Je, Mungu atamsamehe shetani?

Muumba anasamehe isaya 43:25 β€œMimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.”

Ila shetani (waovu) hawana toba na hawakubali kuomba msamaha mara nyingi hupenda kulipa kisasi au kuwa na mahali pa juu (kukosa unyenyekevu).
 
Haitakaa itokee..maana kwenye kitabu cha henoko imeandikwa kabisa...shetani atakua wa kwanza kwenye hukumu....

Lakini malaika walioasi...wale walioshuka na semzaya wamefungwa kwenye giza totoro wakisubiri hukumu...

Malaika akikosa...hasamehewi
Binadamu akikosa akiomba anasamehewa...na hapo ndio chuki kati yetu na malaika hua inaanza

Wanaona tunapendelewa...
 
MUNGU yeye aliye mwanzo na mwisho...mwenye ufahamu wote....mwenye ujuzi wote...na mwenye nguvu zote...alimpa Lucifer miaka mingi ya kutubu lakini akufanya ivo. Lucifer kwa kukataa mwito wa toba aliopewa miaka elfu nying hatimaye alivuka mipaka ya rehema zake na sasa anasubiria hukumu......
 
kitabu cha henoko..πŸ˜†πŸ˜πŸ˜…πŸ€£
 
Limebakia sharti moja. Binadamu wote dunia nzima, leo hii tukimtambua na kumkubali Mungu wa kweli na tukamwombea shetani msahamaha, atasamehewa siku hiyo hiyo.
 
Matendo ya Mungu si ya mwanadamu kwakuwa Mungu ni roho si mwili na mbingu sio yabisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila shaka ni ile hadithi imuhusuyo Mungu mwenye uwezo wote ujuzi wote na upendo wote ambae anaishi mbinguni.

Hadithi hii kwani inamuendelezo hadi tujue hilo?

Navyofahamu mimi Hii hadithi ya Mungu na shetani iliishia hapo hapo tu.
 
Sifa moja wapo ya creator anaouwezo wa kuedit alivyovitengeneza.

Je Mungu huyo mwenye uwezo wote ujuzi wote na upendo wote hakuwa na uwezo wa kuedit mindset ya shetan huyo akakubali kuomba msamaha?

Kwanini aruhusu kosa hilo lije kuathiri vizazi vya viumbe wengine (human)?

Huon kama hakuna logic hapo?

Huyo Mungu wako ni wa haki kweli?
Je ni Mungu wa upendo kweli?
 
Limebakia sharti moja. Binadamu wote dunia nzima, leo hii tukimtambua na kumkubali Mungu wa kweli na tukamwombea shetani msahamaha, atasamehewa siku hiyo hiyo.
Mungu wa kweli ni yupi!?
 
Wakati Mungu anamuumba huyo kiumbe wake hakujua tarehe fulani ataasi?
Kama hakujua basi sio mjuzi wa yote... Na kama alijua kwanini asingemboresha ili asiasi?
Yes na nmeuliza kitu kama hiki, kumbe umeniwahi bro.

Kwanini Mungu huyo mwenye sifa ya uwezo wote na ujuzi wote ashindwe kuedit viumbe wake!?
 
Kitabu Cha henyoko ndo kitabu gan hiko?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…