Je Kuna Umuhimu Wowote wa ................??

Hebu tuangalie historia inatuambia nini juu ya mtoto wa kike na wakiume. Hebu tutumie Biblia kama reference yetu ktk hili.

Utaona tangia enzi za Adamu na Eva, hadi walivyoondelea mpaka kina Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Tukija mpaka hata kipindi cha Agano jipya, utaona mtoto wa kiume alikuwa anapewa nafasi kubwa katika jamii. Tena walikuwa wanatumia lugha hii watoto wakiume waliitwa WANA na wa kike BINTI. Kwa hiyo utasikia ana wana wawili na binti mmoja.

Akizaliwa mtoto wa kike bila kuwepo wa kiume na ikatokea hata baba akafariki, lazima ifanyike njia azaliwe mwana (kiume) wakumuinulia huyo mwanaume aliyefariki jina.

Mtoto wa kiume ndio mrithi, ndio mwenye kuendeleza ukoo, ndo wa kuhifadhi jina la nyumba husika!!
Na hata Mungu alianza kumuumba Adamu ndo akamuumba Eva!!

Nafikiri dunia iliumbwa hivo,iliumbiwa kumtazama mwanamke kama kiumbe dhaifu na kinachotegemea sana uwepo wa mwanaume!! Na mimi binafsi naona pamoja na yote mwanamke hawezi kuwa sawa na mwanaume hata siku moja!!

Haina maana tusisome au tusifanye kazi hapana, na jamii inatakiwa imsaidie mtoto wa kike ajikomboe kutokana na ujinga, na aweze kusimama kwa miguu yake pale inapobidi. Mwanamke tangia mwanzo ameumbiwa roho ya huruma na upendo na ndio maana sio rahisi mtoto wa kike kuwatupa wazazi wake hata kama hawakumtendea mazuri.

Kwa hiyo sasa watoto wote wana nafasi yao katika familia. Nafasi ya mtoto wa kiume ipo na ya wa kike ipo.Ingawa pia inategemea huyu mtoto atakuwa vipi na tatokea mtu wa aina gani katika ukubwa wake!!!!!

Injili imetulia, Ni mpango wa Mungu, naamini kama Mungu yupo basi hizi vurugu za usawa zitaishia kama ile ishu ya mnara wa Babeli. Lakini kwa vyovyote vile Mungu hakuumba Mwanamme amtese mke wake/wanawake wateswe na wanaume , bali kila mmoja asimame katika nafsi yake na wala kusiwe na ubaguzi.
 
Injili imetulia, Ni mpango wa Mungu, naamini kama Mungu yupo basi hizi vurugu za usawa zitaishia kama ile ishu ya mnara wa Babeli. Lakini kwa vyovyote vile Mungu hakuumba Mwanamme amtese mke wake/wanawake wateswe na wanaume , bali kila mmoja asimame katika nafsi yake na wala kusiwe na ubaguzi.

Ni kweli kabisa kaka, wanadamu ndio tulioVuruga hii dunia, tangia mwamzo mtoto wa kike pamoja na kwamba hakuwa anatajwa ktk mambo mbalimbali muhimu lakini alikuwa anathaminiwa, anatunzwa vizuri na anaheshimiwa sana.

Lakini dunia ya leo wanaume wametumia uanaume wao kumkandamiza mtoto wa kike/mwanamke kiasi kwamba inatubidi kupigania haki zetu. Lakini kiukweli ni kwamba Mtoto wa kiume anayo nafasi kubwa kwenye jamii na Familia, na mtoto wa kike naye anayo nafasi yake kubwa pia.
 
Mtoto ni mtoto tu.

Ila likija swala la kuangalia wazazi pindi wote wanapokuwa katika ndoa mtoto wa kike anakuwa na nafasi kubwa kuliko wa kiume.

Mimi mwenyewe ni wa kwanza kuzaliwa, wa pili naye mshichana watatu ndo mwanaume na wanne.

Ukilinganisha hapo utashangaa hawa wakiume wote wanafayakazi na wanafamilia zao kama sisi kila ukiwaambia kuna shida hii na hii home sababu kibao ooohhh watoto shule, ujenzi unasumbua, mara gari yangu imepata ajali iko garage pesa yote imeishia huko mra mke wangu kaenda kusalimu wazazi nyumbani nauli imecost sana ili mradi tu visingizio haviishi.

