Je, hizi ndio tabia za wanawake?

Je, hizi ndio tabia za wanawake?

kwetumasoko

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2016
Posts
866
Reaction score
517
Wakuu

Leo ni miaka nane imetimia toka niachwe na mke wangu, nasema ni mke wangu kwa sababu hakuna talaka yoyote tuliyopeana kisheria kuivunja ndoa yetu na kwa muda wote huo nimekuwa nikimbembeleza sana ili arudi tulee familia imeshindikana.

Sababu za kuniacha hazikuwa na msingi wowote, kwani alidai kuwa aliambiwa na rafiki zake kuwa nina uhusiano na dada mmoja, hivyo akaamua kuchukua uamuzi huo. Ukweli ni kuwa huyo ambaye nilituhumiwa kuwa na mahusiano naye wala nilikuwa simfahamu, nikamwambia alete ushahidi, ilishindikana zaidi ya maneno tu kuwa aliambiwa.

Nilijaribu kuwaomba wazee wamsihi na vikao vya ukoo vilifanyika lakini ilishindikana, juhudi zangu zote ziligonga ukuta, na hivyo kuwalazimu ndugu waniambie kama naweza kupata mwanamke mwingine, nioe.

Kwa muda wote huo nimeishi peke yangu nikiwa na wanangu, namshukuru Mungu kwa sasa wameshakua. Mmoja alimuacha akiwa na miaka 6 na sasa ana miaka 14 na mwingine alimuacha akiwa na miaka 3 na sasa ana miaka 11.

Huyo mke wangu, sasa yapata miaka sita imepita sijamtia machoni pangu, ila nasikia tu yupo mkoa fulani.

Wanajamii, nimeshindwa kuoa mwanamke mwingine kila nikifikiria mateso ambayo wanaweza kupata wanangu kutoka kwa mwanamke mwingine. Kila nikifikiria tu manyanyaso ambayo wanapata watoto wengine ambao wanalelewa na mama tofauti akili yangu inapoteza network kiasi kwamba hata sitamani kuoa tena.

Najiuliza, pengine hizo ndo tabia za wanawake wote au ni baadhi tu ambao kwao upendo umewapita mbali.

Naombeni ushauri waungwana!
 
Kwa umri uliokaa na hao wanao nafikr uendlee kuish nao tu we mwenyewe
 
Hongera kwa kuwa multipurpose yaani baba apo apo mama..... Sio kazi ndogo
 
Kaka acha kuishi kwa mazoea na mambo ya kufikirika. Wapo wanawake wanaweza kutesa watoto wa kambo na wapo wasiotesa

Hivi huyo mama yao mzazi si ndio mama yao wa Damu kabisa? Mbona hana huruma nao na amekuwa tayari kuwatesa kwa kuwaacha wataabike na wewe peke yako? Kama formula ni mama mzazi kupenda watoto na mama wa kambo kutesa watoto, mbona kwako haijafanya kazi hiyo formula?

Acha maisha ya endelee, huyo mama hakukupenda na alishaendelea na maisha yake kwann unambembeleza kwa miaka 8?

Acha hivyo jamaa, tafuta mama mwenye maadili, mwenye upendo oa akusaidie watoto hao
 
Wakuu

Leo ni miaka nane imetimia toka niachwe na mke wangu, nasema ni mke wangu kwa sababu hakuna talaka yoyote tuliyopeana kisheria kuivunja ndoa yetu na kwa muda wote huo nimekuwa nikimbembeleza sana ili arudi tulee familia imeshindikana.

Sababu za kuniacha hazikuwa na msingi wowote, kwani alidai kuwa aliambiwa na rafiki zake kuwa nina uhusiano na dada mmoja, hivyo akaamua kuchukua uamuzi huo. Ukweli ni kuwa huyo ambaye nilituhumiwa kuwa na mahusiano naye wala nilikuwa simfahamu, nikamwambia alete ushahidi, ilishindikana zaidi ya maneno tu kuwa aliambiwa.

