Je, Ninunue Simu Gani , Samsung au Google Pixel ?
wewe ulisema Apple wananunua camera kutoka Smsung ndio maana nikakupinga na kukuelewesha usijizime data kaka pitia vizuri majibu yako usijitoe ufahamu
We nae mtu mzima akivuliwa taulo huchuchumaa kuficha aibu. Sasa me nachuchumaa wewe unanianika tena. 😂
 
Nishaurini kati ya samsung s10+ na google pixel 6pro,, nachopendelea mwonekano mzuri kwa nje,isiwe nzito au nene,napendelea edged screen,,
 
sio kweli , ingekuwa vizuri ungefanya kwanza research kabla haujaandika ....
utofauti upo hivi...

kwenye pixel simu ya msingi ni plain yaani mfano , pixel 5,6,7,8,9
lakini kutokana na sababu tofauti za kibiashara mfano budget ,prefferences na ushindani wanalazimika kutengeneza model nyingine ili kukidhi soko husika .

kwa wale wanao hitataji simu yenye vitu extra zaidi pixel wamekuja na model za pro
mfano 6Pro, 7 pro nk. hii inakuwa na sifa za ziada zaidi mfano battery yenye uwezo zaidi umbo kubwa, edged screen nk ukilinganisha na ile simu ya msingi (plain).

lakini kuna watu ambao hawawezi kuafford zile simu za msingi,yaani plain ndio kampuni imewaletea model zenye A ,kiuhalisia hazitofautiani sana na zile simu za msingi.

mfano, model za pixel zenye A zinapunguzwa uwezo kidogo kwenye battery, camera ,umbo ,na vitu vingine ambavyo very technical kama refresh rate ya screen.

hata bei zake hazitofautiani sana. mfano hapa kwetu pixel 6 pro ni 680,000, 6plain ni 540,000 na 6a ni 490,000.

na simu zote hizo zinatengenezwa na kampuni ya google yenyewe. kama ilivyo kuwa kwa Apple ambapo model za plus .

kwa Ishue ya samsung A series.

kitu ambacho hujui ni kwamba hizi simu hazitengenezwi na kampuni ya samsung moja kwa moja ,zinatengenezwa na THIRDPARTY companies.

kwa maana rahisi samsung wameuza rigts kwenye kampuni nyingine kutengeneza simu aina nyingine ambazo hazifanani kimuundo na simu za samsung zilizo zoeleka lakini kwa jina la samsung.

kama haujaelewa soma tena hapa...

simu za samsung official nyingi hutengenezwa Indonesia, india na vietnam japo makao makuu yao yapo korea .

lakini kwa samsung A series zote zinatengenezwa china yaani kila kitu, kwa hiyo kampuni ya kichina imenunua rights kwa samsung kutengeneza hizo simu ndio maana ukiangalia hazifanani kwa muundo,na hata performance ndio maana hata bei za Aseries ni rahisi ikilinganisha na S ,NOTE na zile za Zamani za J.

Pia SAMSUNG waliuza rights kwa kampuni ya kichina kutengeneza series za M.

Nimejaribu kukuelezea kwa urefu ili uelewe usipotoshe watu wengine maana ukiandika humu watu wengi wanafuatilia.

by the way kama unahitaji simu au laptop original nicheki 0757468193 hata kama unahitaji ushauri wa kitalamu kuhusu simu na laptop nicheki nikusaidie.

tembelea ukurasa wetu wa instagram kama SIMUKIDIGITALI ujifunzw zaidi
Sasa kama mtu amekutana na Sansung S21 na kamera yake haijafubaa kwa miaka 10 asiseme? 😅😅😅😅
 
sasa hupaswi kusema unirekebishe mimi nimeongea kutokana na research yangu kama vipi na wewe uje na research kaka.
lakini kingine nimejaribu kuchambua advantage na dis advantage za google pixel za samsung over google pixel kiujumla .

kwa maneno rahisi sio samsung zote zipo hivyo ila kwa asilimia kubwa.

kwa nini ?
GOOGLE PIXEL simu zao kutoka toleo la kwanza walikuja na technolojia ya kuzuia vumbi na water resist kwa vimiminika. unaweza itumia google pixel kwa muda mrefu zaidi na mazingira magumu na ikabaki kuwa salama tofuti na samsung ambapo technolojia ya water resistant ni simu chache sana inazo na hizi model kubwa.

kuhusu Apple , labda umechanganya vitu vichache hapo...

