Je inawezekana kumfungulia mtu kesi ya jinai na ya madai

turbocharger

Member
Dec 14, 2016
52
67
Habarini wanajukwaa siku si nyingi nimekutana na changamoto ya wafugaji kuvamia shambalangu na kuharibu mazao pamoja na bwawa langu la samaki. Nilifanikiwa kuripoti polisi na baada ya siku mbili niliwatia nguvuni kwa ushirikiano na polisi kesi ipo mahakamani na bado sijafunga ushahidi wangu lakini kwa uelekeo mtuhumiwa anaweza akafungwa.

Nia yangu ni kulipwa madhara yaliyotokana na uharibifu kabla mtuhumiwa hajafungwa Je ninaweza kufungua shauri la madai yaani civil huku kesi ya jinai ikiendelea? Kama jibu ni ndio je kifungu kipi kinanipa haki hiyo au precedent yoyote ya kitu kama hicho. Msaada tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kesi ya jinsi ikiisha n.a. kutiwa hatiani kwa mshitakiwa unaweza kufungua shauri la madai ya fidia.

Sababu ni adhabu atakayopewa ya faini au kifungo haina tija sana kwako.

Kufungua shauri la madai ya fidia utadai hasara uliyoingia.n.a. gharama zingine.Fidia ilitolewayo shauri la jinai ni kidogo Saana mahakama hukadiria tu.

Kifungu hakina maana sana kwani mahakama/wakili watashughulikia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani ina wezekana, mfano kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu,, hiyo ni jinai, sasa unafungua madai ya kiasi cha pesa alicho chukua,,, hapo na dhani ndivyo ilivyo,, sorry, sio mwanasheria kitaaluma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Soma section 68 ya Interpretation of Laws Act. Soma na kesi zifuatazo:

BDULLAH RAMADHANI V. ASINATE KIMOMWE [1969] HCD 24

RAMADHANI HASSANI V. RAMADHANI IDDI [1972] HCD 129

Hivyo vitakupa mwanga na majibu pia
 
Back
Top Bottom