Kuna familia mbili wake na waume zao walikua marafiki sana kwa bahati mbaya mume wa mke m1 akafariki, yule mke mjane akawa anaendeleza urafiki na kuomba misaada kwa rafiki zake hao na mume wa familia rafiki akawa anamsaidia, mke wa hy mume hakufurahia na alimweleza mumewe kw anawasiwasi kw mumewe anatembea na mjane huyo. JANA MJANE HUYO AKAMWALIKA MUME HUYO KWNY SHEREHE NYUMBANI KWAO LKN HAKUMWALIKA MKEWAKE, MUME AKAENDA NA AKARUDI SA 2 USIKU, MKE AKAMWAMBIA MUMEWE KW HAKUJUA KUWA NI MJINGA KIAS HICHO. mume akaamua kuhama chumba. JE ALIVYOFANYA MUME KWENDA KWENYE SHEREHE BILA MKEWAKE NI SAWA? NA JE MKE KUMUITA MUMEWE MJINGA NI SAWA? NA MUME KUCHUKUA UAMUZI WA KUHAMA CHUMBA NI SAHIHI?
huyu mjane nae bwana kwanini amualike mme bila mkewe ..
Kama sio kutafuta visa vya mama mwenye nyumba ..waambie wasameheane wagange yajayo hilo kosa sio la kufanya mme kuhama chumba ..
Na huyo mke wa jamaa nae kwa nn amuite mmewe mjinga wakati wanalala kitanda kimoja wanaume hawapendagi kudhalilishwa namna hiyo.
waambie wasikosane
pana walakini, kwa nini mke hakualikwa? Hata kama ukaribu ukaribu usipitilize. Labda mume anagonga kweli huyo mjane. Na inawezekana mume ni mjinga kweli(maana ukiachilia hlo hujui mangapi afanyayo )kudhihrisha ujinga wake badala ya kuketi na mkewe wawekane wazi kahama chumba