Ni kweli APPLE hununua vifaa vyake kutoka kampuni tofauti kuanzia battery , body , mashine, camera nk

Lakini sio kweli APPLE hutumia camera kutoka samsung .... camera za iphone hutengenezwa na SONY ila kutoka SAMSUNG apple wananunua DISPLAY au vioo kwa maneno rahisi labda ulichnganya kidogo hapo mkuu.

lakini all in all point hapo ni kuwa technolojia ya kuzuia vumbi na maji Samsung ipo kwenye simu kubwa tu za hivi karibuni ,lakini iphones na pixel zinahiyo teknolojia .
Research huwa zinakosoa Research ko mtaalamu acha kupaniki mtaalamu, uwe unakubali kukosolewa, ACCEPT CRITICISM, anayekukosoa naye kafanya RESEARCH na huenda ni mtumiaji wa muda mrefu wa kitu anachokwambia ko usipaniki mtaalamu. Hata madaktari wenyewe huwa wanakosea sembuse wewe? Ko mtu akikurekebisha kitu kwenye eneo ambalo una uzoefu nalo usimchukulie NEGATIVELY wewe msikilize tu halafu katafiti zaidi na zaidi halafu uje na RESEARCH RESULTS mpya. Haijakatazwa kutafiti kitu kimoja hata mara 100. Ko usiridhike na knowledge uliyoipata kwa utafiti uliofanya mara moja tu kwenye uuzaji wako wa simu, keep on researching huenda utafiti uliopita kuna vitu hukutafiti vizuri au upendeleo ulikuzidi maarifa ukapendelea BRAND fulani. Ko usikome kutafiti juu ya kitu unachokijua tayari.
 
Mara nyingi huambia watu pixel ni simu kali sana

Asante
Ni kweli lakini ukali haujawa limited to them only, hata Samsung S Series ni kali inategemeana umejikita kwenye criterion gani ya simu.
 
Pengine wewe unayesoma uzi huu unawaza ni lini utapata pesa ya kununua simu lakini kwa mtu mwingine hali ni tofauti kabisa ...!

Kivipi ,? ..... pesa Anayo lakini hajui ni simu gani nzuri atanunua kwa ajili ya shughuli zake . .... Je , Wewe upo kundi gani la kwanza au la pili ?

.........Jibu baki nalo , lakini leo tunazungumzia hasa kundi la pili .

Aina za simu zipo nyingi nzuri lakini leo twende kwanza na hizi brand 2 zinazo zungumzwa sana na zinazopendwa na vijana wengi ukiacha Apple.

Nitakutajia faida na hasara za kila simu hapa chini 👇

Twenzetu ...
Kabla hatujafika mbali !….. Je, Ungetamani kidogo kujua kuhusu mimi ?

Naitwa Mkisi ...
Mtaalamu wa Teknolojia na masuala ya kimtandao , kwa muda wa miaka 7-8 nipo Kariakoo kama muuzaji Muaminifu wa Laptop na Simu .
..... Ningeweza kujieleza zaidi lakini kwa sababu ya kufanya stori kuwa fupi ....

.........kama unahitaji simu na laptop za uhakika nicheki
+255 757468193 WhatsApp na Normal call .

Unaweza kunifuatilia Instagram, Facebook na TikTok kama SIMUKIDIGITALI kwa tips mbali mbali na habari za Teknolojia.
Unaweza pia kujiunga na Group langu la WhatsApp.
Naongea sana eeh .... Tusameheane bhassiii 😀😄.

.....Ngoja niwe serious sasa .
Kwa uzoefu wangu na research yangu asilimia 75 wanaokuja kununua simu dukani hawajui simu wanazotaka wanategemea zaidi muonekano wa nje na influence ya marafiki na muuzaji .

Kwa siku za hivi karibuni napatwa na maswali mengi hasa wateja kushindwa kuamua anunue Google pixel au SAMSUNG ?

Nitachambua simu moja moja hapa 👇 Faida na Hasara zake.

NB. MJADALA HUU HAUTAHISISHA SAMSUNG A SERIES 📌

Samsung.....

.....Faida zake

-Portability (uwezo wa kubebeka)

Kuna baadhi ya matoleo ya samsung ni nyepesi sana kubebeka
Mfano S8 , S9 , S8+ , S9+ , S10 na S10+, s10e ,S20 nk.
Kama hupendi simu yenye umbo kubwa bhasi hayo ni machaguo sahihi.

-Refreshness (High Refreshrate of screen)

Hili lipo Technical kidogo kuelewa , Kwa maana rahisi ni uwezo wa Screen kurespond pale unapotouch na kusense Samsung zipo juu mno huku kioo chake kikiwa na uwezo mkubwa.

- Muonekano

Samsung inamuonekano wa kijanja sana hasa nyingi zikiwa na material ya Glass mbele na Nyuma . Kama unapenda simu yenye muonekano mkali bhasi hizi ni simu chaguo lako .

