The Evil Genius
JF-Expert Member
- Mar 21, 2014
- 5,479
- 17,342
Leo Jumapili, siku ya Wakristo ama madhehebu mengi ya Kikiristo kuabudu ama kusali.
Hivyo basi naomba tutafakari jambo moja la imani, je kati ya shetani na binadamu ni nani hasa mwenye dhambi nyingi zaidi?
Maandiko yanasema Mungu ni mtakatifu sana asiye na mawaa, ambae dhambi ama uovu haukai ama hauwezi kukaa karibu yake. Mfano mzuri ni kwa Musa, aliambiwa hawezi kumuona Mungu kwa sababu binadamu ni wadhambi wa kuzaliwa.
Binadamu tunaambiwa sisi ni wadhambi hatuwezi kumkaribia Mungu, tunaambiwa sisi ni wadhambi wa kuzaliwa kwa sababu ya Adam, (wakati huo huo biblia inasema Mungu alitujua kabla ya kuumba misingi ya ulimwengu, maana yake alijua atatuumba wenye dhambi tu hata kabla hajatuumba) there was no way adamu asitende dhambi kwa sababu Mungu alijua kabla ya kumuumba kua atatenda dhambi.
Tukiachana na hayo, kwenye hadithi za Ayubu, shetani ananekana kukutana na Mungu na kupiga soga nyingi hadi kukubaliana kumjaribu Ayubu. Hivyo inaonekana ni kawaida kwa shetani na Mungu kukutana. Hatuambiwi wanakutana wapi.
Hoja yangu ni je, kati ya shetani na binadamu ni nani hasa mwenye dhambi nyingi ambae haruhusiwi kumkaribia Mungu?
Maovu yote Duniani tunaambiwa yameletwa na shetani lakini shetani huyo huyo anaruhusiwa kukutana na Mungu na kupiga soga tena za kiurafiki kabisa. Binadamu ambae ameletewa dhambi yeye haruhusiwi kumkaribia Mungu, je binadamu ni mdhambi kuliko shetani?
Watu wa dini naombeni mawazo yenu.
Hivyo basi naomba tutafakari jambo moja la imani, je kati ya shetani na binadamu ni nani hasa mwenye dhambi nyingi zaidi?
Maandiko yanasema Mungu ni mtakatifu sana asiye na mawaa, ambae dhambi ama uovu haukai ama hauwezi kukaa karibu yake. Mfano mzuri ni kwa Musa, aliambiwa hawezi kumuona Mungu kwa sababu binadamu ni wadhambi wa kuzaliwa.
Binadamu tunaambiwa sisi ni wadhambi hatuwezi kumkaribia Mungu, tunaambiwa sisi ni wadhambi wa kuzaliwa kwa sababu ya Adam, (wakati huo huo biblia inasema Mungu alitujua kabla ya kuumba misingi ya ulimwengu, maana yake alijua atatuumba wenye dhambi tu hata kabla hajatuumba) there was no way adamu asitende dhambi kwa sababu Mungu alijua kabla ya kumuumba kua atatenda dhambi.
Tukiachana na hayo, kwenye hadithi za Ayubu, shetani ananekana kukutana na Mungu na kupiga soga nyingi hadi kukubaliana kumjaribu Ayubu. Hivyo inaonekana ni kawaida kwa shetani na Mungu kukutana. Hatuambiwi wanakutana wapi.
Hoja yangu ni je, kati ya shetani na binadamu ni nani hasa mwenye dhambi nyingi ambae haruhusiwi kumkaribia Mungu?
Maovu yote Duniani tunaambiwa yameletwa na shetani lakini shetani huyo huyo anaruhusiwa kukutana na Mungu na kupiga soga tena za kiurafiki kabisa. Binadamu ambae ameletewa dhambi yeye haruhusiwi kumkaribia Mungu, je binadamu ni mdhambi kuliko shetani?
Watu wa dini naombeni mawazo yenu.