Je, kuna uwezekano ukakopa mkopo benki wa Tsh 600m kwa kutumia hati za mtu mwingine bila mwenye hati kujua?

Je, kuna uwezekano ukakopa mkopo benki wa Tsh 600m kwa kutumia hati za mtu mwingine bila mwenye hati kujua?

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
19,291
Reaction score
39,975
Nimeona Istagram Mhe. PM akiagiza kukamatwa kwa kijana aliyechukua hati za mama fulani na mumewe ambao wana kampuni yao binafsi kuchukulia mkopo wa Tsh 600m taslimu. PM kasema kuwa huyo mama na mumewe walikubaliana kijana awasaidie kutafuta mkopo na kumkabidhi hati ila kijana akajiombea yeye mkopo na mbaya zaidi harejeshi.

Ninalaani kitendo cha huyo kijana maana ni utapeli huo. Lakini swali la kujiuliza ni kuwa kijana aliwezaje kupewa 600m na benki bila wenye hati kuthibitishwa na benki ikiwemo kusaini makaratasi benki? Pia swali kwamba huyu mama na mumewe hadi wanaweza kuwa na kampuni na mali isiyohamishika yenye uwezo wa kuchukulia 600m kushindwa kushughulikia mkopo wenyewe nadhanni sio la muhimu sana.

TAKUKURU pigeni kambi kwenye hiyo benki huenda kuna uhuni unafanyika.


View: https://www.instagram.com/reel/DS2oi4ECGea/?igsh=NjNrZHRtc3ZscXJ5
 
Huo ni utapeli
Labda alikula Dili na watu wa bank, maana benki haiwezi kukosa umakini kiasi hicho na kuidhinisha mkopo huo kizembe hivyo
 
Ukiwa na hati ya mtu hicho kitu kinawezekana, ila ni kwa kufanya collusion na watu wa ardhi.

Watakufanyia transfer halafu ukienda benk wana create charge wakijua wewe ndo mmiliki.

Ila muhimu hapa: ni lazima watu wa ardhi wahusike.
 
Huo ni utapeli
Labda alikula Dili na watu wa bank, maana benki haiwezi kukosa umakini kiasi hicho na kuidhinisha mkopo huo kizembe hivyo
Hapo sio benki mkuu, hapo ni watu wa ardhi wanahusika pakubwa, japo kwa mimi banker mstaafu, hizo fraud scenarios nilikuwa naziumbua mara kibao, ila kwa bankers wazembe ni ngumu sana kugundua huo mchezo.
 
Kwa namna ambavyo umeandika ni kwamba jamaa aliwashirikisha kila hatua ya kuomba mkopo ila baada ya mchongo kukamilika ndo jamaa akaingia mitini
 
Back
Top Bottom