Je, Mulugo analenga kuleta maendeleo ya Elimu au Kiujizolea Misifa tu?

changanya

Member
Oct 17, 2012
32
4
Nimesikiliza Kipindi cha Dak 45 ITV naibu Waziri one 1964 alikuwa anaongea pumba tupu. Eti watu wampugie sime kama kuna shule ambayo haijasajiliwa, hivi hiyo ndiyo kazi ya Waziri? atapokea simu ngapi? Kwa nini yeye kama naibu waziri asiletemikakati ya wizara hiyo nyeti kuliko hata nyeti zenyewe ya namna ya kuhakikisha kuwa mfumo wa elimu unadhibitiwa kikamilifu? Je, huo ***** aliokuwa anaongea ametumwa na waziri wake au anatumia upole wa waziri wake kujizolea misifa ili aonekane yeye ndiye mtendaji pekee. Kwa maelezo yake ni kuwa Shukuru hana kazi kabisa, lakini mikakati ya kuleta maendeleo ya elimu aliyoisema ni ipi? Wadau nisaidieni naona namie hapo nimetaga yai kama wanafunzi wa shule za kata sikuelewa kabisa lengo kwenye kipindi ilikuwa ni kufikisha ujumbe gani?
 
Back
Top Bottom