Bob Manson
JF-Expert Member
- May 16, 2021
- 4,546
- 8,759
Huwezi kuwapa sifa ya uongozi watu ambao wanatuhumiwa kutumia madhaifu ya wananchi kuimarisha mamlaka na tawala zao. Zifuatazo ni sababu za kuamini kwamba hatuna viongozi bali watawala.
1. Inadaiwa Wananunua vituo vya matangazo (media) kubwa zote.
Lengo ni ku control mitazamo ya wananchi, kuwalisha drama na propaganda ili wazidi kuwa wajinga na wasijue nini hasa kinaendelea katika uhalisia wa taifa lao. Media Ni kiungo muhimu katika ustawi wa taifa, na wanajua umuhimu huo ndyomaana wanafaya juhudi kununua kama sio kuhonga media hizo ili zifanye yale yenye manufaa kwao.
2. Wanatuhumiwa kuteka, kutesa na kuuwa wakosoaji.
Wakosoaji ambao wanafanya juhudi kubwa kuwazindua wananchi na kuwatoa katika janga la ujinga, hugeuka kuwa adui wa utawala huu. Atateswa hata kupotezwa kabisa ili wananchi wasipate atakaye wafumbua macho.
3. Inadaiwa Wanarubuni wasomi kwa kuwaaminisha wakiungana na chama chao basi watapata nafasi za ajira.
Vyuoni tunaona wimbi kubwa la wanafunzi kujiunga na kuwa wanachama wa chama fulani kwasababu wameaminishwa pasipo kufanya hivyo basi hawatapata ajira hasa serikalini.
4. Wanatumia uwanja wa sanaa kama silaha yao ya kupata ushawishi wa wananchi ( Bread and circuses).
Tunaona pesa nyingi zinatumika kuandaa matamasha ya muziki na kuwalipa wasanii, lengo ni kuwapumbaza wananchi kwa muziki na maigizo ili wazidi kuzama katika kiza cha burudani na kusahau mambo ya muhimu katika taifa lao.
5. Wanatumia michezo kama njia ya kucheza na hisia za watu.
Badala ya kuimarisha sekta ya michezo kwa kubuni na kuanzisha programu zenye manufaa, wao wanaonunua magoli na kulipia mashabiki tiketi za ndege. Lengo ni kuwaaminisha mashabiki kwamba wapo nao pamoja na wanawajali.
Hawa sio viongozi bali ni watawala ambao lengo lao kuu ni kuhakikisha wanabaki madarakani kwa nguvu zote, lengo lao sio kusaidia na kuwaokoa wananchi bali ni kuwatawala na kuwafanya wawe wajinga zaidi.
NOTE: Ujinga wetu ndyo mtaji wao mkubwa.
1. Inadaiwa Wananunua vituo vya matangazo (media) kubwa zote.
Lengo ni ku control mitazamo ya wananchi, kuwalisha drama na propaganda ili wazidi kuwa wajinga na wasijue nini hasa kinaendelea katika uhalisia wa taifa lao. Media Ni kiungo muhimu katika ustawi wa taifa, na wanajua umuhimu huo ndyomaana wanafaya juhudi kununua kama sio kuhonga media hizo ili zifanye yale yenye manufaa kwao.
2. Wanatuhumiwa kuteka, kutesa na kuuwa wakosoaji.
Wakosoaji ambao wanafanya juhudi kubwa kuwazindua wananchi na kuwatoa katika janga la ujinga, hugeuka kuwa adui wa utawala huu. Atateswa hata kupotezwa kabisa ili wananchi wasipate atakaye wafumbua macho.
3. Inadaiwa Wanarubuni wasomi kwa kuwaaminisha wakiungana na chama chao basi watapata nafasi za ajira.
Vyuoni tunaona wimbi kubwa la wanafunzi kujiunga na kuwa wanachama wa chama fulani kwasababu wameaminishwa pasipo kufanya hivyo basi hawatapata ajira hasa serikalini.
4. Wanatumia uwanja wa sanaa kama silaha yao ya kupata ushawishi wa wananchi ( Bread and circuses).
Tunaona pesa nyingi zinatumika kuandaa matamasha ya muziki na kuwalipa wasanii, lengo ni kuwapumbaza wananchi kwa muziki na maigizo ili wazidi kuzama katika kiza cha burudani na kusahau mambo ya muhimu katika taifa lao.
5. Wanatumia michezo kama njia ya kucheza na hisia za watu.
Badala ya kuimarisha sekta ya michezo kwa kubuni na kuanzisha programu zenye manufaa, wao wanaonunua magoli na kulipia mashabiki tiketi za ndege. Lengo ni kuwaaminisha mashabiki kwamba wapo nao pamoja na wanawajali.
Hawa sio viongozi bali ni watawala ambao lengo lao kuu ni kuhakikisha wanabaki madarakani kwa nguvu zote, lengo lao sio kusaidia na kuwaokoa wananchi bali ni kuwatawala na kuwafanya wawe wajinga zaidi.
NOTE: Ujinga wetu ndyo mtaji wao mkubwa.