Je, ni sawa Rais Magufuli aongezewe muda madarakani?

Je, ni sawa Rais Magufuli aongezewe muda madarakani?

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2017
Posts
392
Reaction score
954
IMG_20200609_172301.jpg
Hivi karibuni mbunge Kessy ametoa wazo juu ya Mhe.Raisi apate kuongezewa muda wa kukaa madarakani. Na Mhe.Spika ameridhia na kusema JPM atake asitake ataongezewa muda.

Kwa mujibu wa katiba yetu ya jamhuri wa muungano ya mwaka 1977, theluthi ya wabunge wakisema ndio basi muswada umepita. Na Kama tunavyojua wabunge wa CCM ni wengi bungeni, kwa namna nyingine huu muswada au hii hoja ikienda bungeni maanake imepita.

Swala si JPM aongezewe muda, swala Ni Tanzania inahitaji kiongozi Bora au taasisi Bora? Tanzania inahitaji taasisi imara au kiongozi imara? Tanzania inahitaji mifumo Bora ya Serikali endelevu au tunahitaji kiongozi Bora endelevu?

Kwanza tujue nchi yetu inahitaji Nini. Tukishajua inahitaji Nini itakuwa rahisi kufanya maamuzi yenye maslahi kitaifa. Tunahitaji maamuzi yenye maslahi kitaifa au maslahi ya chama?

Maslahi yenye tija na Bora kitaifa, Ni kubadili kikatiba Uhuru na utendaji Kazi wa mihimiri mikuu mitatu ya serikali Yani bunge, mahakama na serikali Yani Executive.

Wazo la bunge kutaka JPM aongezewe muda halina maslahi kitaifa Bali Lina maslahi ndani ya chama.

Ipate kufahimika wazi JPM ni binadamu nae atakufa, na akifa maanake uongozi wake thabiti umepotea. Ila tukiweka mifumo ya serikali thabiti na taasisi thabiti chini ya sheria thabiti, mifumo hi ya serikali itabaki miaka na miaka. Kuliko kumpachika mtu aendelee kuongoza eti tu kwa sababu Ni kiongozi mzuri na imara, hayo Ni mawazo ya makalioni.
Ashakumu si matusi.

Hitaji la Tanzania si kiongozi imara au benovelant dictator, hitaji la Tanzania Ni mifumo, taasisi na sheria imara na thabiti.

JPM kwa uimara wake inatupasa tumtumie ili kusimika taasisi hizi na mifumo hii. Na si kumuona Kama ndie kiongozi mteule miaka kumi au ishirini mbele au thelathini mbele.

Bunge linapaswa kwanza lipiganie Uhuru wake na sauti yake juu ya mhimili serikali (Executive) na si kupitisha wazo au muswada wa kumtaka JPM azidi kubaki madarakani.

images (17).jpeg

Bunge la awamu ya tano Ni dhaifu Sana, Tena chini ya spika mdhaifu. Ndugai hajui ukubwa na uthamani wa chombo anachokiongoza.

Kisiasa naweza sema anapekeleshwa na mhimili serikali (executive), wakati Ndugai mhimili wake unapaswa kuwa mhimili mama na mlezi wa taasisi zote za serikali Sasa kwake imekuwa vice versa. Tumhenzi Sana marehemu Samwel Sitta.

Bunge pia lingepaswa kuandaa mifumo Bora ya kiutawala na mifumo ya kupata na kuandaa viongozi imara na thabiti Kama JPM, na si kusimamia mtazamo wa kwamba JPM aongezewe muda.

Je, JPM siku akifa maanake ndio hatupata raisi imara Kama yeye? Mazuri yote aliyofanya JPM ndio yatashindwa kuendelezwa? Alipo ishia JPM hapato endelezwa Tena?
 
Hivi karibuni mbunge Kessy ametoa wazo juu ya Mhe.Raisi apate kuongezewa muda wa kukaa madarakani. Na Mhe.Spika ameridhia na kusema JPM atake asitake ataongezewa muda.

