Je Rais wetu anajifunza lolote hapa?

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,552
19,420
attachment.php


m5+%u002525281%2529.jpg

Picha hiyo nimeitoa kwa MICHUZIBLOG (Mdau wa Libeneke) Inaomuonyesha rais Kikwete akimkaribisha Makamu wa Rais wa Kenya aliyewakilisha Kenya kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru (wa aibu) wa Tanzania.

Kama Kenya inaona kuwa sherehe kubwa kama hii kwa Tanzania inatosha kuwakilishwa na makamu wa rais wao tu, je inakuwaje yeye anakwenda kila mahali hata ambapo hapana umuhimu wowote?

Presence ya Kenya kwenye sherehe ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika kama sehemu ya Tanzania ni wa muhimu sana kwao kwa vile ni primary beneficiaries wa EAC, lakini bado wanaona kuwa VP anatosha kufanya kazi hiyo.

Kikwete yeye yupo kila mahala hata kwenye shereze za Muswati kuchagua vigoli. Leo baada ya miaka 50, Tanzania bado na dimbwi la umaskini pamoja na raslimali zote tulizo nazo jambo ambalo ni la aibu kweli kweli. Inawezekana makosa ya umaskini wote wa Tanzania siyo ya Kikwete, lakini yeye kwe leo anasaidia kuendeleza dimbwi hilo kwa kasi kubwa sana kuliko kiongozi yeyote aliyemtangulia hasa kutokana na kasi ya maendeleo ya dunia ya leo.
 
JK ukimfuatilia sana unaweza hata ukajikuta unajitafutia matatizo kuanzia JF mpaka kwa mungu amini nakuambia hayo..

kama yeye ndio kaamua hivyo kosa ni la watz ambao hawataki kuelimika

mungu ibariki tz
mungu ibariki afrika masharika..
 
Huwa napata shida sana wanaotetea kuwa ooh Tz ilikuwa maskini toka kipindi cha mwl. Sawa! Lakini je kuna jitihada za kukabiliana na hilo tatizo?

Mara oh hali ya mbaya ya uchumi ni dunia nzima. Sisi kama Taifa huru tunastrategies gani? Kutokuwa na stategies huru ni sawa na na baba kutohangaika kuwatafutia wanae msosi kisa kaona hata kwa jirani wamelala njaa. Au mwanamme mlevi kukubaliana na mlevi mwenzie kwenda kuwapiga wake zao lkn mwenye akili kwenda kupiga ngoma badala ya mke.

Na hili ndilo linalotakiwa kufanywa na serkali yetu kuwahudumia wananchi wake kwa kutumia utajiri wake wa asili.
 
Kwanini ajifunze kwani wewe unadhani haya anayoamua JK hajui madhara yake kwa Taifa, mimi nalaumu waliomchagua kwanza then mbunge wangu niliyemchagua kwanini alalamiki bungeni hii tabia ya JK maana wananchi ambao hatukumchagua ndio tunaumia.
 
Kwanini ajifunze kwani wewe unadhani haya anayoamua JK hajui madhara yake kwa Taifa, mimi nalaumu waliomchagua kwanza then mbunge wangu niliyemchagua kwanini alalamiki bungeni hii tabia ya JK maana wananchi ambao hatukumchagua ndio tunaumia.

ndugu yangu kama kulalamika watu wanalalamika isue iko kwenye utekelezaji. Ebu imagine suala mswada wa katiba mpk watu wanakufuata ikulu kitu ambacho ni nadra kutokea lkn ni kizunguzungu kwa yanayoendelea. Ebu tuone baada ya jubilee huenda nasi Mungu ataturehemu kama alivyofanya kwa wana wa waisrael baada ya kukaa utumwani babeli miaka 50.
 
Huyu rais wetu hawezi kujifunza kitu.Sababu yeye mwenyewe ameshajikatia tamaa na huo mzigo alionao wa urais wa TZ.Anatafuta namna ya kuutua, autue pazuri au pabaya watajua waTZ.
 
attachment.php


View attachment 43144

Picha hiyo nimeitoa kwa MICHUZIBLOG (Mdau wa Libeneke) Inaomuonyesha rais Kikwete akimkaribisha Makamu wa Rais wa Kenya aliyewakilisha Kenya kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru (wa aibu) wa Tanzania. Kama Kenya inaona kuwa sherehe kubwa kama hii kwa Tanzania inatosha kuwakilishwa na makamu wa rais wao tu, je inakuwaje yeye anakwenda kila mahali hata ambapo hapana umuhimu wowote? Presence ya Kenya kwenye sherehe ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika kama sehemu ya Tanzania ni wa muhimu sana kwao kwa vile ni primary beneficiaries wa EAC, lakini bado wanaona kuwa VP anatosha kufanya kazi hiyo. Kikwete yeye yupo kila mahala hata kwenye shereze za Muswati kuchagua vigoli. Leo baada ya miaka 50, Tanzania bado na dimbwi la umaskini pamoja na raslimali zote tulizo nazo jambo ambalo ni la aibu kweli kweli. Inawezekana makosa ya umaskini wote wa Tanzania siyo ya Kikwete, lakini yeye kwe leo anasaidia kuendeleza dimbwi hilo kwa kasi kubwa sana kuliko kiongozi yeyote aliyemtangulia hasa kutokana na kasi ya maendeleo ya dunia ya leo.

kibaki is too old to roam
 
hii iwe fundisho kwa watz kwamba hatuchagui mtu kutokana na jinsi alivyo presentable, (handsome) bali uwezo wa kuongoza, na sera zenye mantiki.
Wanawake hapo mpo?
 