Ila sisi wa kwanza na wa pili tukitaarifiwa kuna matatizo hapo hapo safari inafungwa na kwenda kutatua matatizo.

So watoto wa kike wanaumuhimu sana katika jamii yetu isipokuwa tu pale watu wanapokuwa hawaelewi na kuwa na dhana mbovu kuwa utaletewa mjukuu sasa hivi hapo ndo huwa nachoka kabisa.

Siku njema mwanajamii
 
Wazazi ni watu wa ajabu sana kwa kweli hawatabiriki kabisa, mkiwa watoto kunakua na kaubaguzi fulani hivi ila amini mkishakua wakubwa na mmeanza kujitegemea yule mwenye pesa ndio anapendwa zaidi ukiishiwa unaanza kudharauliwa anaheshimiwa mwenye pesa tena yaani kazi kweli kweli.
 
Tumeona watoto wengi wakike wanachakachuliawa na misela mtu kavaa buti kubwa kupita mguu halafu ni kinyozi wakati demu kwao zipo za ku mwaga na elimu anapewa - matokeo yake mimba tena ya masela hapo ndo huwa na kwazika sana, yaani fimbo inamchanganya kiasi kwamba hasikii la mzazi
 
Haya mapenzi ya uzao wa kwanza wa mtoto wa kiume hayapo kwa wanaume pekee yao....naamini wanawake wengi wanatamani wapate uzao wa kwanza wa mtoto wa kiume kuliko hata wanaume....

Kwa wanaume (labda) wanatamani wapate mrithi wa jina+miji+tamaduni zao....wapate atakayeendeleza ukoo wao (majina ya wanawake na koo za wazazi wa wanawake hayarithishwi kwa uzao wao)....nadhani hii kwamba uzao ni kwa nia ya matunzo ya baadae sio sahihi sana (au labda ni sio sababu ya kwanza)....
 
......Hii tabia ya kuona mtoto wa kiume ni bora kuliko wa kike mie inanikera sana, tena utakuta watu ni wasomi lakini bado tu wana wanachambua jinsia ya mtoto.
Mie mwenyewe nilijionea nilipopata mtoto wangu, rafiki za mume wangu walipokuja kumuona mtoto kila mtu anamwambia mume wangu eti ana bahati kwa kuwa kapata mtoto wa kiume....... cha ajabu hata kuna wamama nao wanasema hivyo hivyo....aiseeeee walikuwa wananiudhi kweli kweli halafu ni watu walioelimika haswa.
Watu hawajui kwamba siku hizi mtoto ni mtoto ilimradi awe mzima wa afya, mpe elimu bora ili aje kuwa na future nzuri maishani mwake.
 
Mi wacwac wangu kwa mtoto wakike coz ndo wanachakachuliwa mapema.
Kuchachuliwa inategemea na malezi kama hujamfundisho dos and donts atachakachuliwa mapema tu!
mie nina mabinti wawili nina faraja maana ni mabest zangu , wadogo zangu na kila kitu am happy wala cjuti kukosa wa kiume
 
wajameni, Nina tangazo.

Ninatafuta mtoto wa KIKE, na natafuta wa 'kutafuta' naye. Matunzo yote juu yangu, aliye tayari ani PM tafadhali.

Aksante MJ1 kwa hoja nzuri kabisa. (karibu tunakusubiri huku)
 
Dah! Hivi kuna mtu bado anazo hisia za kupendelea mtoto wa kiume zaidi kuliko wa kike?

Siamini kabisa!!!
 