Nilijaribu kuwaomba wazee wamsihi na vikao vya ukoo vilifanyika lakini ilishindikana, juhudi zangu zote ziligonga ukuta, na hivyo kuwalazimu ndugu waniambie kama naweza kupata mwanamke mwingine, nioe.

Kwa muda wote huo nimeishi peke yangu nikiwa na wanangu, namshukuru Mungu kwa sasa wameshakua. Mmoja alimuacha akiwa na miaka 6 na sasa ana miaka 14 na mwingine alimuacha akiwa na miaka 3 na sasa ana miaka 11.

Huyo mke wangu, sasa yapata miaka sita imepita sijamtia machoni pangu, ila nasikia tu yupo mkoa fulani.

Wanajamii, nimeshindwa kuoa mwanamke mwingine kila nikifikiria mateso ambayo wanaweza kupata wanangu kutoka kwa mwanamke mwingine. Kila nikifikiria tu manyanyaso ambayo wanapata watoto wengine ambao wanalelewa na mama tofauti akili yangu inapoteza network kiasi kwamba hata sitamani kuoa tena.

Najiuliza, pengine hizo ndo tabia za wanawake wote au ni baadhi tu ambao kwao upendo umewapita mbali.

Naombeni ushauri waungwana!
Hongera pia bora aliondoka...
Huenda ukakutana na kubwa zaidi ya kuachiwa watoto...
Baadhi ya hawa kina mama zetu huitikia sana maneno kutoka nje....
Jiulize mama anawezaje kumwacha mtoto wa miaka mitatu...?
 
Kaka acha kuishi kwa mazoea na mambo ya kufikirika. Wapo wanawake wanaweza kutesa watoto wa kambo na wapo wasiotesa

Hivi huyo mama yao mzazi si ndio mama yao wa Damu kabisa? Mbona hana huruma nao na amekuwa tayari kuwatesa kwa kuwaacha wataabike na wewe peke yako? Kama formula ni mama mzazi kupenda watoto na mama wa kambo kutesa watoto, mbona kwako haijafanya kazi hiyo formula?

Acha maisha ya endelee, huyo mama hakukupenda na alishaendelea na maisha yake kwann unambembeleza kwa miaka 8?

Acha hivyo jamaa, tafuta mama mwenye maadili, mwenye upendo oa akusaidie watoto hao
Nashukuru kwa ushauri mkuu, lakini mi naona kwangu wapo mikono salama zaidi kuliko angekuwa nao yeye, ingawa kuna baadhi ya mapenzi wamekosa kutoka kwa mama
 
Hongera pia bora aliondoka...
Huenda ukakutana na kubwa zaidi ya kuachiwa watoto...
Baadhi ya hawa kina mama zetu huitikia sana maneno kutoka nje....
Jiulize mama anawezaje kumwacha mtoto wa miaka mitatu...?
Ndo hivi mkuu, najiuliza hivi hawa akina mama wote ndivyo walivyo au ni baadhi tu
 
Ndo hivi mkuu, najiuliza hivi hawa akina mama wote ndivyo walivyo au ni baadhi tu
Ingekuwa wote ungekuta wanajamvi wote wanalia...

Wenye tatizo kama lako ni wengi ila wameamua kuweka maji mdomoni....

Kuna jamaa aliachiwa wa mwaka tena na ada ya mwanamke akawa analipa sasa mtoto ana miaka mitatu
 
Waswahili wanasema kila bahati mbaya ina heri yake
 
Wakuu

Leo ni miaka nane imetimia toka niachwe na mke wangu, nasema ni mke wangu kwa sababu hakuna talaka yoyote tuliyopeana kisheria kuivunja ndoa yetu na kwa muda wote huo nimekuwa nikimbembeleza sana ili arudi tulee familia imeshindikana.

Sababu za kuniacha hazikuwa na msingi wowote, kwani alidai kuwa aliambiwa na rafiki zake kuwa nina uhusiano na dada mmoja, hivyo akaamua kuchukua uamuzi huo. Ukweli ni kuwa huyo ambaye nilituhumiwa kuwa na mahusiano naye wala nilikuwa simfahamu, nikamwambia alete ushahidi, ilishindikana zaidi ya maneno tu kuwa aliambiwa.

