Je, roho inaweza kujidhuru?

Je, roho inaweza kujidhuru?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,096
Reaction score
828,932
Refer mada ya kwanini watu wengi hufa usiku
Kuna maelezo na justifications za kisayansi kuhusu watu kufa usiku ambazo hata hivyo hazitoi majibu kwa asilimia mia moja.

Tunaishi katika dunia mbili (ulimwengu) tuna ulimwengu wa roho na ulimwengu unaoonekana... Ulimwengu wa roho ndio ulimwengu halisi na pumzi/uhai wa ulimwengu unaoonekana.

Chochote kinachotokea kwenye ulimwengu unaoonekana asili na chanzo chake ni ulimwengu wa roho.

Mwili kwenye ulimwengu wa roho hujilinda na chochote kibaya hasa pale inapotokea vita ya kiroho. Lakini kuna wakati mwili kupitia nafsi roho huamua kujidhuru yaani kufanya lolote lenye madhara kwa mwili mfano matumizi ya vilevi, ama kutouhudumia mwili na hata kujitoa uhai.

Kinachotokea kwenye ulimwengu unaoonekana ni replica ya ulimwengu wa roho! Mtu anapoamua kujinyonga, huyu anakuwa na utashi katika nafsi na ufahamu wake wa kile anachofanya!

Kwenye ile mada ya makutano ya kiroho , tunaona kwamba binadamu anapolala, utashi na ufahamu wake huenda mapumzikoni (dormancy/ muted state) ni kipindi hiki ambapo roho huchukua mikoba yote.

Ni kipindi hiki ambapo roho huivinjari dunia huko na huko, kwenye mabaya na mazuri, kwenye misitu yenye wanyama wakali, kwenye ajali, kwenye vita nk nk... Roho yako hukutana na kupambana na yote hayo.. Kumbuka ndoto nzuri au mbaya unazoota kila siku usingizini.

Roho inapokuwa huko na kupata ajali yoyote mbaya huwa hairudi mwilini.... Kinachotokea hapo ni kifo cha usingizini! Lakini pia roho huweza kujipeleka yenyewe kwenye shida ama vita isiyoweza kushinda na kujeruhiwa kabisa
Vile vile roho huamua yenyewe kuondoka na kutorejea tena mwilini (dhana ya kujinyonga).

Kwakuwa roho ni kitu kisichokufa, hivyo tunaposema kifo cha roho ni roho yenyewe kutorejea mwilini.

Kuna vichoo pia husababisha roho kujitenga na mwili na hapa ndio ushirikina na uchawi vinapoingia.

Kwamba unatumiwa roho nyingine iifukuze roho yako mwilini.... Matokeo yake ni kifo lakini daima kikiwa ni kifo chenye walakini.

Wafao usingizini ni matokeo ya roho zilizoenda kuvinjari dunia na zikashindwa kurejea ngamani.
 
ila kuna tafsiri nyingi kuhusu ndoto. mi ninachojua ndoto yoyote ni Mungu anasema nawe au shetani anasema nawe au kuwa na shuguli nyingi wakati wa mchana na kuelekea akili kutotulia wakati umelala ndio zinaitwa ndoto zitokanazo na shuguli nyingi
sa sijui hapa mshana ana tua elimu ya namna gani tena?
 
ila kuna tafsiri nyingi kuhusu ndoto. mi ninachojua ndoto yoyote ni Mungu anasema nawe au shetani anasema nawe au kuwa na shuguli nyingi wakati wa mchana na kuelekea akili kutotulia wakati umelala ndio zinaitwa ndoto zitokanazo na shuguli nyingi
sa sijui hapa mshana ana tua elimu ya namna gani tena?
Uko sahihi kabisa lakini ndoto ziko za aina nyingi sana
 
Kama ni hivyo, kile kinachoitwa mizimu, Je ni roho zilizokatishwa uhai wa mwili?
 
Na vipi mshana Kwa mfano nimelala nikaamka nikasahau ndoto niliyoota hapo roho inakuwaje??
 
elimu kama hizi hazipo uraiani kabisa..
mtu akifa usingizini wazee wetu utaeaskia..marehemu amerogwa" basi wanaanza mnyooshea vidole aliekuwa na ugomvi na marehemu..
or alikua na presha ikapanda au ikashuka usingizini"
dakatar nae haoni chochote..anaacha sintofahamu kwa wafiwa.
 
mshana mi nlivokua mdogo kama miaka 7 hadi 9 nlikua naota ndoto moja ..na hii lazima nistuke usiku mnene..
naota niko juu ya mlima mrefu mwembamba...ila ni mrefu kama mnara..nimesimama on the peak najirusha...nashuhudia kabisa hivi naenda chini...ila nkukaribia ardhi ndo nastuka..uani sipat kushuhudia nlihit vipi ardhi..halafu kustuka kwangu ni kwa spidi had nakaa kabisa mapigo yanaenda kasi.
 
Refer mada ya kwanini watu wengi hufa usiku
Kuna maelezo na justifications za kisayansi kuhusu watu kufa usiku ambazo hata hivyo hazitoi majibu kwa asilimia mia moja.

Tunaishi katika dunia mbili (ulimwengu) tuna ulimwengu wa roho na ulimwengu unaoonekana... Ulimwengu wa roho ndio ulimwengu halisi na pumzi/uhai wa ulimwengu unaoonekana.

