Sio siri kuwa aliyekuwa waziri wa mazingira Theresa Huvisa alikuwa mwiba sana kwa wale wote waliokuwa wamejenga nyumba zao ufukweni kwa kuvunja sheria; alisimamia sheria na kusababibisha nyumba nyingi za matajiri kubomolewa kule ufukweni na hivyo kuchukiwa sana na hao waliohusika wakiwemo wabunge wenzie!!!
Mbunge mmoja wa chama tawala amejenga hekalu lake huko Mbezi beach kinyume na sheria na pale sheria ilipotaka kuchukua mkondo wake akakimbilia mahakamani kuweka stop order iliyoinusulu nyumba yake isivunjwe mpaka hivi sasa!! Toka huyu mama kuondolewa kwenye madaraka, kasi ya kujenga ufukweni kinyume na sheria imerudi tena na cha kushangaza zaidi ni kuona kuwa hapo karibu ya nyumba ya huyo mbunge aliyejenga huko Mbezi beach kinyume na sheria fisadi mwingine anajenga hekalu lake kwa kasi ya ajabu ingawa mamlaka husika zimemuwekea notisi kuwa asiendelee kujenga!! Je serikali itakaa kimya mpaka amalize kujenga hilo hekalu lake ndio ilibomowe? Je,kasi hii ya ujenzi holela huko Mbezi beach baada ya yule mama kuondolewa ni ushahidi kuwa mafisadi wameiweka serikali mifukoni kwa sababu ya hela zao?
Mbunge mmoja wa chama tawala amejenga hekalu lake huko Mbezi beach kinyume na sheria na pale sheria ilipotaka kuchukua mkondo wake akakimbilia mahakamani kuweka stop order iliyoinusulu nyumba yake isivunjwe mpaka hivi sasa!! Toka huyu mama kuondolewa kwenye madaraka, kasi ya kujenga ufukweni kinyume na sheria imerudi tena na cha kushangaza zaidi ni kuona kuwa hapo karibu ya nyumba ya huyo mbunge aliyejenga huko Mbezi beach kinyume na sheria fisadi mwingine anajenga hekalu lake kwa kasi ya ajabu ingawa mamlaka husika zimemuwekea notisi kuwa asiendelee kujenga!! Je serikali itakaa kimya mpaka amalize kujenga hilo hekalu lake ndio ilibomowe? Je,kasi hii ya ujenzi holela huko Mbezi beach baada ya yule mama kuondolewa ni ushahidi kuwa mafisadi wameiweka serikali mifukoni kwa sababu ya hela zao?