Kwa mujibu wa katiba yetu ya jamhuri wa muungano ya mwaka 1977, theluthi ya wabunge wakisema ndio basi muswada umepita. Na Kama tunavyojua wabunge wa CCM ni wengi bungeni, kwa namna nyingine huu muswada au hii hoja ikienda bungeni maanake imepita.

Swala si JPM aongezewe muda, swala Ni Tanzania inahitaji kiongozi Bora au taasisi Bora? Tanzania inahitaji taasisi imara au kiongozi imara? Tanzania inahitaji mifumo Bora ya Serikali endelevu au tunahitaji kiongozi Bora endelevu?

Kwanza tujue nchi yetu inahitaji Nini. Tukishajua inahitaji Nini itakuwa rahisi kufanya maamuzi yenye maslahi kitaifa. Tunahitaji maamuzi yenye maslahi kitaifa au maslahi ya chama?

Maslahi yenye tija na Bora kitaifa, Ni kubadili kikatiba Uhuru na utendaji Kazi wa mihimiri mikuu mitatu ya serikali Yani bunge, mahakama na serikali Yani Executive.

Wazo la bunge kutaka JPM aongezewe muda halina maslahi kitaifa Bali Lina maslahi ndani ya chama.

Ipate kufahimika wazi JPM ni binadamu nae atakufa, na akifa maanake uongozi wake thabiti umepotea. Ila tukiweka mifumo ya serikali thabiti na taasisi thabiti chini ya sheria thabiti, mifumo hi ya serikali itabaki miaka na miaka. Kuliko kumpachika mtu aendelee kuongoza eti tu kwa sababu Ni kiongozi mzuri na imara, hayo Ni mawazo ya makalioni.
Ashakumu si matusi.

Hitaji la Tanzania si kiongozi imara au benovelant dictator, hitaji la Tanzania Ni mifumo, taasisi na sheria imara na thabiti.

JPM kwa uimara wake inatupasa tumtumie ili kusimika taasisi hizi na mifumo hii. Na si kumuona Kama ndie kiongozi mteule miaka kumi au ishirini mbele au thelathini mbele.

Bunge linapaswa kwanza lipiganie Uhuru wake na sauti yake juu ya mhimili serikali (Executive) na si kupitisha wazo au muswada wa kumtaka JPM azidi kubaki madarakani.

Bunge la awamu ya tano Ni dhaifu Sana, Tena chini ya spika mdhaifu. Ndugai hajui ukubwa na uthamani wa chombo anachokiongoza.

Kisiasa naweza sema anapekeleshwa na mhimili serikali (executive), wakati Ndugai mhimili wake unapaswa kuwa mhimili mama na mlezi wa taasisi zote za serikali Sasa kwake imekuwa vice versa. Tumhenzi Sana marehemu Samwel Sitta.

Bunge pia lingepaswa kuandaa mifumo Bora ya kiutawala na mifumo ya kupata na kuandaa viongozi imara na thabiti Kama JPM, na si kusimamia mtazamo wa kwamba JPM aongezewe muda.

Je, JPM siku akifa maanake ndio hatupata raisi imara Kama yeye? Mazuri yote aliyofanya JPM ndio yatashindwa kuendelezwa? Alipo ishia JPM hapato endelezwa Tena?
HIVI WEWE UNAJUA KWANINI UZI WAKO HAUJAPATA MCHANGIAJI HATA MMOJA TANGU UTUMWE SAA 7 MCHANA NA SASA NI SAA 12 JIONI?
 
Mimi nadhani asiongezewe, kwa sababu kama itafutwa sheria ya ukomo wa Urais ina maanisha kwamba, kila Rais atakuwa na uwezo wa kuongezewa muda. Ubaya wake utakuja pale tutakapopata Rais asiye mzalendo; si itakuwa balaa tupu?
Mimi nadhani badala ya kumwongezea muda, yeye afanye kazi ya kumwandaa mtu makini kabisa, mwenye uzalendo, mfuatiliaji, anayejiamini, mwenye msimamo mkali na mwaminifu ambaye atakuwa Rais baada ya yeye.
 
