Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,483
- 30,155
Kwenye taaluma ya sheria kuna kitu kinaitwa "circumstantial evidence" au kwa kiswahili tunaita ushahidi wa mazingira, ambao unaweza kumtia hatiani mtuhumiwa
Hivi inawezakanaje Bwana yule kutamka hadharani kuwa Mbunge Tundu Lissu amelitelekeza jimbo la Singida Mashariki na hivi sasa ndiyo limepata Mbunge safi, ambaye ni Miraji Mtaturu wa CCM??
Anaendelea kueleza kuwa jimbo hilo hivi sasa ndiyo litapata maendeleo ya haraka haraka baada ya "kuporwa" Tundu Lissu wa upinzani na hivi sasa kukabidhiwa Miraji Mtaturu wa CCM!
Hivi tangu lini maendeleo ya majimboni nchini kwetu yameanza kupangiwa bajeti na Ikulu badala ya Bunge??
Hivi ni nani katika dunia hii ambaye hajui kilichomsibu Mbunge Tundu Lissu, takribani miaka miwili iliyopita, baada ya kumiminiwa risasi zaidi ya 30 kwenye gari lake na risasi 16 kumwingia mwilini mwake, katika jaribio la kumwua, ambapo alinusurika kimuujiza na hadi hivi Leo anaendelea na matibabu huko ubelgiji??
Katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi halijafanya juhudi zozote za kuwatafuta wale waliotekeleza mpango huo wa kidhalimu, hivi anapotokea mtu na kusema kuwa Tundu Lissu amelitelekeza jimbo hilo, hivi tunaweza kumuelewa vipi mtu huyo??
Katika hali ya kawaida kwa binadamu yoyote alipaswa "a-sympathize" na hali aliyonayo Tundu Lissu hivi sasa, kwa hiyo ni ajabu kusikia Bwana yule akitamka hadharani kuwa Tundu Lissu eti amelitelekeza jimbo lake la Singida Mashariki na hivyo kumlazimu Spika Ndugai afanye utaratibu wa kuweza kumpata Mbunge mwingine!
Ni kutokana na muujiza wa Mungu pekee ambao umeendelea kumpa uhai Tundu Lissu hadi hivi Leo na naendelea kuamini kuwa lipo kusudi maalum la Mungu la kuendelea kumpa uhai Tundu Lissu hadi hivi leo na hivyo hadi hilo kusudi litimie na hivyo tumwombe Mungu wetu azidi kutujaalia uhai ili tuweze kushuhudia hicho kitu "so special" ambacho Mungu mwenyewe amekipanga kwa mja wake huyu
Mungu ibariki Tanzania
Hivi inawezakanaje Bwana yule kutamka hadharani kuwa Mbunge Tundu Lissu amelitelekeza jimbo la Singida Mashariki na hivi sasa ndiyo limepata Mbunge safi, ambaye ni Miraji Mtaturu wa CCM??
Anaendelea kueleza kuwa jimbo hilo hivi sasa ndiyo litapata maendeleo ya haraka haraka baada ya "kuporwa" Tundu Lissu wa upinzani na hivi sasa kukabidhiwa Miraji Mtaturu wa CCM!
Hivi tangu lini maendeleo ya majimboni nchini kwetu yameanza kupangiwa bajeti na Ikulu badala ya Bunge??
Hivi ni nani katika dunia hii ambaye hajui kilichomsibu Mbunge Tundu Lissu, takribani miaka miwili iliyopita, baada ya kumiminiwa risasi zaidi ya 30 kwenye gari lake na risasi 16 kumwingia mwilini mwake, katika jaribio la kumwua, ambapo alinusurika kimuujiza na hadi hivi Leo anaendelea na matibabu huko ubelgiji??
Katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi halijafanya juhudi zozote za kuwatafuta wale waliotekeleza mpango huo wa kidhalimu, hivi anapotokea mtu na kusema kuwa Tundu Lissu amelitelekeza jimbo hilo, hivi tunaweza kumuelewa vipi mtu huyo??
Katika hali ya kawaida kwa binadamu yoyote alipaswa "a-sympathize" na hali aliyonayo Tundu Lissu hivi sasa, kwa hiyo ni ajabu kusikia Bwana yule akitamka hadharani kuwa Tundu Lissu eti amelitelekeza jimbo lake la Singida Mashariki na hivyo kumlazimu Spika Ndugai afanye utaratibu wa kuweza kumpata Mbunge mwingine!
Ni kutokana na muujiza wa Mungu pekee ambao umeendelea kumpa uhai Tundu Lissu hadi hivi Leo na naendelea kuamini kuwa lipo kusudi maalum la Mungu la kuendelea kumpa uhai Tundu Lissu hadi hivi leo na hivyo hadi hilo kusudi litimie na hivyo tumwombe Mungu wetu azidi kutujaalia uhai ili tuweze kushuhudia hicho kitu "so special" ambacho Mungu mwenyewe amekipanga kwa mja wake huyu
Mungu ibariki Tanzania