Je, ni kwanini wenye magari hung'ang'ania kuvuka kwenye kivuko badala ya kutumia daraja la Nyerere?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,066
40,725
20180409_184809.jpg

Mara zote huwa natumiaga daraja la Nyerere, ila leo nikasema nijaribu kuvuka kwa kutumia kivuko, najuta, ninachokiona hapa ni maajabu kabisa, sikutegemea, yaan 2hrs hata geti la kivuko sijalifikia, sasa watu huwa wanang'ang'aniaga nini kwa hali hii?

Tofauti ya ferry na darajan ni kwamba darajan abiria wa kwenye gari hawalipi ila ferry gari na abiria wote wanalipa..

Mfano kama una saloon car umepakia abiri wawili, means utalipia gari 1500 na abiria watalipa 200 kila mmoja kama uta opt kupitia ferry. Ila ukipita darajan utalipa 1500 tu kwa saloon car bila kujari umepakia abiria wangapi.. Sasa swali why watu wana opt kupita ferry wakat kuna daraja??

Darajan kwasasa hakufai labda mvua zikwishe.. Kuna mahandaki ya hatari.. Na pia barabara inatope la kuteleza so usipokua vizuri na kua na tairi kipara unaweza kwama au ukapata ajari kwa gari kuteleza.

Kwenye panton changamoto ni kwamba kuna vivuko vitatu (mv magogoni, kigambon, na kazi) wakati zinafanya kazi zote folen huwa hakuna, ila kwasasa kuna changamoto ya panton moja kua bovu (mv kigamboni) hvo kutokana na kuongezeka kwa volume ya magari ambayo yanakwepa kupita darajani kutokana na ubov wa barabara, panton 2 zilizopo zina shindwa handle supply ya magari...

Mimi natumia daraja asubuhi kati ya saa mbili na saa mbili na nusu na huwa natumia muda wa dakika zisizozidi 20 nakuwa nishafika Posta. Jioni natumia njia hio hio kati ya saa kumi na mbili na nusu na saa moja jioni natumia dakika zisizozidi 20 kuvuka darajani.

Ni kweli ile njia baada ya daraja ukitokea mjini au kabla ya daraja ukienda mjini ni mbaya na changamoto lakini huwezi kulinganisha na kero ya kusubiri pantoni. Nikisema nitumie pantoni nafika Kivukoni saa mbili kamili inachukua zaidi ya nusu saa hadi kuingia kwenye pantoni. Baada ya kuingia kuvuka ni kama dakika 5-10 baada ya hapo unatumia tena dakika kama 20 hivi kushuka kwenye pantoni na kuanza kuhangaika na kichochoro cha kutoka Kivukoni hadi uifikie Sokoine Drive.

Ukiamua kutumia daraja ndani ya nusu saa uko Posta ila ukitumia Pantoni ni saa nzima. Kwa Pantoni umbali ninaotumia hadi kufika mjini ni km 10, nikitumia Daraja umbali unakuwa km 14. Kumbuka wakati unahangaika nusu saa nzima kuingina kwenye pantoni gari inakuwa inaunguruma unakula AC kwahio unaweza kuona umbali ni mfupi ila unatumia mafuta mengi kuliko anaezunguka darajani.

Ukitaka kutumia pantoni kwa raha ukiwa unatoka mjini vuka na pantoni kabla ya saa kumi jioni ila ikivuka saa kumi utakaa si chini ya saa nzima hadi kuvuka. Muda mwingi unapotea kwenye kupanda na kushuka, kuvuka majini ni chini ya dakika kumi.
 
Gharama za kutumia kivuko na za kutumia daraja zikoje ukilinganisha?
 
Zote ni 1,500/= kwa salon car
Duh, nilifikiri labda wanakimbia gharama kubwa upande mmoja, lakini inaonekana siyo kwa mujibu wa jibu lako.

Hiyo 1,500 kwenda na kurudi? auunalipa 1,500 kila marakwenda na kurudi 3,000 ?
 
Duh, nilifikiri labda wanakimbia gharama kubwa upande mmoja, lakini inaonekana siyo kwa mujibu wa jibu lako.

Hiyo 1500 kwenda na kurudi? auunalipa 1500 kila marakwenda na kurudi 3000 ?
Yaan nashangaa, kwa usiku inaonekana hali huwa inakuwa mbaya sana hapa, labda kwa mchana, lakini usiku hapafai.., au hawajui kwamba kuna daraja au ni nini? Hadi dakika hii gari hazijasogea hata nukta
 
Kwan ilo daraja lina kama kilometer ngapi tuanze ? Alaf na congestion kwenye daraje ikoje ?
 
Duh, nilifikiri labda wanakimbia gharama kubwa upande mmoja, lakini inaonekana siyo kwa mujibu wa jibu lako.

Hiyo 1,500 kwenda na kurudi? auunalipa 1,500 kila marakwenda na kurudi 3,000 ?
1.5k for each cross kote darajani na kivukoni, 2 way inakuwa 3k. Ndio tume-board, feels pretty danngerous and crowded.
20180409_190623.jpg
 
Kwa mtazamo wangu kuna sababu kuu mbili.
Kwanza kabisa, watu wengi tunapenda vitu rahisi au niseme vosivyosumbua kichwa. Wakati hili daraja linazinduliwa, yaliletwa maelezo mengi ya kutia watu hofu kwamba usipokuwa makini unaweza kujichanganya ukatokea usikotarajia, wengi wabaona kwanini wakadhalilike? Wanaamua kuogopa hatakujaribu kuona kama yasemwayo ni kweli. Wanaamua kubaki walipozoea hata kama kuna foleni lakini njia ni rahisi.

Pili, miundo mbinu haikuwa rafiki. Barabara mbovu hasa wakati wa mvua na ule mzunguko wengi wanaamua kuvumilia adha za foleni za kivuko.

Naamini baada ya muda mambo yatabadilika, ukizingatia wanatengeneza barabara kwa upande wa Kigamboni.
 
Darajani mbali sana kule mzunguko mkubwa tofauti na hapo kivukoni
 
kuna wengine wanakaa mbali na upande wa daraja hata akishavuka so short cut kwake ni daraja bt nashangaa kwani hali bd ni.mbaya ya foleni licha ya kivuko cha tatu kuongezeka ntauliza wadau tujue km vyote vinafanya kazi isije kuwa keep moja kibovu!!!
 
Lile daraja linge kuwa supported na mabadiliko ya matumizi ya barabara.lle barabara ya SOKOINE DRIVE ingetumika kuelekea GEREZANI yaani ukitoka city centre unanyoosha kuelekea KURASINI.

Hivyo kundi kubwa ktkt ya jiji lingefuata huko Ferry ingepumua ,daraja lingetumika Ipasavyo.
 
Back
Top Bottom