Ni kizomanizo ndo kamwaga hyo lecture,mshana mweupe2 anamwaga matangopori hapa hahaha
Haya nimerudi hapa sasa. Nitaeleza kidogo juu ya Iluminati (tena) na hiyo sentensi ya kirumi.
Illuminati
Tofauti na maoni ya watu wengi ambayo yamekuwa yakiyokana na maneno ya kuzungumzwa mitaani yaani porojo, Illuminati sio kundi la watu wa uchawi uchawi. Moja ya dhumuni kuu la kuanzishwa kwa jamii ya illuminati ilikua ni kupinga imani za kishirikina na imani za kidini kuingizwa katika maisha ya raia ya kila siku.
Huko Bavaria Ujerumani mnamo miaka ya kati ya 1700 hivi ndio kuna watu wasomi na wanasayansi waliamua kuanzisha jamii ya watu walioona mwangaza(ndio maana ya illuminati) ya huko Bavaria. Kwa kuwa miaka ile ya utawala wa kikabaila(feudalism) maaskofu, kanisa na maduki walikuwa na nguvu sana, walitaka sera zao ndio ziwe kama muongozo au katiba ya jamii. Maaskofu walitoa hukumu za kunyongwa wanaowapinga, maduki waliohodhi ardhi waliwaita watu wazanfiki na wachawi(villains). Hii yote ilionekana kwenda kinyume na maendeleo ya kiuchumi wakati huo. Ikumbukwe kuwa miaka hiyo ndio nchi kama Marekani zilikua zinapata uhuru wake na biashara ya mbali kupitia bahari ikaanza kushamiri. Hawa watu waliokuwa na mwangaza wa elimu wakaanzisha jamii yao ila ikawapasa kufanya mambo kwa siri maana utawala ungewahukumu kifo kutokana na kuhubiri sera tofauti na dini, uchawi na ufalme.
Baada ya miaka kumi hivi, kikundi hiki kiliweza kuchota wasomi wengi kama kina Wolfgan van Goethe na wana diplomasia kadha wa kadha kama kina Brunswick ambao walikuwa na ushawishi kwa jamii. Hatua ya serikali ya Bavaria wakati huo kupiga marufuku vikundi vyote vya siri siri ndio imeleta minong'ono mingi sana kuhusu illuminati mpaka leo hii. Taarifa rasmi zinasema kwamba baada ya marufuku hiyo, illuminati ilikosa nguvu na hatimaye kufa kabisa ndani ya hiyo miaka kumi. Vipi vikundi kadha wa kadha ndani ya nchi kama Ufaransa na Bavaria kwenyewe waliibuka baada ya miongo kadhaa na kusema illuminati haikufa na wao ndio wanaoiendeleza. Miaka ya hivi majuzi kutokana na ukuaji wa usambazaji habari na watu kuwa na uwezo wa kuchapa habari zao wenyewe, wimbi jipya la kutangaza watu ni wa illuminati likaibuka tena mara tukasikia rais Bush mdogo ni illuminati, mara mwanamuziki Jay Z naye ni mmojawao. Kwa nijuavyo mimi, kama dhana ya uilluminati bado ni ile ile ya kutoa mwangaza (illumination), wako watu wazuri zaidi na wasomi wangekiwa humo na sio Jay Z, Kanumba na Diamond.
Mwanzo nilimshambulia Mshana kwa kuwachanganya Illuminati na Wamasoni, ni kweli kuwa wao sio wamoja kimalengo na kivikundi. Wamasoni wao wapo kaa mambo ya kiinani zaidi wakati waluminati wao wapo kwa mambo ya kidunia zaidi. Tutaelezana kuhusu wamasoni huko mbeleni.
Halafu kwa mtoa hoja, nembo ya illuminati sio jicho linalotazama bali ni bundi aloketi juu ya kitabu kilichofunguliwa. Sasa sijui nembo ya BBA na bundi na kitabu vina uhusiano gani. Utakuwa umechukua porojo za hapa ukachanganya na za pale basi ba wewe ukawa na cha kuandika humu jamvini.
