Waingereza wana msemo, "crocodile tears": machozi ya mamba. Mamba anapokula minofu ya mnyama aliyemwuuwa hulia, hutoa machozi. Machozi haya siyo ya majonzi au huzuni la hasha, ni machozi ya furaha na shangwe ya ushindi. Tukirudi nyuma wakati ule mwl. Nyerere angali hai viongozi wengi walijifanya "walokole" kwa itikadi na maadili ya chama-CCM ( mfano, sitopokea wa kutoa rushwa,rushwa kwangu ni mwiko; sijui, labda mwiko wa kupakulia na kujiandalia chakula). Mara baada ya kifo cha Mwl. Nyerere ndipo hata yule kipenzi cha mwalimu, W. Mkapa akawa dhahiri sawa na Lowassa, sawa na Kikwete. Nyangenyange wote hufanana na huruka kwa mstari mmoja. Na katika familia ya kambale, wote wanashrafa baba, mama, dada,kaka nk. huwezi kuwatofautisha.
Watu hawa ni miongoni mwa Watanganyika waliotoa machozi wakimlilia Hayati Mwl. Nyerere. Kpt. Komba na wasanii wa JWTZ wakawaongoza kumlilia mwalimu. Hao wote, wakatoa salaam zao za rambirambi kila mmoja kwa wakati wake wakisema tutamuenzi Mwalimu, kumbe visogoni waliwalamba watanganyika. Leo hii, watu hao hawataki kabisa kulishika na kulienzi japo jambo moja zuri la Mwl. Nyerere. Utajiri wao unatisha, wote wamewahi kudiriki kumiliki vinu vya kufua umeme. Wawili kati yao wamekwama kiasi,mmoja kaweza. Utajiri wao umepatikanai kwa gharama za uhai na maisha ya watanganyika kuanzia walipokuwa madarakani hadi vizazi kadhaa vijavyo.
Watoto wa watanganyika wanapata utapiamlo, kwashiakoo, kwa kugharamia utajiri wa watu hawa. Shule, hospitali hazina vifaa wala wataalam kwa gharama za utajiri wa watu hawa na wenzao kadhaa ndani ya CCM na serikali yake.
Ndipo tunaposema, tulipomlilia Mwl. Nyerere na hata tunapomkumbuka'machozi' yetu hayakufanana na wala hayatafanana. Mjane wa Mwalim; familia yake;na watanganyika wanyonge tulilia tofauti na watu hao na mafisadi woote!
Watu hawa ni miongoni mwa Watanganyika waliotoa machozi wakimlilia Hayati Mwl. Nyerere. Kpt. Komba na wasanii wa JWTZ wakawaongoza kumlilia mwalimu. Hao wote, wakatoa salaam zao za rambirambi kila mmoja kwa wakati wake wakisema tutamuenzi Mwalimu, kumbe visogoni waliwalamba watanganyika. Leo hii, watu hao hawataki kabisa kulishika na kulienzi japo jambo moja zuri la Mwl. Nyerere. Utajiri wao unatisha, wote wamewahi kudiriki kumiliki vinu vya kufua umeme. Wawili kati yao wamekwama kiasi,mmoja kaweza. Utajiri wao umepatikanai kwa gharama za uhai na maisha ya watanganyika kuanzia walipokuwa madarakani hadi vizazi kadhaa vijavyo.
Watoto wa watanganyika wanapata utapiamlo, kwashiakoo, kwa kugharamia utajiri wa watu hawa. Shule, hospitali hazina vifaa wala wataalam kwa gharama za utajiri wa watu hawa na wenzao kadhaa ndani ya CCM na serikali yake.
Ndipo tunaposema, tulipomlilia Mwl. Nyerere na hata tunapomkumbuka'machozi' yetu hayakufanana na wala hayatafanana. Mjane wa Mwalim; familia yake;na watanganyika wanyonge tulilia tofauti na watu hao na mafisadi woote!