Mr Bean.
Senior Member
- Jan 25, 2015
- 185
- 133
Wadau,
Nimekuwa nikijiuliza mara kadhaa bila kupata majibu sahihi. Ni matumaini yangu humu jamvini wamo wataalam wa mambo mbalimbali.
Ninachotaka kujuzwa ni kuhusu haya maeneo na hasa viwanja vya mpira. Utasikia kiwanja kinaitwa kwa jina la CCM. Vipo viwanja kadhaa hapa nchini na Majumba kadhaa na Maeneo kadhaa ya wazi utasikia pia hata eneo fulani la wazi linaitwa kwa jina la ccm.
Swali langu, Je ni kweli CCM ndiyo walijenga hivyo viwanja vyote tunavyosikia ni mali ya CCM? Je, ni kweli CCM inamiliki kihalali maeneo ya wazi wanayochezea watoto? Je, ni kweli CCM inamiliki kihalali majumba na kumbi za starehe tunazozijua? nk.
Naomba nijibiwe lakini si kiushabiki wa chama tafadhali.
Nimekuwa nikijiuliza mara kadhaa bila kupata majibu sahihi. Ni matumaini yangu humu jamvini wamo wataalam wa mambo mbalimbali.
Ninachotaka kujuzwa ni kuhusu haya maeneo na hasa viwanja vya mpira. Utasikia kiwanja kinaitwa kwa jina la CCM. Vipo viwanja kadhaa hapa nchini na Majumba kadhaa na Maeneo kadhaa ya wazi utasikia pia hata eneo fulani la wazi linaitwa kwa jina la ccm.
Swali langu, Je ni kweli CCM ndiyo walijenga hivyo viwanja vyote tunavyosikia ni mali ya CCM? Je, ni kweli CCM inamiliki kihalali maeneo ya wazi wanayochezea watoto? Je, ni kweli CCM inamiliki kihalali majumba na kumbi za starehe tunazozijua? nk.
Naomba nijibiwe lakini si kiushabiki wa chama tafadhali.