Jamaa Leo wamewasha mtandao lakini pia zimeanza kutiririka meseji kutoka jeshi la Polisi la kuwaasa watu kuepuka kutuma picha au video mtandaoni zenye kuweza kuzua taharuki.
Je, hii si ishara kuwa wanawatisha kisionekane kile Walichokifanya dhidi ya watanzania?
Wakichobaki wanajifariji nacho ni propaganda kuwa waandamanaji wametoka nje ya nchi..
Na kama ni hvyo basi idara zetu ya uslama na uhamiaji zimeoza haiwezekani wageni wote hao waingie nchini na wasambae Dar, Mwanza, Mbeya, Arusha, Dodoma, Tarime, Makambako na kwingineko na wao jushindwa kuwadhibiti.