Je, ni kweli Ugali wa Dona ni bora kuliko wa Sembe?

Mleta mada nakusifu kwa kuandika makala hii ndefu..

Mimi pia ni mtaalamu wa Nutrition lakini kiukweli ni mvivu kuandika...
Umenena vizuri sana mkubwa, mwenye macho na aone asisubr kuadithiwa, wanaume wa dar washazoea kula sembe afu miguu juu kutizama season mazoezi hawafanyi matokeo yake kila mtu ana kitambi na uzito uliokithiri
 
Umeeleza vzr sana mzee lkn umesahau kitu kinachoitwa mfumo wa utoaji taka mwilini kulingana na mwenyewe maelezo yako hapo juu tu Dona litabaki kuwa bora kwakuwa unapata choo kwa haraka na chepesi kuliko Sembe ambapo waweza kaa hata wiki nzima bila kupata haja inayoeleweka na ukijakutoa utakunya kma mbuzi wacha tupige Dona bwana
 
Da nimekaribia kufika mwishoni but sijamaliza maana nimeona mengi umeyarudia kwa kutumia lugha tofauti,swali langu ni moja kwa nini unga wa sembe uzalishe glucose nyingi kuliko dona huku sembe imetokana na dona??? na katika maelezo yako hujaseme kama kuna virutubisho vyovyote labda vinaongezwa kwenye sembe??
Hilo ni swali zuri sana.

Hata Mimi nilipiga hesabu Kama zako.

Kwamba mahindi ya dona ndio sources ya mahindi ya sembe.

How comes mahindi yaliyopunguzwa baadhi ya virutubisho yakawe bora kuliko yale ya asili.
 
Nianze kwa kumshukuru mtoa mada kwa mada yako nzuri. Niseme tu mimi nimevutiwa na sehemu moja tu kwenye mada yako nayo ni "Sumu kuvu" japo wewe umeiita sumu kuvu (jina siyo sahihi). Mimi binafsi nataka niongezee hapo kwenye sumu kuvu maana ni eneo langu ambalo nimelifanyia utafiti na ninaendelea kulifanyia utafiti.

Sumu kuvu ni Sumu unayozalishwa na fungi aina ya "Aspergillus" fungi hawa imeripotiwa wanavamia sana nafaka wakati wa kuvuna, kusafirisha mazao, wakati wa kuyaongezea thamani mazao na wakati wa kuyahifadhi. Mahindi na karanga ndio mazao mama yanayoonekana kuvamiwa na fungi hawa kwa wepesi ukilingamisha na mazao mengine, kwasababu mada yetu ni ugali naomba nijikite kwenye mahindi zaidi.

Kama nilivyo sema mahindi na karanga ndo mazao mama yanayoshambuliwa na fungi hawa wanaosababisha sumu kuvu kuliko mazao mengine yote, hivyo basi kushambuliwa kwa mahindi kunaweza kupunguza usalama wa ugali pia. Swali la msingi ambalo tunatakiwa kulijua ni sehemu gani ya mahindi ambayo inashambiwa na fungi hawa?

Ukweli ni kwamba ganda la juu la mahindi ndo mhanga wa kwanza wa shambulio hilo, na ndipo sumu kuvu huzalishwa kwa wingi. Kitu pekee cha kuelewa zaid sumu kuvu ni compound zikibahatika kuingia mwilini kwa kiwango kizuri zinaweza kusababisha kansa, na compound (chemikali) hizi hiziodolewi kwa kuosha au kuchemsha au kupika (very stable compound).

Njia moja ya kupungu kadhia hii ni kutoa ganda la juu la mahindi, japo haiondoi tatizo kwa asilimia mia lakini inapunguza tatzo. Kwa matiki hiyo basi Mtu anaye kula dona kwa sana anauwezekano mkubwa wa kupata matitizo yatokanayo na sumu kuvu.

Hitimisho:
"Ugali wa sembe" ni bora kiafya kuliko "Dona", kwasababu tumeona kwakutoa maganda ya juu ya mahindi yaani kukoboa kunapunguza sumu kuvu kwenye mahindi pia ugali.

