Je Jesca Magufuli ni nani?

Je Jesca Magufuli ni nani?

funaku

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
38,534
Reaction score
31,198

Tumeona vipande vya Mahojiano kati ya mwandishi Millard Ayo na Mtoto wa aliyewahi kuwa kiongozi Mkuu nchini.

Jambo hili ni la kipekee na kihistoria nchini.

Humu jamvini na mtandaoni tuliwahi kumtaja au kumjadili Jesca Magufuli wakati wa uhai wa baba yake.
Yapo tuliyozusha au kuyasema bila ushahidi juu ya binti huyu.

Tumetumia sana a.k.a ya baba Jesca wakati tunamtaja Mhe .Rais hayati John Pombe Magufuli.




ni wakati wa kumjadili kwa haki !!
je Jesca Magufuli ni nani?

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!
 

Tumeona vipande vya Mahojiano kati ya mwandishi Millard Ayo na Mtoto wa aliyewahi kuwa kiongozi Mkuu nchini.
Jambo hili ni la kipekee na kihistoria nchini.
Humu jamvini na mtandaoni tuliwahi kumtaja au kumjadili Jesca Magufuli wakati wa uhai wa baba yake.
Yapo tuliyozusha au kuyasema bila ushahidi juu ya binti huyu.
Tumetumia sana a.k.a ya baba Jesca wakati tunamtaja Mhe .Rais hayati John Pombe Magufuli.

je Jesca Magufuli ni nani?

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!
Kwa nini unasema kwa hisani ya mtu wa Tanzania!!?
 
Kwa nini unasema kwa hisani ya mtu wa Tanzania!!?
Kwa kuwa huwa nachukizwa na lile neno la KWA HISANI YA WATU WA MAREKANI.
unapoona mada yangu nimeweka hili neno jua kabisa ni mada nyeti na ya kizalendo sana inayoigusa Tanzania
 
Kwahiyo tayari huyo Jesca kufanya interview ndio apewe relevance?

Ni wakati muafaka pia kufanya interview na familia za kina Ben Saanane, Azory Gwanda, Leopold Lwajabe na wale mawakala wa vyama vya upinzani waliopata kesi za mchongo siku ya uchaguzi 2020.
 
Watu wa Marekani huwa wanakuwa wametoa hisani fulani hadi kufikia kuweka hiyo kauli, wewe umetoa hisani gani mpaka useme hayo maneno??
naamini kuna baadhi ya mada huwa nazitoa kutokana na uzalendo usio na shaka kwa Taifa langu...nawe fanya hivyo ...tumia hashtag hii unapotoa hoja muhimu kwa mustakabali wa Taifa lako la Tanzania
 
Hii ni mada nyeti na ya kizalendo?
Hii mada inaigusa vipi Tanzania?
Ndio...kwa kuwa yapo ya ndani sana yamezungumzwa kuhusu legend John Pombe Magufuli.
 
ben+saananee.jpg

R.I.P Ben
 
naamini kuna baadhi ya mada huwa nazitoa kutokana na uzalendo usio na shaka kwa Taifa langu...nawe fanya hivyo ...tumia hashtag hii unapotoa hoja muhimu kwa mustakabali wa Taifa lako la Tanzania
Kwa nini unarudia neno uzalendo mara nyingi sana? Watu gani unahisi sio wazalendo kwa taifa lao??
 
Kwahiyo tayari huyo Jesca kufanya interview ndio apewe relevance?

Ni wakati muafaka pia kufanya interview na familia za kina Ben Saanane, Azory Gwanda, Leopold Lwajabe na wale mawakala wa vyama vya upinzani waliopata kesi za mchongo siku ya uchaguzi 2020.
zifanyike tu...ila zifanyike kwa haki na sio uhuni kama wa kitabu kile cha kutakatisha fedha chafu
 
Kwa nini unarudia neno uzalendo mara nyingi sana? Watu gani unahisi sio wazalendo kwa taifa lao??
wapo wengi ambao sio wazalendo ...wapo wengi mamluki na wapo wengi sio raia wa nchi hii wenye nia ovu dhidi ya Mama Tanzania....wote hao lazima tuwape hii slogan KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!
 
zifanyike tu...ila zifanyike kwa haki na sio uhuni kama wa kitabu kile cha kutakatisha fedha chafu
Tunaanza na claims zilizopo kwenye kitabu kama mnazipinga mbona hakuna hatua mmechukua kukanusha?

Halafu unatakatishaje pesa kwa kitabu cha $23?
 
Back
Top Bottom