelezo cha kabila/nchi yoyote duniani,Hapa ndipo swali langu linapokuja je Tanzania ni ni nchi mfu? ni kielelezo gani kinachotutambulisha na kutuonyesha utaifa wetu?je tukisimama nje ya tanzania nani atajua kama sisi ni watanzania? au ndio utandawazi umetuharibu?
Wenzetu hutumia nguvu nyingi sana kulinda tamaduni zao je Tanzania yetu inafanya hivyo? mimi nilifikiri labda lugha yetu ya kiswahili ndio inayoweza kutusaidia lakini mbona sijaona ikipewa umuhimu wake? nenda leo mahakamani utaona ni kichekesho mtu kutoka kijijini anapohukumiwa kwa kiingereza, yaani tumeshidwa kabisa kulinda utamaduni wetu! lugha za makabila yetu zinapotea lakini sijaona juhudi zozote za kuziokoa lugha hizo,Elimu ya sayansi haileti matokeo mazuri kwa sababu ya lugha, wanafunzi badala ya kuelewa wengi wanakariri,Tofauti na nchi kama japani au china ambao tamaduni zao wanazienzi,si ushirikina bali ni kwa tamaduni zao ndio maana leo wapo hapo walipo.
uMEFIKA WAKATI TANZANIA INATAKIWA IBADILIKE KWA KUENZI NA KULINDA UHAI WAKE ILI LIENDELEE
Wenzetu hutumia nguvu nyingi sana kulinda tamaduni zao je Tanzania yetu inafanya hivyo? mimi nilifikiri labda lugha yetu ya kiswahili ndio inayoweza kutusaidia lakini mbona sijaona ikipewa umuhimu wake? nenda leo mahakamani utaona ni kichekesho mtu kutoka kijijini anapohukumiwa kwa kiingereza, yaani tumeshidwa kabisa kulinda utamaduni wetu! lugha za makabila yetu zinapotea lakini sijaona juhudi zozote za kuziokoa lugha hizo,Elimu ya sayansi haileti matokeo mazuri kwa sababu ya lugha, wanafunzi badala ya kuelewa wengi wanakariri,Tofauti na nchi kama japani au china ambao tamaduni zao wanazienzi,si ushirikina bali ni kwa tamaduni zao ndio maana leo wapo hapo walipo.
uMEFIKA WAKATI TANZANIA INATAKIWA IBADILIKE KWA KUENZI NA KULINDA UHAI WAKE ILI LIENDELEE