Je, ni mapenzi au ana lake jambo?

Je, ni mapenzi au ana lake jambo?

XII Tz

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2020
Posts
4,350
Reaction score
7,102
Tuliachana mwezi January mwaka 2018, kila mtu aka-move on na yakwake, binafsi niliumia sababu nilimpenda kweli na yeye alinipenda ila kama unavyojua sababu tu za kiufundi za hapa na pale zikatutenganisha.

Nikiri tu kuwa shinikizo kubwa la mimi na yeye kuachana ilikua ni rafiki zake. Rafiki zake walichangia pakubwa sana sisi kuachana na haikuishia hapo wakamjaza maneno akawa anatema shombo sana juu yangu, kama mwanaume wala siku-react, nikaona ni mambo ya kawaida tu yatapita.

As people say, time heals everything, with time I started getting better and I reached a point where I completely forgotten about her. Lakini pamoja na kuwa tulisha-move on karibia miaka 5 nyuma, yeye bado anaonyesha wivu sana juu yangu.

Bado anaonekana kuumia sana anionapo na mwanamke mwingine, na inapowezekana atatumia njia yeyote hata ya kusambaza sumu ili ahakikishe tumeachana, kuna muda tulikua tuki-chat Ile kishkaji tu ila through her conversations unaona kabisa kuna kitu ana push.

Kuhusu kimuonekano nisiwe muongo ni binti mzuri sana, ambaye almost kila mwanaume angependa kuwa naye, na ninawaona vijana wanavyopishana kwake. Ila ndo hivyo tu, sisi wengine tumejaaliwa mioyo migumu hatupelekeshwi na wanawake, ukileta miyeyusho unapita kushoto.

Basi ndo hivyo wakuu, najua humu kuna wakubwa zangu wenye experience kubwa kwenye hii sekta, naombeni ufafanuzi au ushauri wenu. He haya ni mapenzi au mchawi tu?

Naombeni kuwasilisha
 
Tuliachana mwezi January mwaka 2018, kila mtu aka-move on na yakwake, binafsi niliumia sababu nilimpenda kweli na yeye alinipenda ila kama unavyojua sababu tu za kiufundi za hapa na pale zikatutenganisha.
Uchawi tu
 
Unadanganya kuwa mliachana na bado mnawasiliana! Kama mmeachana kwake huna mtoto, hukumpa Figo unawasiliana nae vitu gani? Nyie bado mnapendana ukijumlisha na utoto mlionao mnatuchezea kamchezo kakombolela.

Haya mmefikia wapi atakuja kwako au mtakutana tu sehemu mpashe kipolo?
 
Mbona inaonekana kua wewe ndio unaumia juu yake? mpaka unajua kua vijana wanapishana kumuwania? unajifanya eti una moyo mgumu kumbe huna lolote,nyie vivulani mmezidi kutujazia server za JF kwa vithd vya kifala,

Unataka ushauri gani na umesha sema kua mlisha achana na kila mtu ame move on? after 5 years ila bado huja move on!
 
Una bahati sana. Muda mlioachana umeweza kupata picha halisi ya wanaume wanaomzunguka. Kimbia mbali naye. Watu wanchomwa kwa mkaa, risasi 7 mfulilizo, katana kichwa, chomewa ndani ya nyumba kwa sababu ya VIVU WA MAPENZI. Tafuta mwanamke wa kawaida sio anayekokota wanaume rundo.
 
Sasa na ww ushaachana naye mawasiliano ya nini????PIGA CHINI UNAJIFANYA UNA MOYO MGUMU KUMBE HAMNA KITU,huyo bado unamtaka ustuzuge mkuu
Yeye ndo anaanzaga kunitafuta mkuu, alafu mimi sinaga muda wa kuwekeana vinyongo na mtu kwahiyo Huwa najibu tu text zake kama kawaida.
 
Unadanganya kuwa mliachana na bado mnawasiliana! Kama mmeachana kwake huna mtoto, hukumpa Figo unawasiliana nae vitu gani? Nyie bado mnapendana ukijumlisha na utoto mlionao mnatuchezea kamchezo kakombolela.

Haya mmefikia wapi atakuja kwako au mtakutana tu sehemu mpashe kipolo?
Yeye ndo anaanzaga kunitafuta, na mimi sina kinyongo nae, kwahiyo huwa najibu tu meseji zake.
 
Mbona inaonekana kua wewe ndio unaumia juu yake? mpaka unajua kua vijana wanapishana kumuwania? unajifanya eti una moyo mgumu kumbe huna lolote,nyie vivulani mmezidi kutujazia server za JF kwa vithd vya kifala,

Unataka ushauri gani na umesha sema kua mlisha achana na kila mtu ame move on? after 5 years ila bado huja move on!
Mkuu ni long story ila nimefupisha tu, alafu kuna vitu vipo obvious na pia tunaishi karibu so kujua bitu kama hivyo ni obvious.
 
Una bahati sana. Muda mlioachana umeweza kupata picha halisi ya wanaume wanaomzunguka. Kimbia mbali naye. Watu wanchomwa kwa mkaa, risasi 7 mfulilizo, katana kichwa, chomewa ndani ya nyumba kwa sababu ya VIVU WA MAPENZI. Tafuta mwanamke wa kawaida sio anayekokota wanaume rundo.
Asante kwa ushauri wako mkuu..
 
Back
Top Bottom