Je, ingemtokea mpambe wa Rais (ADC) wangefanyaje?!

Je, ingemtokea mpambe wa Rais (ADC) wangefanyaje?!

Chifu mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2025
Posts
846
Reaction score
884
Habari ja jioni wadau.

Kuna jambo nimejiuliza nikakosa majibu nikaona niwashirikishe wadau saa nyingine yupo mwenye uelewa akanisaidia kunielimisha.

Ni kuhusu tukio lililotokea siku za karibuni la mmoja wa walinzi wa mheshimiwa rais kushikwa na kizunguzungu na kulazimika kwenda kupumzika.

Ni kwamba pamoja na rais kuwa na walinzi lakini pia ana mlinzi maalumu (bodyguard) ambaye pia hujulikana kama MPAMBE WA RAIS (ADC) ambaye yeye huwa na sare za kijeshi ( japo mara kadhaa tumeona mh Rais anapokuwa msikitini MPAMBE wake huyu na yeye pia hupiga HIJABU YA KIISLAMU na upendeza sana akiwa ndani ya hijabu hadi nashawishika akistaafu huko 2035 nikajaribu bahati yangu ).

SASA SWALI LANGU ni kwamba lau tatizo la kizunguzungu lingemshika MPAMBE WA RAIS wangefanyaje au ni nani angeshika nafasi yake wakati muhusika anaenda kupumzika?!
 
ADC siyo mlinzi wa Rais kwahiyo ingetokea kwake ingekua haiathiri chochote.
 
ADC siyo mlinzi wa Rais kwahiyo ingetokea kwake ingekua haiathiri chochote.
Ila tunaona kila anapokuwa rais lazima ADC awe nyuma yake , na nimeona mh rais anapokuwa nje ya nchi hupewa mpambe anayetokana na jeshi la nchi aliyotembelea yaani kama vile rais haruhusiwi kusimama peke yake!
 
Ila tunaona kila anapokuwa rais lazima ADC awe nyuma yake , na nimeona mh rais anapokuwa nje ya nchi hupewa mpambe anayetokana na jeshi la nchi aliyotembelea yaani kama vile rais haruhusiwi kusimama peke yake!
Hebu leta picha inayoonyesha akiwa nje ya nchi amepewa ADC mwingine
 
2035 jaribu bahati yako Mkuu mangine hutayajua huko huko


Nako na series day of jackal yaani mpambewa rais au ADCb sijui malipo Yao na kazi zao ndo zile billion 371 za matumizi yasiyo na tija . Charles Cathrop aka Jackals akiamua kudungua kichwa Ile anadungua vizuri Tu.
 

Attachments

  • IMG_20250411_175641.jpg
    IMG_20250411_175641.jpg
    60.9 KB · Views: 31
Umeleta mapema mkuu mngebishana bishana kidogo mtukanane mpigwe na ban ya wiki halafu mkirudi ndo mnaleta picha sasa wewe kubishiwa kidogo tu tayari picha hiyo hapo!, tena unasema ulete nanyengine!.. Imekuwa laini sana!..😂
Na wewe nakuletea ya kwako hii hapa! 😄😄😄
 

Attachments

  • images(64).jpg
    images(64).jpg
    14.8 KB · Views: 25
Umeleta mapema mkuu mngebishana bishana kidogo mtukanane mpigwe na ban ya wiki halafu mkirudi ndo mnaleta picha sasa wewe kubishiwa kidogo tu tayari picha hiyo hapo!, tena unasema ulete nanyengine!.. Imekuwa laini sana!..😂
Mtoa mada amekasirika akaamua aue Kila kitu mapema tuu
 
Mimi haya mambo nayajua huna haja hata yakunielimisha wakati haya mambo tulishajadili humu ndani toka zamani sana!
Nimekuelewa. Kuna baadhi ya watu wengine hupenda kubishana kwa jambo ambalo hawajalifanyia japo uchunguzi wa kawaida usiohitaji kutumia akili nyingi. Sasa mimi huwa nawafunga midomo mapema tu!
 
Mimi haya mambo nayajua huna haja hata yakunielimisha wakati haya mambo tulishajadili humu ndani toka zamani sana!
Kwakuwa haya mambo unayajua naomba unisaidie uelewa au mtu mwingine yeyote mwenye majibu anisaidie kama ifuatavyo:.
Siku za hivi karibuni kuna habari zilienezwa mitandaoni kuwa mh rais kampandisha cheo mpambe wake kutoka kuwa kanali na kuwa brigedia jenerali.
Lakini habari zikasema pia kwamba kwakuwa huyu afande Mashauri kapanda cheo kwa taratibu za kijeshi hatoendelea kuwa mpambe wa rais bali atapangiwa majukumu mengine!
Sasa wasiwasi wangu ni kuwa tangu habari hizi ziandikwe muda umepita na sijaona kuwa mpambe wa rais kabadilishwa !.
Sasa sijui habari hizi hazikuwa na ukweli, au taratibu za kijeshi zilizotajwa ndio hazipo , au ADC alibadilishwa ila mimi ndio sijui tafauti ya ADC mpya na yule ADC wa zamani?!
Kwa yeyote anayejua anielimishe kwani mimi ninapouliza swali kuhusu jamno fulani huwa sijui kweli hivyo naomba kuelimishwa tafadhali!.
 
Back
Top Bottom