Je ni sahihi kuweka uzungu kwenye majina ya kikabila?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Waungwana,
Kuna kitu kimekuwa kinanitatiza kwa kipindi kirefu. Kitu hiki kinahusu kugeuza majina ya kikabila na kuyapa uzungu bila sababu za msingi.Labda kuna sababu ambayo siijui. Inakuwaje kwa mfano mmaasai anayeitwa Laiza kugeuza jina na kujiita " Laizer/Laiser", au mchaga anayeitwa Hoi-se na kujiita "Hoyce"..
wapo pia wale wanaoongeza "s" mwisho wa majina yao kama "Mnzavas", "Matingas" au kugeuza kabisa jina kama vile Juma kujiita " "Jimmy"
Inakuwaje hii? watu wanaonea aibu majina yao au wanafikiri kuyapa nakshi ya kizungu/kigeni ndio ujiko?Nahitaji somo hapa.
 
Woman of substanc...kwa Kiswahili maana yake nini? Mbona mnatumia Kizungu jamani?Labda tujadili hili lako kwanza..jibu la swali lako litapatikana hapo!
 
Woman of substanc...kwa Kiswahili maana yake nini? Mbona mnatumia Kizungu jamani?Labda tujadili hili lako kwanza..jibu la swali lako litapatikana hapo!


Mkuu swali lako sijakupata..unataka maana ya majina hayo kwa kiswahili au?Kama ndivyo basi nitawaomba wenye kujua maana yake watujuze.

Ninachotaka kijadiliwe hapa ni kwanini majina hayo yasiandikwe vile inavyotakiwa badala ya kuyapamba kuyawekea " er", au "s" mwisho au kubadili kabisa na kuyawekewa herufi zisizohitajika alimradi yatamkike kizungu.Hayo majina ni ya makabila husika ila wanayaandika kizungu.
 
Woman of substanc...kwa Kiswahili maana yake nini? Mbona mnatumia Kizungu jamani?Labda tujadili hili lako kwanza..jibu la swali lako litapatikana hapo!

Mkuu,
Wos ni utambulisho tu hapa na si jina langu hahahahahah!!
 
Juma=Jimmy??? that's hillarious. Cultural inferiority complex seems to be the problem here
 
Accademia school maana yake nini? Naomba nielimishwe kwa Kiswahili,wengine Lugha ya Kiingereza inatupiga chenga!
 
Accademia school mkuu

Mkuu,
kama ni kuonekana msomi... kwani majina yetu ya kiasili yanatupunguzia usomi wetu? mbona hayo majina ya kienyeji yanayorembwa yaonekane ya kizungu mbona ndo yanachekesha zaidi?
Chukulia mfano jina kama Juma - unapoligeuza kuwa Jimmy unapoteza maana halisi na hata ile identity.Juma nijuavyo mimi ni jina la kiislamu wakati Jimmy ni shortform ya James ambalo ni jina la kikristo.Si ni upotoshaji huu?(angalizo: huu ni mfano tu maana watu hawakawii kuanza malumbano ya kidini hata kwenye ishu ndogo kama hii!)
 
Mkuu,
Wos ni utambulisho tu hapa na si jina langu hahahahahah!!
kazi hasa...kwani jina maana yake ni nini? si utambulisho......mfano naitwa Jamila ili watu wanitambue kama Jamila......au?.......jina lako tatizo hebu tujibu kwanza weye kwanini ukajiipachika utambulisho wa jina la kizungu?
 
Mkuu,
kama ni kuonekana msomi... kwani majina yetu ya kiasili yanatupunguzia usomi wetu? mbona hayo majina ya kienyeji yanayorembwa yaonekane ya kizungu mbona ndo yanachekesha zaidi?
Chukulia mfano jina kama Juma - unapoligeuza kuwa Jimmy unapoteza maana halisi na hata ile identity.Juma nijuavyo mimi ni jina la kiislamu wakati Jimmy ni shortform ya James ambalo ni jina la kikristo.Si ni upotoshaji huu?(angalizo: huu ni mfano tu maana watu hawakawii kuanza malumbano ya kidini hata kwenye ishu ndogo kama hii!)

Musa - Moses

Hawa - Eve

Juma - James

Daudi - David

Bahati - Hope

Furaha - Happy/ness ...nk nk...nk....majina sio kigezo cha imani ya Dini kama tunavyoona kina Augustino Ramadhani, Said John, nk...

sidhani kama kuna ubaya wowote kuweka "nakshi" kwenye jina ulopewa na wazazi wako, unless ni jina linalohitaji kilitamka bila kujiuma ulimi...mfano la brother KINJEKETILE KINGUNGE NGOMBALE MWIRU, UKIWAONA MZUZURI DITOPILE, au KILONSI MUHAMA MPOROGONYI.
 
WoS, watu wanatumia majina ya kizungu just to suit their ego. Kutokana na kujisikia raha ya moyoni jina lako kutamkwa kwa jinsi ile unayoitaka. Karibu majina yote ya kizungu, yana ya Kiwahili yake, mfano John ni Yohana, James ni Yakobo, Mark ni Mariko, Luke ni Luka, Mary ni Maria, Joseph ni Yusufu. Moses ni Musa etc. Yoyote kati ya hao ambaye amepewa jina la kizungu hatakubali kuitwa lile la kiswahili chake hata kama huo ndio ukweli wenyewe.

