Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,552
- 19,420
Picha hiyo nimeitoa kwa MICHUZIBLOG (Mdau wa Libeneke) Inaomuonyesha rais Kikwete akimkaribisha Makamu wa Rais wa Kenya aliyewakilisha Kenya kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru (wa aibu) wa Tanzania.
Kama Kenya inaona kuwa sherehe kubwa kama hii kwa Tanzania inatosha kuwakilishwa na makamu wa rais wao tu, je inakuwaje yeye anakwenda kila mahali hata ambapo hapana umuhimu wowote?
Presence ya Kenya kwenye sherehe ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika kama sehemu ya Tanzania ni wa muhimu sana kwao kwa vile ni primary beneficiaries wa EAC, lakini bado wanaona kuwa VP anatosha kufanya kazi hiyo.
Kikwete yeye yupo kila mahala hata kwenye shereze za Muswati kuchagua vigoli. Leo baada ya miaka 50, Tanzania bado na dimbwi la umaskini pamoja na raslimali zote tulizo nazo jambo ambalo ni la aibu kweli kweli. Inawezekana makosa ya umaskini wote wa Tanzania siyo ya Kikwete, lakini yeye kwe leo anasaidia kuendeleza dimbwi hilo kwa kasi kubwa sana kuliko kiongozi yeyote aliyemtangulia hasa kutokana na kasi ya maendeleo ya dunia ya leo.