VICARIVS FILII DEI
Hiyo kauli hapo juu ilikuwepo tangu karne ya 3 hivi yaani kama miaka 278 baada ya Yesu. Ni jina ambalo alipewa askofu wa Roma ambaye ndiye Papa kwa wengi wetu. Biblia za kikatoliki(lazima kueleweka hapa) zinaonesha kwamba Yesu kwa maneno yake aliwaambia mitume kwamba huyu ndiye Kefa (Petro) na juu ya mwamba huo atalijenga kanisa lake. Na pia alitumia lugha ya kumkabidhi funguo za rehema ili kila atalolifunga duniani, na mbinguni pia litafungwa. Mistari hiyo inafanya kanisa katoliki kuamini kuwa Petro mtumw ndie alikuwa papa wa kwanza kabisa. Kwa wasomaji wa mara kwa mara wa biblia watafahamu kwamba baada ya Yesu kuondoka, kuna wakati ulitokea mkwaruzano mkubwa kati ya Paulo na Petro juu ya kuwapokea watu toka mataifa mablimbali(wasio wayahudi). Baada ya mkwaruzano huo Petro aliamua kuhubiri kwa wayahudi wakati Paulo alienda kwa watu wa nje (gentiles). Baada ya kufa kwa Petro(au hata kabla, sina ushahidi) aliteuliwa mtu chini ya uangalizi wa Paulo ili ashike nafasi ya Petro na mtu huyo angekaa Roma(ambapo ndio ilikua kama New York ya dunia enzi hizo) na aendeleze huduma kwa watu wa dunia nzima. Huyu mtu alikuwa akiitwa Linus na vile vile kanisa katoliki linamtaja kuwa ndiye Papa wa pili baada ya Petro.
Hayo maneno yooote juu ya kina petro nimeyasema ili kumjenga msomaji ajue matumizi ya hiyo sentensi ya kirumi. Baada ha kupita mapapa kadhaa, wakaanza kuwaita kwa cheo yaani mrithi wa kazi ya mwana wa mungu. Kama alivyoachiwa Kefa na Yesu, naye kumuachia Linus na kadhalika na kadhalika. Vicarivs Filii Dei kwa tafsiri ya kiingereza ni 'vicar of the son of God' na kwa kiswahili ni kama tu kusema mrithi wa mwana wa Mungu. Sasa baada ya karne kadhaa, kuna wachambuzi wakaanza kuchambua jina la kile cheo kwa namba za kirumi. Ikumbukwe kwamba warumi hawakuwa na tofauti kati ya alfabeti U na V wakati huo, kwa hiyo hilo jina miaka ya 1000 hivi lilianza kuandikwa kwa herufi kama za leo yaani 'VICARIUS FILII DEI'. Sasa ukichukua kila herufi ndani ya hilo neno na kuipa thamani yake kama na mba ya kirumi na kuipa thamani ya 0 herufi isiyo na namba ya kirumi, jumla unapata 666.
V = 5
I = 1
C = 100
A
R
I = 1
V = 5
S
F
I = 1
L = 50
I = 1
I = 1
D = 500
E
I = 1
Hapo ukifanya hisabu utaona kuna 5+1+100+1+5+1+50+1+1+500+1=666
Miaka hiyo ya kati ikawa ni fursa ya watu kusema wameshamjua mpinga Kristo kwamba ni Papa maana namba yake kama ilivyofunuliwa kwenye vitabu vya Ufunuo na Danieli, namba yake ni 666. Hii ilikaa kwa muda sana mpaka watu wakaichoka japo bado kashfa hii inasemwa semwa na baadhi ya watu. Naona sasa watu kama kina Mshana wamekuja na mpya za kusema Password na ATM na mambo ya dijitali ndio 666 mpya. Tusubiri miaka mingine 1000 ndio watabadilika.
Source: ku Google hapa na pale na kusoma baadhi ya vitabu na makala. Hasa hasa Roberts, J.M. (1974). The Mythology of Secret Societies.