-Bajeti.

Uzuri Simu hizi zina matoleo Mengi za wale wenye bajeti ndogo na kubwa . Hivyo mtumiaji anaweza kujikadilia kununua simu anayoweza kuimudu .
.
.
.
Hasara....

- Battery... Samsung nyingi ukiachana na matoleo ya hivi Karibuni. Kama S23, S24 , S25 hazitunzi sana charger .

- Camera ...kutokana na maoni ya watu wengi Samsung zinapokuwa mpya zinakuwa na Camera kali lakini kadiri muda unavyozidi kwenda zinafubaa na kama kuinesha ukungu .

-Teknolojia

Samsung nyingi za matoleo ya zamani hazina uwezo mkubwa wa kiteknolijia mfano Ai ,Camera , Settings. Labda kwa matoleo ya hivi Karibuni kama s23 na kuendelea.

- Repair , Simu zimegawanyika katika maeneo 2 (Mashine ) na Kioo .

Vioo vya samsung ambavyo ni Original vinauzwa Ghahama sana , pengine hata thelusi 3 ya bei halisi ya simu .

Mfano kwa simu ya 300,000 sio ajabu kioo chake kuuzwa 220-250k kwa soko la Tanzania.
.
.
.
Google Pixel ....

...... Faida Zake

- Camera ,
Google wanatumia yeknolojia ya hali ya juu kwenye camera (picha na Video zake) zinatoka na Resolution kubwa na hazichuji pia masahihisho yake yanakuja mara kwa mara kuboresha uwezo wake na huwa haifubai haraka.

- Battery,

Google Pixel wanajitahidi kuleta matoleo ambayo wana improve battery capacity inayoweza kukaa na charger kwa muda mrefu kuanzia 6a na kuendelea.

- Teknolojia .

Watumiaji wa Google Pixel wanafaida ya moja kwa moja ya kupata kipaumbele cha teknolojia mpya inavyotambulishwa wao huwa ni watu wa kwanza kupata updates kisha simu nyingine .
Mfano Camera , Kioo cha quality ya juu , Tips mbali mbali ,Ai nk.

- Display Refresh rate .

Kioo cha Google Pixel kimetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zaidi kwenye upande wa resolution pia uwezo wa kurespond haraka na Sensitivity ya hali ya juu pale unapo bofya .

- Muonekano wa Kipekee.

Simu za Google pixel zilizo nyingi hazina maumbo makubwa snaa kulinganisha na Samsung . Aina ya material yaliyo tengenezwa ni ya kung'aa na yanafanya muonekano wa kipekee.

-Bajeti Rafiki .

Google Pixel hazitofautiani sana uwezo kutoka model 1 kwenda nyingine. Hivyo bhasi unaweza kutumia gharama ndogo kupata simu nzuri yenye uwezo mkubwa.

Mfano Pixel 3a ,(280,000) 4a (380,000) 6a( 480,000) 6 ( 520,000) .
.
.
.
Hasara za Google Pixel.

- Inahitajika Ununue Simu yenye uwezo Mkubwa.

Kwa sababu ya uwezo wake wa Camera , hurekodi Video za Quality kubwa na picha zenye mb kubwa hadi 10 .

Hivyo hujaza simu kwa haraka kama ni mtu wa Contents au picha sana unahitaji ununue simu yenye Gb angalau kuanzia 256.

-Haina spair kwa Tanzania (Hasa Vioo)

Kwenye soko la Tanzania simu hizi bado zina ugeni kiasi . Hivyo bado vifaa vyake haipatikani kwa urahisi inapo haribika hasa Vioo vyake unalazimika kupata kutoka kwenye simu nyingine kama hiyo.

-Inahitaji Umakini kuishika.
google pixel imeundwa kwa material ya kuteleza mno, Kama hupendelei kuweka Cover ni rahisi kuchoropoka mkononi na kuanguka ,hivyo Cover na Protector ni Muhimu sana.

Haya #mwanakidigitali hapo Kazi ni kwako ,Uchambuzi huo je, Utanunua Samsung au Google Pixel ?

Sisi SIMUKIDIGITALI,tutakushauri kabla hatujakuuzia simu /Laptop kutokana na Bajeti yako au matumizi yako.

Karibu sana Tunapatikana Kariakoo mtaa wa AGGREY na Msimbazi .

Unaweza kutembelea ukurasa wetu wa Instagram, Facebook na TikTok kama SIMUKIDIGITALI au piga 0757468193.

Usinunue Simu / Laptop hovyo hovyo Zingatia zaidi mahali unaponunua je ni sahihi ?

Thank you .​
Infinix kitochi
 
Hii ndo Simu
IMG_0421.jpeg
 
Back
Top Bottom