Mwisho kabisa Dawa zinazotumika kutunza mahindi wakati wa kuyahifadhi au wakati wa kulima siyo chazo cha sumu kuvu kama mtoa mada alivyotaka kusema, bali wadudu (insect) wanaovamia mahindi ndo chazo kikubwa cha sumu kuvu, pili uhifadhi mbaya wa mazao (mahindi) ni chazo kikubwa cha sumu kuvu, kuhifadhi mazao kwa muda mrefu nichazo pia cha sumu hii, kulima mazao kwenye maeneo ya ukame kunaongeza hatari ya mazao kupatwa na sumu hii na kuchelewa kuvuna mazao au kuyavuna mabichi yaweza kuongeza tatizo hili.

Kwakuhitimisha njia pekee ya kupunguza tatizo is la sumu kuvu ni kutumia njia bora za kilimo na uhifadhi mzuri wa mazao baada ya kuvunwa, lakini njia ya kupunguza tatizo hili ni kukoboa mahindi yaani kutumia sembe badala ya dona.

Therefore sembe is better than Dona, nimekubaliana na hoja zako zote za kibaiologia, Mimi ni Mchemia by professional.
 
...wa Dar katika kutetea sembe...

Endelea kushangilia glucose kujazwa mwilini

Endelea pia kushangilia kupata virutubisho kutoka vyakula ambavyo ni artificial

Tuache sisi tuendelee na dona ilimradi tu ni ratified
 
Wewe kuwa alive sio guarantee kwamba ulaji wa dona ni salama.

Anyway endelea kula dona mpaka uwe dona kantree(donor country)ile ya magu
Unaongea usichokijua, ninaandika haya kwa sababu najua na ninajua kuwa najua. hata hivyo usijali endelea kula ukipendacho. Very likely uko kwenye group la elite, the brain washed ones. Ila fahamu kuwa nina kijua chakula kuliko wewe
 
Nianze kwa kumshukuru mtoa mada kwa mada yako nzuri. .........
Therefore sembe is better than Dona, nimekubaliana na hoja zako zote za kibaiologia, Mimi ni Mchemia by professional.
Asante kwa post.
Sijui tumesoma wapi, sijui!!!
Sijui sample size yako ya utafiti kuhusu hiyo "sumu kuvu" ipoje!!!!
Kama kweli mpo serious, na hilo la sumu kuvu, nilitarajia mtakuwa mnaendelsha kampeni kali ya kufa mtu kupiga vita ulaji wa karanga, ambazo ni mostly contaminated with it.

Jibu ni hapana, why?

Ni wazi hoja yako haina mashiko kwa sababu, sumukuvu huzalishwa kwenye chakula ambacho hakijakauka vizuri. Kwa bahati nzuri Tanzania iko ukanda wa tropical ambao una jua saa 24/7.

Soma kazi nzuri ya PhD ilifanywa na Dr.mmoja (sitaji jina lake) wa SUA akiwa chuoni Australia kuhusu sumu kuvu kwenye mahindi. He didn't end up his work with this nonsense conclusion. Msituletee conclusion za akina Trump za majuzi kuwa maziwa ya kopo ni mazuri kuliko ya mama.

Yes that how your conclusion is, mnapata wapi ujasiri wa kusema "mahindi yaliyopunguzwa baadhi ya virutubisho ni bora kuliko yale ya asili. Mlienda shuleni kufanya nini? Even if all members will support this stupidity, I will not, I better stand alone on this. Tukutane uzeeni
 
Unaongea usichokijua, ninaandika haya kwa sababu najua na ninajua kuwa najua. hata hivyo usijali endelea kula ukipendacho. Very likely uko kwenye group la elite, the brain washed ones. Ila fahamu kuwa nina kijua chakula kuliko wewe
Sawa
mjuzi wa chakula kuliko mimi
 
Dona ndio bora kuliko sembe, nyingine ni blah blah tu kwa sababu sembe ni tamu na inavutia kuliko dona.
 
Dona ndio bora kuliko sembe, nyingine ni blah blah tu kwa sababu sembe ni tamu na inavutia kuliko dona.

Dona la kulima mwenyewe na kuandaa mwenyewe na sio hii ya kununua madukani
 
Back
Top Bottom