Je, Reshuffle ijayo PM Kasim Majaliwa atapona?

Je, Reshuffle ijayo PM Kasim Majaliwa atapona?

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,056
Reaction score
10,729
Kwa hali hii kisiasa tutegemee reshuffle kubwa zaidi ndani ya miezi michache ijayo na ambapo hata Waziri Mkuu atahusika.

Ni dhahiri bin shairi kuna kutoeleweka kwa Rais kwa Mawaziri wake, ama kwa kuwa hawaelewi sera, kanuni na miongozo ya kazi au Rais Magufuli mwenyewe haeleweki.

Utendaji wa Mawaziri wetu wa kutokujiamini, hofu na unafiki hautawaacha wengi.

Kwa kauli ya Raisi, Waziri mkuu amekuwa ni mtu wa kutumwa kufuatilia utendaji wa shughuli za wizara ambazo kimsingi yeye ndiye kiranja Mkuu wa Wizara hizo.

Alidai kamtuma Mtwara, Kamtuma Bukoba, kamtuma Lushoto nakadhalika.

Aliwahi kushuhudia, aliwahi kufikiri kuwatimua wabunge wote kusini akiwepo Waziri Mkuu kuhusiana na sakata la gawio la korosho ambalo liliachiwa kujadiliwa kizembe Bungeni.

Jana tena katamka akirefer kazi aliyomtuma waziri mkuu Bukoba "...Kwa nini tu nisikuteue kuwa Waziri wa Kilimo?"

Napata mashaka sana kwa kauli kama hizi kama Rais ana furaha sana utendaji wa waziri wake Mkuu!
 
Kwa ADMINI kule magogoni, anaweza hata asiamke kesho asubuhi na Uwaziri Mkuu Wake . Re-shuffle ikawa mbali sana.
 
Ulimsikia au ulisimuliwa? Ulibahatika kuunganisha akichozungumza au upeo wako uliishia hapo tu kuwa hajafurahishwa na waziri mkuu..waambie wazazi wako au kaka zako wakusimulie.
 
Twende taratibu kidogo "aliwahi kufikiria kuwatimua wabunge wote kusini"

Inamaana rais anamamlaka ya kumvua mtu ubunge? Naomba shule kidogo wakuu.
 
Ulimsikia au ulisimuliwa?ulibahatika kuunganisha akichozungumza au upeo wako uliishia hapo tu kuwa hajafurahishwa na waziri mkuu..waambie wazazi wako au kaka zako wakusimulie.
Mbona unakuwa mkali, wewe kwa akili yako karne hii ya kujenga hoja haikufai ulitakiwa uishi karne ya 19/20 ambayo binadamu walikuwa wababe kuliko kufikiri
 
Mkuu Mgibeon, kuwafukuza ubunge ni kwamba alitaka kuwatimua uanachama kama Lipumba.
 
Mbona unakuwa mkali, wewe kwa akili yako karne hii ya kujenga hoja haikufai ulitakiwa uishi karne ya 19/20 ambayo binadamu walikuwa wababe kuliko kufikiri
No nimeuliza tu..unajua katengeneza topic kwa taarifa ambayo hana uelewa nayo wa kutosha.
 
Twende taratibu kidogo "aliwahi kufikiria kuwatimua wabunge wote kusini"

Inamaana rais anamamlaka ya kumvua mtu ubunge? Naomba shule kidogo wakuu.
Kuwatimua wabunge ni rahisi tu; anaenda Chamani anawavua uanachama, kazi kwisha.
 
Twende taratibu kidogo "aliwahi kufikiria kuwatimua wabunge wote kusini"

Inamaana rais anamamlaka ya kumvua mtu ubunge? Naomba shule kidogo wakuu.
Anachoweza kufanya ni kuwafukuza kwenye chama na ndio mwisho wao. Otherwise, hana namna nyingine.
 
Bora kajenga uwanja wa mpira tutamkumbuka kwa hili pia

0660DFCA-9477-4784-8E98-045FED6C2F3F.jpeg
 
Raisi hana mamlaka ya kuwatimua wabunge kikatiba. Labda unamaanisha mawaziri...
 
Kasimu yuko vizuri sana, ana huruma na ni binadamu sana!, Naamini kuna ishu nyingine kutokana na utu wake hashirikishwi maana kwa hulka yake hatopenda kuzifanya!

Nilimsikiliza mbunge Bungala (almaarufu Bwege) akieleza jinsi Waziri mkuu alivyolia machozi baada ya Mbunge huyo kumpeleka mtu aliyetolewa jicho kwa kipigo cha polisi ofisini kwa waziri mkuu.

Pia Kasimu ameadjust sana, ameimprove sana, amekuwa Statesman zaidi badala yale mambo ya kufokafoka aliyoanza nayo mwanzoni, yale ni mambo ya kizamani!

Mimi nadhani tatizo siyo Kasimu, Tatizo ni Jiwe!
Jiwe ndiye aliyevuruga hata mambo ya msingi aliyoyakuta.

1. Kakuta sekta binafsi inayoanza kutake off, kairudisha nyuma

2. Kakuta sector ya habari kama magazeti, TV etc zikiwa zinakwenda vizuri kazirudisha nyuma

3. Kakuta vibrant democracy, watu wana freedom of speech, sasa hivi ukiwa kijiweni kuongea dhidi ya serikali lazima uangalie nani yupo miongoni mwenu

4. Kakuta kuna harmony nchini, women empowerment, uongozi wa sura ya kitaifa, lakini angalia teuzi zake, anasema wazi kwamba si zamu ya kaskazini. Angalia teuzi zake, Idadi ya Waislamu aliowateua, ni kiduchu mno, watu wanamwangalia tu afanye analoweza, bora aliyepita alijitahidi kadri alivyoweza kuwa na uongozi unaoreflect composition ya Taifa kwa uwakilishi wa makundi yake

5. Operesheni za kuumiza, bomoabomoa etc

Sasa kwa Mazingira kama haya hata uwe na Waziri Mkuu mzuri kiasi gani huwezi kufika popote!

Jiwe ana option mbili tu, ama akubali kubadirika, au apige zake mark time miaka yake miwili au saba iliyobaki kisha aondoke, sisi turudi square one tuanze ku undo aliyoyafanya tuirudishe nchi katika msitari sahihi.

So far tunatumia nguvu nyingi sana kuliko mipango makini!
 
Ulimsikia au ulisimuliwa?ulibahatika kuunganisha akichozungumza au upeo wako uliishia hapo tu kuwa hajafurahishwa na waziri mkuu..waambie wazazi wako au kaka zako wakusimulie.
Najua wewe ndie mwenye uelewa mdogo wa kufikiri. Kama wewe hukusikia kaa kimya tu. Hii kauri kaisema jiwe
Raisi hana mamlaka ya kuwatimua wabunge kikatiba. Labda unamaanisha mawaziri...
Rais hana mamlaka kumtimua pm. Labda amfute uanachama wa ccm hapo atakuwa amepoteza sifa ya kuwa mbunge hivyo hawezi kuwa Pm.
 
Akimuondoa itakua mwisho wa serikali, PM ndio kila kitu. Kazi ya jiwe ni kubwabwaja tu.
 
Back
Top Bottom