Nilifikiri hii thread ina chamaana kumbe ni lia lia za wanamagwanda. Jipangeni kwa 2015. Imebaki miaka 3 ya kujipanga. Nafikiri yule rais wenu mnayemtambua akitoka martenity/partenity atakuwa na nguvu ya ziada.
 
JK hana cha kujifunza,huyo ni Vasco Dagama wa Tanzania anataka kila sehemu afike,kama alienda kubembea nchi fulani !!!kwel Tanzania tumepata mzigo sijui tutautua lini
 
Nilifikiri hii thread ina chamaana kumbe ni lia lia za wanamagwanda. Jipangeni kwa 2015. Imebaki miaka 3 ya kujipanga. Nafikiri yule rais wenu mnayemtambua akitoka martenity/partenity atakuwa na nguvu ya ziada.
Tafsiri yangu ya post yako ni kuwa mimi ni lia lia wa Mwagwnada kwa vile ndiye niliyeazisha thread hii. Nakuomaba utambue kuwa swala ninaloongea hapa lina mtazamo mpana zaidi ya unafiki wa kisiasa. Kama nchi ya jirani yako wa karibu anakuletea makamu wa rais kuwakilisha nchi yake kwenye sherehe zako; ina maana kuwa ama rais wao ana shughuli za muhimu nchini kwao kiasi kuwa shughuli za nje hazina nafasi kubwa, au ama shughuli zako hazina uzito mkubwa kwa nchi yao kutuma rais wao kuiwakilisha. Kikwete anatakiwa ajifunze kuwa ama kuna mambo ya anje ambayo hatakiwi kuyahudhuria haka kama amealikwa. Kiprototakali, mialiko yote hiyo itakuja kwake lakini ni jukumu lake kuchambua mialiko hiyo kama kiongozi wa nchi na kuamua ni ipi ahudhurie na ni ipi awakilishwe; siyo kila mwaliko yeye ndiye aende. Kwa hili la Uhuru wa Tanganyika ilikuwa pigo kubwa sana usoni mwake kwa Rais wa Kenya kukataa kuhudhuria hata kwa masaa machache tu kwa vile hapo ni mwenfo mfupi sana kwake, na badala akamtuma makamu wake pamoja na mfale wa kabila moja dogo sana ambalo hata hatulijui.
 
Tafsiri yangu ya post yako ni kuwa mimi ni lia lia wa Mwagwnada kwa vile ndiye niliyeazisha thread hii. Nakuomaba utambue kuwa swala ninaloongea hapa lina mtazamo mpana zaidi ya unafiki wa kisiasa. Kama nchi ya jirani yako wa karibu anakuletea makamu wa rais kuwakilisha nchi yake kwenye sherehe zako; ina maana kuwa ama rais wao ana shughuli za muhimu nchini kwao kiasi kuwa shughuli za nje hazina nafasi kubwa, au ama shughuli zako hazina uzito mkubwa kwa nchi yao kutuma rais wao kuiwakilisha. Kikwete anatakiwa ajifunze kuwa ama kuna mambo ya anje ambayo hatakiwi kuyahudhuria haka kama amealikwa. Kiprototakali, mialiko yote hiyo itakuja kwake lakini ni jukumu lake kuchambua mialiko hiyo kama kiongozi wa nchi na kuamua ni ipi ahudhurie na ni ipi awakilishwe; siyo kila mwaliko yeye ndiye aende. Kwa hili la Uhuru wa Tanganyika ilikuwa pigo kubwa sana usoni mwake kwa Rais wa Kenya kukataa kuhudhuria hata kwa masaa machache tu kwa vile hapo ni mwenfo mfupi sana kwake, na badala akamtuma makamu wake pamoja na mfale wa kabila moja dogo sana ambalo hata hatulijui.
Pole sana ndugu yangu, unapoteza muda kumuelimisha Rejao! Rejao na kundi lake huwahawaelewi chochote chenye kumkosoa Kikwete wao. Kwa Rejao, Kikwete ni malaika na huwa hakosei na ameleta maendeleo na maisha bora kwa kila mtanzania.
 
JK ukimfuatilia sana unaweza hata ukajikuta unajitafutia matatizo kuanzia JF mpaka kwa mungu amini nakuambia hayo..

kama yeye ndio kaamua hivyo kosa ni la watz ambao hawataki kuelimika

mungu ibariki tz
mungu ibariki afrika masharika..
Ibariki na JF yetu iendelee kusonga mbele
 
Kwanini ajifunze kwani wewe unadhani haya anayoamua JK hajui madhara yake kwa Taifa, mimi nalaumu waliomchagua kwanza then mbunge wangu niliyemchagua kwanini alalamiki bungeni hii tabia ya JK maana wananchi ambao hatukumchagua ndio tunaumia.

Jk hakuchaguliwa na mtu, alijichagua mwenyewe kupitia tume ya uchaguzi labda tuseme aliyemchagua ni Lewis Makame
 
Back
Top Bottom