Sasa mwanajami1 siumesha jua nini sababu ya familia kuhitaji mtoto wa kiume. anaongeza hapunguzi na kuhusu swala la kuwa karibu na wazazi hiyo ni maumbile mungu kawapa imani. ninyi mioyo yenu ina huruma. na pia mwanaume anamajukum yakulea familia yake na wazee. wewe umesema una mtoto una mzazi mwenzio ankusaidia kulea hebu jaribu kushekecha hapo utapata jibu zuri. au ndo tayari ile haki inayozungumzwa kilakukicha inawapa mwanya wakuamini kuwa kweli nanyi hamna tofauti na wanaume? kuna maswala ambayo ni necha huwezi kubadili kama ulaya na magharibi wanvyo idanganya dunia huko kwao yamewashinda, nafasi ya kumuendeleza mtoto wakike ni hakiyake aendelezwe kielim bila kubaguliwa na hakizote apewe lakini zina mipaka yake naimani mwanajami1 unajua Africa na Asia ni tofauti maana yangu kusemna kuna mipaka yake kwakuwa sisi tuna tamaduni zatu. huwezi wewe binafsi yako ukawa kama mwanaume mbele ya wazee wako kuna utofauti hapo japo unawalea lakini kuna sehem fulani mwenyewe huwezi kuikeuka mfano huwezi kuwa nje ya nyumbani kwa muda mwingi kila siku. huu ni mfano mmoja lakini mwanaume ni kawaida akisha fikia umri flani nazani naeleweka. ispokuwa kuna familia zinafanya makosa kutowashirikisha wanawake kenye mfumo wa kiuchumi haya ni makosa.
LAKINI NIMAONO YANGU
Wapenzi wa JF, kwa heshima na taadhima ninawasalimu wote.

Nimejikuta ninawaza jinsi mimi kama mtoto wa kike ndani ya familia yetu ambaye nina majukumu ya not only to take care of my own family i.e. mwanangu kipenzi pamoja na familia ya wazazi wangu i.e. wazee na wadogo zangu- by the way mimi ni mzaliwa wa kwanza kwetu).

Nimejikuta nikitingwa na mawazo ya umuhimu wa sisi wazazi wa leo (wote wake kwa waume) kung'ang'ania kutafuta au kupata mtoto wa kiume kwanza (Ingawa hali hii inaanza kidogo kubadilika now days but to many families it is an issue).

Nahisi inakuwa na logic sana iwapo wazazi mna jiwweza na mnabiashara ambazo mna uhakika kuwa mtoto wa kiume tu ndiye atakayeweza kuziendeleza i.e. kwa kuwa yeye huwa haondoki kwenye familia- akioa anaongeza familia na si kupunguza kama mtoto wa kike.

Lakini najiuliza iwapo mzazi/wazazi hawana asset yoyote ambayo wanahisi wanawezakumrithisha mtoto wa kiume kwa manufaa ya familia hapo baadae. Experience imeonyesha kuwa watoto wa kiume huwa wana attachment ndogo sana kwa wazazi wao (especially pale wanapoanza kujijengea familia zao) kuliko watoto wa kike. Watoto wa kike wanatend kujali wazazi zaidi ya wale wa kiume...........

Je kuna umuhimu bado wa kukazania mtoto wa kiume? Yaani je bado kina mama tunastahesabiwa wanawake wa shoka kama tunauzao mkubwa wa watoto wa kiume zaidi ya wa kike?? Je nafasi ya mtoto wa Kike hasa katika kumwendeleza kielimu inastahili kupuuzwa?

Ninajiuliza sipati jibu, ninakuomba msaada ewe kaka, dada, baba na mama, mjomba, shangazi, Babu na bibi yangu......
Aksanteni, karibu tuchangie........
 
Sasa mwanajami1 siumesha jua nini sababu ya familia kuhitaji mtoto wa kiume. anaongeza hapunguzi na kuhusu swala la kuwa karibu na wazazi hiyo ni maumbile mungu kawapa imani. ninyi mioyo yenu ina huruma. na pia mwanaume anamajukum yakulea familia yake na wazee. wewe umesema una mtoto una mzazi mwenzio ankusaidia kulea hebu jaribu kushekecha hapo utapata jibu zuri. au ndo tayari ile haki inayozungumzwa kilakukicha inawapa mwanya wakuamini kuwa kweli nanyi hamna tofauti na wanaume? kuna maswala ambayo ni necha huwezi kubadili kama ulaya na magharibi wanvyo idanganya dunia huko kwao yamewashinda, nafasi ya kumuendeleza mtoto wakike ni hakiyake aendelezwe kielim bila kubaguliwa na hakizote apewe lakini zina mipaka yake naimani mwanajami1 unajua Africa na Asia ni tofauti maana yangu kusemna kuna mipaka yake kwakuwa sisi tuna tamaduni zatu. huwezi wewe binafsi yako ukawa kama mwanaume mbele ya wazee wako kuna utofauti hapo japo unawalea lakini kuna sehem fulani mwenyewe huwezi kuikeuka mfano huwezi kuwa nje ya nyumbani kwa muda mwingi kila siku. huu ni mfano mmoja lakini mwanaume ni kawaida akisha fikia umri flani nazani naeleweka. ispokuwa kuna familia zinafanya makosa kutowashirikisha wanawake kenye mfumo wa kiuchumi haya ni makosa.
LAKINI NIMAONO YANGU