Chochote kinachotokea kwenye ulimwengu unaoonekana asili na chanzo chake ni ulimwengu wa roho.

Mwili kwenye ulimwengu wa roho hujilinda na chochote kibaya hasa pale inapotokea vita ya kiroho. Lakini kuna wakati mwili kupitia nafsi roho huamua kujidhuru yaani kufanya lolote lenye madhara kwa mwili mfano matumizi ya vilevi, ama kutouhudumia mwili na hata kujitoa uhai.

Kinachotokea kwenye ulimwengu unaoonekana ni replica ya ulimwengu wa roho! Mtu anapoamua kujinyonga, huyu anakuwa na utashi katika nafsi na ufahamu wake wa kile anachofanya!

Kwenye ile mada ya makutano ya kiroho , tunaona kwamba binadamu anapolala, utashi na ufahamu wake huenda mapumzikoni (dormancy/ muted state) ni kipindi hiki ambapo roho huchukua mikoba yote.

Ni kipindi hiki ambapo roho huivinjari dunia huko na huko, kwenye mabaya na mazuri, kwenye misitu yenye wanyama wakali, kwenye ajali, kwenye vita nk nk... Roho yako hukutana na kupambana na yote hayo.. Kumbuka ndoto nzuri au mbaya unazoota kila siku usingizini.

Roho inapokuwa huko na kupata ajali yoyote mbaya huwa hairudi mwilini.... Kinachotokea hapo ni kifo cha usingizini! Lakini pia roho huweza kujipeleka yenyewe kwenye shida ama vita isiyoweza kushinda na kujeruhiwa kabisa
Vile vile roho huamua yenyewe kuondoka na kutorejea tena mwilini (dhana ya kujinyonga).

Kwakuwa roho ni kitu kisichokufa, hivyo tunaposema kifo cha roho ni roho yenyewe kutorejea mwilini.

Kuna vichoo pia husababisha roho kujitenga na mwili na hapa ndio ushirikina na uchawi vinapoingia.

Kwamba unatumiwa roho nyingine iifukuze roho yako mwilini.... Matokeo yake ni kifo lakini daima kikiwa ni kifo chenye walakini.

Wafao usingizini ni matokeo ya roho zilizoenda kuvinjari dunia na zikashindwa kurejea ngamani.
usiku ndio muda wa uumbaji unafanyika,hivyo hata wagonjwa wengi hupona usiku
 
Mshana hapa nina kitu cha kushare ambacho kilinitokea ila namshukuru Mungu nilipambana nacho nikakishinda. Nakumbuka kuna siku nililala ila nikagundua pumzi inaniishia nikaamka na ikawa kila nikitaka kusinzia naona naishiwa pumzi naamka nikapambana na hii hali hadi saa tisa usiku nilipoamua kuwapigia simu ndugu zangu kuwataarifu kuwa nisipoamka wajue nimeshindwa kupambana na hiyo hali,nililia sana usiku huo ila naifananisha na hichi ulichokisema kuwa roho ilitamani kuuacha mwili na isirudi ila niligoma nahisi. Unasemaje kwenye hali kama hii mshana?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana hapa nina kitu cha kushare ambacho kilinitokea ila namshukuru Mungu nilipambana nacho nikakishinda. Nakumbuka kuna siku nililala ila nikagundua pumzi inaniishia nikaamka na ikawa kila nikitaka kusinzia naona naishiwa pumzi naamka nikapambana na hii hali hadi saa tisa usiku nilipoamua kuwapigia simu ndugu zangu kuwataarifu kuwa nisipoamka wajue nimeshindwa kupambana na hiyo hali,nililia sana usiku huo ila naifananisha na hichi ulichokisema kuwa roho ilitamani kuuacha mwili na isirudi ila niligoma nahisi. Unasemaje kwenye hali kama hii mshana?

Sent using Jamii Forums mobile app
Yeah roho ilikuwa mbali na mwili kisha ikakutana na hali za hatari ama ilikuwa inagoma kurudi
 
Kuna kipindi Fulani nikiwa Nina miaka 14 nilikuwa naota nakufa nilipokaribia kukata roho nashutuka huku moyo unanienda mbio sana na mara nyingi ilikuwa inanitokea hivyo mpaka nikawa naogopa kulala ikifa usiku, mshana roho ilikuwa inataka kuacha?
 
Kuna kipindi Fulani nikiwa Nina miaka 14 nilikuwa naota nakufa nilipokaribia kukata roho nashutuka huku moyo unanienda mbio sana na mara nyingi ilikuwa inanitokea hivyo mpaka nikawa naogopa kulala ikifa usiku, mshana roho ilikuwa inataka kuacha?
Kulikuwa na nguvu ya uvutano kati ya roho yako na nguvu hasi... Hii hali inaisha unaposhinda vita... La sivyo ungeondoka mapema kabisa kama wengine... Kumbuka kifo sio kwa vijana bali kuanzia miaka sabini na ukiwa na nguvu miaka 80
 
umeniacha kidogo fafanua kiongozi
Kuna ndoto huwa marudio ya mawazo matendo na maneno yetu ya siku husika ama nyuma yake...! Uhalisia wake hutegemea sticky ya tukio husika
 
Back
Top Bottom