bacha
JF-Expert Member
- Aug 19, 2010
- 4,282
- 797
Habari zenu wote wapendwa...........................
Rafiki wa dada yangu amekuwa akilalamika hivi majuzi kuwa mume wake,
amekosa uungwana/upendo na uvumilivu. Huyu dada pamoja na kuwa anaishi mbali na mume wake kutokana na majukumu ya kazi, lakini amekuwa akiisaidia sana familia kwa kugharamia matumizi yote ya nyumbani kuanzia chakula, matibabu, usafiri na mambo yote muhimu ya kimaisha.
Sasa amekuja kugundua kuwa mume wake anatembea na mwanamke mwingine,na isitoshe huwa anamleta mpaka hapo nyumbani. Mara baada ya huyu dada kugundua hayo aliona ni bora asitishe kupeleka fedha nyumbani, ukichanganya na hasira kidogo aliyokuwa nayo basi ndo hivyo tena. Pamoja na haya yote bado mumewe amekuwa ni mtu wa kumletea dharau sana na maneno yasokuwa na heshma. Lakini kwa jinsi huyu bwana asivyokuwa na haya, anazidi tena kumpigia magoti mkewe ili atume pesa za matumizi hapo nyumbani!
wanajamii,Je huu ni uungwana kweli?
Rafiki wa dada yangu amekuwa akilalamika hivi majuzi kuwa mume wake,
amekosa uungwana/upendo na uvumilivu. Huyu dada pamoja na kuwa anaishi mbali na mume wake kutokana na majukumu ya kazi, lakini amekuwa akiisaidia sana familia kwa kugharamia matumizi yote ya nyumbani kuanzia chakula, matibabu, usafiri na mambo yote muhimu ya kimaisha.
Sasa amekuja kugundua kuwa mume wake anatembea na mwanamke mwingine,na isitoshe huwa anamleta mpaka hapo nyumbani. Mara baada ya huyu dada kugundua hayo aliona ni bora asitishe kupeleka fedha nyumbani, ukichanganya na hasira kidogo aliyokuwa nayo basi ndo hivyo tena. Pamoja na haya yote bado mumewe amekuwa ni mtu wa kumletea dharau sana na maneno yasokuwa na heshma. Lakini kwa jinsi huyu bwana asivyokuwa na haya, anazidi tena kumpigia magoti mkewe ili atume pesa za matumizi hapo nyumbani!
wanajamii,Je huu ni uungwana kweli?