Sasa ukiachina uzungu, maneno na majina yote ya kibantu ni lazima yanaishia na irabu (vowels) a,e,i,o na u. Jina lolote la kibantu nje ya hapo ni uzungunaizesheni. Wachaga ndio wanaongoza na Wahaya wangefuatia kama wangeweza. Mungi ni Mungy, Mmari ni Mmary, Moshi ni Moshy, Mushi ni Mushy, Kundi ni Kundy etc

N.B, naomba uutenganishe huu uzungunaizesheni na makabila ya Tanzania ambao sio Wabantu kama Nilotic,Semi Nilotic, Wairaque na Bushmen, hawa lugha yao haitumii alphabeti ya kawaida hivyo katika kuandika maneno na majina yao, ni kufuata matamshi kwa kukopa maneno ya hii alphabeti ili japo yaandikike. Haya ni makabila ya Arusha, Singida na Dodoma ukiondoa Wagogo na Wameru ambao ni wa Bantu. Wamasai, Wambulu, Wabarbaig, Wasandawi, Warangi, Wanyaturu sio wabantu. Ukiona consonants mwisho wa majina yao, ni mkopo tuu ili yatamkike.
 
Musa - Moses

Hawa - Eve

Juma - James

Daudi - David

Bahati - Hope

Furaha - Happy/ness ...nk nk...nk....majina sio kigezo cha imani ya Dini kama tunavyoona kina Augustino Ramadhani, Said John, nk...

sidhani kama kuna ubaya wowote kuweka "nakshi" kwenye jina ulopewa na wazazi wako, unless ni jina linalohitaji kilitamka bila kujiuma ulimi...mfano la brother KINJEKETILE KINGUNGE NGOMBALE MWIRU, UKIWAONA MZUZURI DITOPILE, au KILONSI MUHAMA MPOROGONYI.

Mkuu with all due respect,
Sidhani kama kuna ubishi katika hiki unachokisema hapo juu.
Hoja yangu iko palepale... sizungumzii kutafsiri majina la hasha.Wala sijauliza kwanini watu wawe na majina ya kizungu, kihindi,kiarabu,etc.

Issue ni : kwanini usiandike jina lako inavyopaswa na badala yake ujaribu kuongezea huko "er" au "s " au "y" etc? Kama naitwa mathalani " Uledi" kwanini niongezee d na y isomeke "ULEDDY"au kama jina langu ni Mwanamkasi nijiite " Mwanamkassey"........ni hicho tu!
 
kazi hasa...kwani jina maana yake ni nini? si utambulisho......mfano naitwa Jamila ili watu wanitambue kama Jamila......au?.......jina lako tatizo hebu tujibu kwanza weye kwanini ukajiipachika utambulisho wa jina la kizungu?

Hii ni mada nyingine mkuu..
unaweza kuniuliza badae lakini hoja yangu iko palepale....
 
Hii ni mada nyingine mkuu..
unaweza kuniuliza badae lakini hoja yangu iko palepale....
thread inahusu majina ya kibantu/kizungu.....huwezi kupata jibu wakati na weew una jina la kizungu.......jibu swali na ndio unatapa majibu ywa kwanini kaiza akajiita kaizer......
 
WOS
Naamini jamii tunayoishi kuna watu wengine wana majina ya kibantu na wengine ya kizungu. Hivyo basi mtu mwenye jina la kibantu anaweza kulirembesha kiswanglish zaidi yaani lionekane pia ni la kitasha fulani.
Ni kwa mtu binafsi zaidi anavyojisikia,sidhani watu ote wenye majina ya kibantu wanaongezea manjonjo Tangia hapo majina mengi ya kibantu ni unique na yana maana kutokana na matabaka ya watu kwenye makabila yao.
 
thread inahusu majina ya kibantu/kizungu.....huwezi kupata jibu wakati na weew una jina la kizungu.......jibu swali na ndio unatapa majibu ywa kwanini kaiza akajiita kaizer......


yOyO
kwa vile umesisitiza sana..Nitakujibu kwa kifupi kama ifuatavyo:
A. Women of substance - siyo jina langu mimi au la mtu yeyote bali ni mkusanyiko wa wanawake zaidi yangu mimi wenye kuwakilisha kitu fulani.
B.Mimi kama mimi nina hiari kutumia lugha yeyote ile kuwakilisha mawazo yangu.Ningeweza kutumia lugha zote ninazozifahamu kuwakilisha, ila kwa faida ya wengi nimetumia kiingereza kwa maana ni lugha inayotumiwa na wengi hata kama si wote.
C., Ningeweza kutumia jina langu la kibantu na lenye kuandikwa kibantu bila er, s au Y mwisho lakini maadam sitaki kujulikana hapa kwa jina langu halisi basi yatosha kutumia WoS!
Asante kwa kunielewa
 
Ushamba tu watu kuona majina ya kizungu ni mali !

And it is only in Afrika tumecopy kila kitu cha wazungu...angalia China, Japan have kept their names!

Ajabu US/Ulaya hakuna wanaocopy majina yetu!

Ni swala la mindset yetu sisi haswa Waafrika!
 
Hata waandishi wa habari wanachangia kuvuruga jinsi majina yanavyotakiwa kuandikwa. Kwa mfano, mimi huwa sioni sababu ya gazeti kuandika "Machuppa" badala ya "Machupa", sasa hata Machupa inahitaji iwekewe double p? Kuna mengi tu, kama Pawassa, Wassira, EL naye wanamuwekea double s, etc. Usishangae siku moja Rwechungura ikaandikwa Rwechungurra !!
 
Back
Top Bottom