Anatosha,kwa hakika anatosha,jana nilitimiza miaka kumi na mke wangu.yeye pekee alinitosha kwa miaka sita ya uchumba,na minne ya ndoa!amenitosha kwa miaka kumi,atanitosha kwa miaka kumi mingine ijayo,na mingine na mingine mpaka itakapoitwa milele
Heri yangu sijasema.
Hakika tusiwe wa wanafiki kwa mazingira aliyotaja huyu ndugu hatoshi. na amini hili hata wanawake wanalijua ndio maana wengine wanajiuza ili kutoisheleza hamu na shauku ya mume eti. Kuwa na mke mmoja ni imani na tena ni Ukiristo maana sidhani kama kuna dini nyingine inasisitiza mke mmoja chini ya jua.
zafanana, teteteteteeeee!1 Anatosha kaka yangu, ukiendekeza hata 10 hawatakutosha. Sulemani alizidi 300 mwisho wa siku akaishia kusema yote ni batili.
kama mke mmoja hatoshi ,hata mume mmoja hatoshi pia!
Mke akibeba mimba na kujifungua unaweza kumsubiri hadi miezi mitatu ndiyo muendelee na tendo la ndoa.Kama umeoa mwanamke ambaye akibeba mimba anakuwa kwenye bed rest (mapumziko) mpaka ajifungue ndio kabisa itabidi uvumilie mpaka ajifungue na amalize miezi angalau miwili, na kama ameshonewa nyuzi kwenye cervix ili kuzuia ujauzito kutoka vivyo hivyo utajihitaji kumpa muda wa kutosha ili kukuza kiumbe vizuri (namaanisha kwa wanawake wale ambao kizazi chao hakina uwezo wa kubeba kiumbe).
Je Hiki ndiyo chanzo cha baadhi ya wanaume kutoka nje ya ndoa?Je kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kama Daudi na seleman ndiyo itakuwa suluhisho?
Kiukweli mimi binafsi nina mke mmoja na nina uwezo kufanya tendo la ndoa hata kila siku hivyo changamoto hii hunikumba. Siku zote hujitahidi kufanya kazi muda mwingi ili kuweza kupotezea tamaa za ngono hivyo hulazimika kuchelewa kazini ili nikifika nyumbani nakula chakula na kulala.
Je wana JF wenzangu mnakabilianaje na changamoto hii? Hata kina dada mnaweza kutupa ujanja wa jinsi ya kukabiliana na changamoto hii.