QUALITY
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 853
- 115
wana JF na watanzania kwa ujumla,
Tumeona watawala wetu mbalimbali wakifanya madudu na hakuna anayechukua hatua au kutoa kauri kali kukemea. sasa tumefikia hatua ya mabomu kulipuka mara kwa mara na serikali kukaa kimya. Tumeshuhudia kamati/tume zikiundwa na kuleta majibu yasiyofaa halafu watawala wetu wanachekelea na kukejeli wananchi.
Yako maswali mengi ya kujiuliza kwa serikali yatu
1. Serikali imejifunza nini tangu mabomu ya mbagala kulipuka?
2. Waliosababisha uzembe huu wa Mbagala, walifanywa nini?
3. Wananchi waliopoteza majengo/nyumba zao mbagala mpaka leo kuna ambao hawajalipwa. watalipwa lini?
4. Kuna waliopoteza maisha, serikali imefanya nini kwa familia hizo?
5. Wao wataalamu wa mipango miji wanaopima na kutoa viwanja mpaka jirani na makambi ya jeshi, na hati kutolewa, wameshughulikiwa namna gani?
Tuanzishe vuguvugu la kupata viongozi bora kuepukana na mabalaa haya.
Tumeona watawala wetu mbalimbali wakifanya madudu na hakuna anayechukua hatua au kutoa kauri kali kukemea. sasa tumefikia hatua ya mabomu kulipuka mara kwa mara na serikali kukaa kimya. Tumeshuhudia kamati/tume zikiundwa na kuleta majibu yasiyofaa halafu watawala wetu wanachekelea na kukejeli wananchi.
Yako maswali mengi ya kujiuliza kwa serikali yatu
1. Serikali imejifunza nini tangu mabomu ya mbagala kulipuka?
2. Waliosababisha uzembe huu wa Mbagala, walifanywa nini?
3. Wananchi waliopoteza majengo/nyumba zao mbagala mpaka leo kuna ambao hawajalipwa. watalipwa lini?
4. Kuna waliopoteza maisha, serikali imefanya nini kwa familia hizo?
5. Wao wataalamu wa mipango miji wanaopima na kutoa viwanja mpaka jirani na makambi ya jeshi, na hati kutolewa, wameshughulikiwa namna gani?
Tuanzishe vuguvugu la kupata viongozi bora kuepukana na mabalaa haya.