Nilijaribu kuwaomba wazee wamsihi na vikao vya ukoo vilifanyika lakini ilishindikana, juhudi zangu zote ziligonga ukuta, na hivyo kuwalazimu ndugu waniambie kama naweza kupata mwanamke mwingine, nioe.

Kwa muda wote huo nimeishi peke yangu nikiwa na wanangu, namshukuru Mungu kwa sasa wameshakua. Mmoja alimuacha akiwa na miaka 6 na sasa ana miaka 14 na mwingine alimuacha akiwa na miaka 3 na sasa ana miaka 11.

Huyo mke wangu, sasa yapata miaka sita imepita sijamtia machoni pangu, ila nasikia tu yupo mkoa fulani.

Wanajamii, nimeshindwa kuoa mwanamke mwingine kila nikifikiria mateso ambayo wanaweza kupata wanangu kutoka kwa mwanamke mwingine. Kila nikifikiria tu manyanyaso ambayo wanapata watoto wengine ambao wanalelewa na mama tofauti akili yangu inapoteza network kiasi kwamba hata sitamani kuoa tena.

Najiuliza, pengine hizo ndo tabia za wanawake wote au ni baadhi tu ambao kwao upendo umewapita mbali.

Naombeni ushauri waungwana!
Usioe tena
 
ufafanuzi tafadhari:
Alinikataa sasa ananihitaji
Thread by: kwetumasoko, Sep 20, 2016, 43 replies, in forum: Mahusiano, mapenzi, urafiki
Wakuu wana forum hii,
Habarini za leo,
Kuna msichana mmoja nilimpenda sana na ni muda mrefu nilikuwa nikimfuatillia ili tuwe wapenzi na hatimaye tuoane ili tujenge familia lakini cha ajabu aliniambia kuwa yeye ana mpenzi na kamwe hawezi kumwacha kwa sababu ndiye atakayemuoa na anampenda sana. Nikaona isiwe shida nami nikawa nimekata tamaa.
Sasa ni miaka minne imepita, naona anaanza kunifuatilia na kujaribu kuwa karibu nami, ingawa mpaka sasa bado sijaoa.
Naombeni ushauri juu ya huyu binti!
cc:kwetumasoko
 
Kaka me cjaoa ila kutokana na hali kama hyo haina haja ya kurisk kutafut mwanamk mwingin aje akulelee wanao, Sawa sikatai kwamb sio wanawak wote ndo wenatabia hizo ila tatizo linakuja Nani ndiye Nani siye sasa huon kwamb hyo ni risk. Nimewaza sana umemkuza mtoto toka miak 3 had 11, bila mama aje akushinde 11 kuendelea mtu ameshakua kabic, sikushaur bro lea wanao haina haja ya kucheza Kamar kutafut limwanamke lingine. Bora wangekua na alama kwamb huyu n mzur huyu ni mbaya. Komaa lea wanao wala hutobadilika chocht kile na mungu akutie nguvu na ujacri katika hilo. One day utajivunia juu ya hilo
 
Oa mwingine mkuu, si wenzako hata mke awe mpole au mtaratibu bado tunaoa na nyumba ndogo.

Hakuna siku bila usiku na Mchana mkuu,
Ili maisha yako yawe murua fanya hivyo wala hutokuja kulalamika huku.

Dawa ya mwanamke ni mwanamke mwenzake.
Yeye kadhani kakukomoa lakini kajikomoa mwenyewe. Mwanaume haachwi bali yeye ndiye huacha, Shida ni kuwa mnadhani mliumbwa kwaajili ya wanawake na kusahau yakuwa wao ndio waliumbwa kwaajili yetu.

Kuwa Mwanaume ni jambo kubwa saana, Ukiikosa sifa hii hata upewe mali na utajiri wote wa dunia bado utakuwa dhaifu. Sasa wewe unashindwa jambo kama hilo.
 
Pole kwa madhira yalikukuta ila kitu cha msingi ni kwamba wanawake wote hawafanani kitabia kama ilivyo kwa muonekano kama umeona ni wakati muafaka wa kuoa tena basi fanya hivyo
 
Back
Top Bottom