Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 5,895
- 11,788
Wakuu, kwa maeneo niliyotembea hapa Tanzania naona kama uwekezaji upo haba sana, namaanisha uwekezaji wa makampuni makubwa.
Inaonekana miji yetu inakua kwa kasi ila maghorofa hamna, mfano ukisikia mji umekua kwa kasi basi jua tu ni wakazi ndio wameongezeka na wanaanza kufungua frame na kujenga nyumba, ila uongezekaji wa hotels, makampuni nk naona ni mdogo
Mfano Mwanza Jiji kuna watu zaidi ya milioni 1 lakini ukifananisha maghorofa na Mombasa au Kigali unaweza kujiuliza nini kinafanya Mombasa na Kigali ijengeke kuliko Mwanza licha ya kuwa na population zinazokaribiana
Mimi najiuliza kwa nini miji yetu ya Tanzania ipo hivi? Inakuaje Mbeya jiji la watu laki 7 maghorofa ya kuhesabika?
Mimi nilitegemea sehemu ikiwa na watu wengi basi na makampuni mengi yatakuja kuwekeza, yatajenga ofisi zao na mara nyingi huwa ni ghorofa, lakini la hasha. Sisi miji yetu ukuaji wake ni kuongezeka tu watu, na kupanuka ukubwa. Kwa nini?
Pia napenda kujua miji inayokua na kuongezeka maghorofa Tanzania ukiondoa majiji 6
Naongelea maghorofa kwa sababu najua kwenye sekta nyingine kama barabara, hospitali, shule nk miji ya Tanzania inajitahidi.
📷 Ruangwa, Lindi
Inaonekana miji yetu inakua kwa kasi ila maghorofa hamna, mfano ukisikia mji umekua kwa kasi basi jua tu ni wakazi ndio wameongezeka na wanaanza kufungua frame na kujenga nyumba, ila uongezekaji wa hotels, makampuni nk naona ni mdogo
Mfano Mwanza Jiji kuna watu zaidi ya milioni 1 lakini ukifananisha maghorofa na Mombasa au Kigali unaweza kujiuliza nini kinafanya Mombasa na Kigali ijengeke kuliko Mwanza licha ya kuwa na population zinazokaribiana
Mimi najiuliza kwa nini miji yetu ya Tanzania ipo hivi? Inakuaje Mbeya jiji la watu laki 7 maghorofa ya kuhesabika?
Mimi nilitegemea sehemu ikiwa na watu wengi basi na makampuni mengi yatakuja kuwekeza, yatajenga ofisi zao na mara nyingi huwa ni ghorofa, lakini la hasha. Sisi miji yetu ukuaji wake ni kuongezeka tu watu, na kupanuka ukubwa. Kwa nini?
Pia napenda kujua miji inayokua na kuongezeka maghorofa Tanzania ukiondoa majiji 6
Naongelea maghorofa kwa sababu najua kwenye sekta nyingine kama barabara, hospitali, shule nk miji ya Tanzania inajitahidi.
📷 Ruangwa, Lindi