Kalamu Nzito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 318
- 662
Baadhi ya wakristo na hata waislamu wanaamini kwamba hakuna tena manabii kwa sasa. Waislamu wanaamini baada ya Mtume Muhammad (S.A.W) hakuna mtume aliyetokea na hakuna atakayetokea mpaka kiama. Sitaki kugusia sana upande huo maana sifahamu maandiko ya Quran yanasemaje.
Kwa upande wa wakristo, utume na unabii ni karama na karama hizi hazikuishia kwenye Biblia. Ili Mungu atende kazi zake ni lazima awafunulie watu wake wenye karama hiyo kwa faida ya wengine (AMOSI 3:7)
Hivyo mitume wapo na manabii pia wapo na wataendelea kuwepo mpaka mwisho wa ulimwengu huu. Hata hivyo uwepo wao umekua kichaka cha matapeli. Hilo halibatilishi ukweli kwamba Manabii wa ukweli wapo na unabii unatendeka.
NB: Wale wasioamini katika maandiko matakatifu na uwepo wa Mungu msipoteze muda hapa ili muonekane mnajua sana au ni wajanja kuliko wanaoamini. “Busara” zenu zitunzeni kwaajili ya vizazi vyenu.
Kwa upande wa wakristo, utume na unabii ni karama na karama hizi hazikuishia kwenye Biblia. Ili Mungu atende kazi zake ni lazima awafunulie watu wake wenye karama hiyo kwa faida ya wengine (AMOSI 3:7)
Hivyo mitume wapo na manabii pia wapo na wataendelea kuwepo mpaka mwisho wa ulimwengu huu. Hata hivyo uwepo wao umekua kichaka cha matapeli. Hilo halibatilishi ukweli kwamba Manabii wa ukweli wapo na unabii unatendeka.
NB: Wale wasioamini katika maandiko matakatifu na uwepo wa Mungu msipoteze muda hapa ili muonekane mnajua sana au ni wajanja kuliko wanaoamini. “Busara” zenu zitunzeni kwaajili ya vizazi vyenu.