Mimi nadhani asiongezewe, kwa sababu kama itafutwa sheria ya ukomo wa Urais ina maanisha kwamba, kila Rais atakuwa na uwezo wa kuongezewa muda. Ubaya wake utakuja pale tutakapopata Rais asiye mzalendo; si itakuwa balaa tupu?
Mimi nadhani badala ya kumwongezea muda, yeye afanye kazi ya kumwandaa mtu makini kabisa, mwenye uzalendo, mfuatiliaji, anayejiamini, mwenye msimamo mkali na mwaminifu ambaye atakuwa Rais baada ya yeye.

Watu wanataka mifumo imara, ww unataka yeye akuandalie tena mtu imara!
 
Kwa suala la kuonge zewa muda sihitaji kulizungumzia moja kwa moja. Lakini mifumo duniani kote huwekwa na viongozi. Ukiwa na kiongozi imara na akakaa muda wa kutosha huwacha taasisi imara.

Na sio kinyume chake. Lazima kwanza uwe na kiongozi imara ambae atatengeneza mifumo imara na ndio hapo mifumo imara inaweza kutengeza viongozi imara.

Tuwe wakweli na kwa kujitahidi kuwa wakweli itasaidia kupata michango makini ya yenye kuelimisha.
Wakati wa utawala wa Mh, Mzee Kikwete kila mmoja wetu anafahamu kiwango cha uwajibikaji cha watumishi wa uma katika utoaji wa huduma na tofauti ya hali ya leo. Na kila mmoja wetu anafahamu uwajibikaji wa viongozi wa juu ama wa mashirika au serikali kuu katika matumizi ya fedha za uma , lazima tuyaone haya mabadiliko kwa uwazi.

Kutotambua mabadiliko ambayo yamefanywa na Mh. Magufuli katika kuwawajibisha viongozi wetu pindi wanapofanya makosa ambayo hayavumiliki. Kinyume na kutotambua hili itatupa ugumu kufahamu viongozi wazuri wanatakiwa wawe wa namna gani?.

Tuendelee kupata michango mbali mbali ili uwezo wetu wa uelewa upanuke.

Fifteen leadership qualities that a good leader possess.

Honest and integrity
Confidence
Inspire others
Commitment and passion
Good Communicator
Decision-making Capabilities
Accountability
Delegation and empowerment
Creativity and Empowerment
Empathy
Resilience
Emotional Intelligence
Humility
Transparency
Vision and purpose.
 
Hahahahahahaha nazkia wamepitisha kitu gani sjui kwamba kuna watu ni marufuku kushitakiwa ..anyway emu ngoja tuone itakavokua
 
Hili si sawa kabisa. Yeye sio Mungu wala malaika. Muda wa kikatiba unamtosha sana, hatutaki kuwa na kiongozi wa milele au wa muda mrefu.
 
Nielimishe ndugu.
Achana na kushabikia ccm kabisa. Hiki chama kipo madarakani miaka 60 sasa. Huko tunapokwenda kuomba misaada hawaachii chama kutawala zaidi ya miaka 8 lazima wabadilishe. Sisi tunashabikia chama kimoja miaka 60 halafu tunakwenda kuomba omba, wanatucheka na kutushangaa sana.

Ushabiki wa ccm hapa Tz upo zaidi mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo. Ukiendea mikoa ambayo watu wake wana uelewa wa mambo na wapo vizuri zaidi kiuchumi kama vile Dar es Salaam na Kilimanjaro utaona watu walishaachana na ccm kwa kiasi kikubwa. Inashangaza nyie vijana mliozaliwa mkaikuta ccm bado mnashabikia chama hiki ndio maana hatuendelei.
 