Mkuu umejitahidi sana kuelezea kama nionavyo mimi.
Ubaguzi wa kielimu kwa kweli haufai, watoto wote wapate elimu sawa bila upendeleo.
Na hata ktk maamuzi wawe ktk ushirikiano pia, lakin kuna mambo mengine mwanamke hawezi kuchukua nafasi ya mwanaume au mwanaume kuchukua nafasi ya mwanamke, na si kwa lengo la kibaguzi.
Mwanaume bado anasimama kama mlinzi mkuu kokote duniani ktk masuala yanayohitaji maamuzi magumu au hata kutumia nguvu, mfano ktk kulinda familia na mali zake.
 
Kwa mawazo yangu, Nadhani tunakuwa na watoto ili tuwapende, sidhani kama tunakuwa na watoto ili watusaidie hapo baadae. Fanya kazi kwa bidii na jiwekee akiba ya kukutunza hapo uzeeni, usizae watoto ili utegemee baadae waje kukutunza. Wape maisha bora ili nao baadae waweze kujitegemea. Ukifikiria hivyo sidhani kama utawaza kuwa huyu mtoto ni bora kuliko huyu kwani wote wametokana kwa mapenzi.
 
Tumeona watoto wengi wakike wanachakachuliawa na misela mtu kavaa buti kubwa kupita mguu halafu ni kinyozi wakati demu kwao zipo za ku mwaga na elimu anapewa - matokeo yake mimba tena ya masela hapo ndo huwa na kwazika sana, yaani fimbo inamchanganya kiasi kwamba hasikii la mzazi

Ni kweli kimbweka but kwa maisha ya sasa hivi yenye mambo mengi kama uvutaji banghi, madawa ya kulevya na hata tabia za kishoga..sidhani kama huyo mtoto wa kiume ana salama kwa kweli.
 
Haya mapenzi ya uzao wa kwanza wa mtoto wa kiume hayapo kwa wanaume pekee yao....naamini wanawake wengi wanatamani wapate uzao wa kwanza wa mtoto wa kiume kuliko hata wanaume....

Kwa wanaume (labda) wanatamani wapate mrithi wa jina+miji+tamaduni zao....wapate atakayeendeleza ukoo wao (majina ya wanawake na koo za wazazi wa wanawake hayarithishwi kwa uzao wao)....nadhani hii kwamba uzao ni kwa nia ya matunzo ya baadae sio sahihi sana (au labda ni sio sababu ya kwanza)....

Ni kweli St kuwa mapenzi ya mtoto wa kiume hayako kwa baba peke yake hata kwa mama, but nadhani ni kutokana na kuathiriwa na mtazamo mzima wa jamii, Wamama wengi wanaamini kuwa wakipata mtoto wa kiume ndio wanakuwa na security zaidi kwa sababu tu mumewe anapenda na angependa mtoto wa kiume na mara nyingi mama anapokuwa na ujauzito na mumewe akawa anamwambia anatamani mtoto wa kike basi mama ni mwepesi kujisikia sawa kuliko baba awe anataka mtoto wa kiume kisha mama aprefae wa kike siku akijifungua na kukuta ni wa kike pamoja na kuwa ndo aliyekuwa anamtaka basi atasononeka kwa kuwa mumewe alitamani wa kiume.

BAdo najiuliza kama sababu hasa ya kupenda watoto wa kiume ilikuwa ni nini? Aje awatunze baadae?? au aje arithi mali za familia?? na what if wazazi hawana mali za kumrithisha je ilikuwa ni sifa tu mtaani kuwa una mtoto wa kiume au??
 
Mtoto wa KIKE hawezi kuendeleza "family tree"!

Okay......the family tree if it is string like it used to be nitakuelewa lakini sikuhizi na hizi nyuklia famili zetu ampapo saa nyingine watoto wa mashangazi hawajuani .........................
 
Back
Top Bottom