Achana na kushabikia ccm kabisa. Hiki chama kipo madarakani miaka 60 sasa. Huko tunapokwenda kuomba misaada hawaachii chama kutawala zaidi ya miaka 8 lazima wabadilishe. Sisi tunashabikia chama kimoja miaka 60 halafu tunakwenda kuomba omba, wanatucheka na kutushangaa sana.

Ushabiki wa ccm hapa Tz upo zaidi mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo. Ukiendea mikoa ambayo watu wake wana uelewa wa mambo na wapo vizuri zaidi kiuchumi kama vile Dar es Salaam na Kilimanjaro utaona watu walishaachana na ccm kwa kiasi kikubwa. Inashangaza nyie vijana mliozaliwa mkaikuta ccm bado mnashabikia chama hiki ndio maana hatuendelei.
Apo ulipo agiza kinywaji mkuu ntalipa
 
Kwa suala la kuongewa muda sihitaji kulizungumzia moja kwa moja. Lakini mifumo duniani kote huwekwa na viongozi. Ukiwa na kiongozi imara na akakaa muda wa kutosha huwacha taasisi imara.

Na sio kinyume chake. Lazima kwanza uwe na kiongozi imara ambae atatengeneza mifumo imara na ndio hapo mifumo imara inaweza kutengeza viongozi imara.

Tuwe wakweli na kwa kujitahidi kuwa wakweli itasaidia kupata michango makini ya yenye kuelimisha.
Wakati wa utawala wa Mh, Mzee Kikwete kila mmoja wetu anafahamu kiwango cha uwajibikaji cha watumishi wa uma katika utoaji wa huduma na tofauti ya hali ya leo. Na kila mmoja wetu anafahamu uwajibikaji wa viongozi wa juu ama wa mashirika au serikali kuu katika matumizi ya fedha za uma , lazima tuyaone haya mabadiliko kwa uwazi.

Kutotambua mabadiliko ambayo yamefanywa na Mh. Magufuli katika kuwawajibisha viongozi wetu pindi wanapofanya makosa ambayo hayavumiliki. Kinyume na kutotambua hili itatupa ugumu kufahamu viongozi wazuri wanatakiwa wawe wa namna gani?.

Tuendelee kupata michango mbali mbali ili uwezo wetu wa uelewa upanuke.
Tunaona na jinsi demokrasia ilivyokufa, uhuru wa habari ulivyokufa, bunge kugeuka taasisis ya rais, kupeana madaraka kikabila, kuzawadiwa madaraka, kuteswa kwa wapinzani, kuuwawa kwa wanasiasa, upendeleo wa miradi mikubwa kikanda,...ukabila, ...Hayo ndio mabadiliko makubwa yanayoonekana awamu hii.
 
Tunaona na jinsi demokrasia ilivyokufa, uhuru wa habari ulivyokufa, bunge kugeuka taasisis ya rais, kupeana madaraka kikabila, kuzawadiwa madaraka, kuteswa kwa wapinzani, kuuwawa kwa wanasiasa, upendeleo wa miradi mikubwa kikanda,...ukabila, ...Hayo ndio mabadiliko makubwa yanayoonekana awamu hii.
Mwaba tuvushe ndio chaguo letu 2020
 
Miaka 5 watu wako hoi kiuchumi kwa kusomeshwa namba,vipi another yrs si tutazikwa kabisa
 
kumpta Rais mwengine mfano wa Dr.Magufuli itatuchukua miongo kadhaa.....ni afadhali atusogeze miaka mingi zaidi...maana nchi yetu ilitafunwa sana! na watafunaji wapo pembeni wana njaa ya kufa mtu wanatamani aondoke hata leo waendelee kuitafuna nchi hii, kamwe hatuwezi kukabidhi nchi yetu kwa waroho na walafi.
chini ya Magufuli nchi yetu iko salama sana, kamwe sinto poteza kura yangu mwezi october zaidi ya kumpa mtu mwaminifu Magufuli
 
Back
Top Bottom